Vituo vya Yatima (Orphanages) ni biashara ya utumwa

Vituo vya Yatima (Orphanages) ni biashara ya utumwa

FaizaFoxy

Platinum Member
Joined
Apr 13, 2011
Posts
100,246
Reaction score
123,145
Hata bila ya kuchunguza kwa kina, ukitazama kijuujuu tu utaelewa kuwa vituo vya kulelea Yatima ni biashara ya kujipatia kipato wanaoendesha vituo hivyo.

Vituo vyote vya Yatima vina asilimia 1 au 0 ya yatima kweli. Vingi vimejaa watoto waliopatikana kwa njia haramu (watoto wa zinaa na uasherati).

Pia utakuta humo watoto wa familia masikini zilizorubuniwa kuwa watoto wao watalelewa vizuri na kupelekwa shule. Wapo na wale wa wazazi waliogombana au kutorokana wakamwachia ulezi mzazi mmoja, anaposhindwa kulea peke yake, njia ya mkato ni kumpeleka mtoto au watoto kwenye kituo cha "yatima".

Kwa kuwa vituo vya "yatima" biashara yao ni kujipatia kipato kupitia huruma za watu wanaopeleka misaada na sadaka zao huko, vituo hivyo havikatai mtoto wa aina yoyote vile, mradi wao watoto wawepo ili biashara yao ifane.

Wanaoendesha vituo hivyo, hawajali lolote kuhusu hao watoto, wapo tayari kuwauza wakati wowote kwa wale waliokosa bahati ya kuzaa au hata kwa watu wenye kuharibu watoto (paedophiles).

Jamii, hususan serikali inatakiwa ichunguze kwa kina vituo vya "tatima" vyote, haijalishi ni vya kidini au binafsi. Vyote havifai kabisa kuwepo.

Nashauri wabunge wapeleke muswada bungeni, kama inabidi hivi vituo viwepo basi vitungiwe sheria zitazokua na manufaa na zitazowalinda hao watoto.

Tujadili.
 
Vingi vimejaa watoto waliopatikana kwa njia haramu (watoto wa zinaa na uasherati).
Hizi dini/Imani zinatuharibia sana utu, unawezaje kumuita binadamu mwenzako kuwa ni tunda/zao la uasherati? Hivi Kuna mtu anaependa azaliwe kwa njia hio? Kote nakubaliana na wewe Ila kwa hii statement, HAPANA aiseeee!

Mbegu au hatua ya kuzaliana huwa hainaga hizo Habari za zinaa au uasherati! MUNGU ndio anayeruhusu Uumbaji utokee. Shukrani
 
Vituo vyote vya Yatima vina asilimia 1 au 0 ya yatima kweli. Vingi vimejaa watoto waliopatikana kwa njia haramu (watoto wa zinaa na uasherati).
Hakuanaga watoto haramu regardless wamezaliwa katika mazingira yapi, binadamu ni binadamu tuu.

Acha kukufuru wewe bibi, hata wewe huwezi jua huenda mama yako alibakwa au alichepuka nje ya ndoa ndiyo ukazaliwa wewe.
 
Vituo vyote vya Yatima vina asilimia 1 au 0 ya yatima kweli. Vingi vimejaa watoto waliopatikana kwa njia haramu (watoto wa zinaa na uasherati).


Jaalia kwa wanandoa wenyewe ndoa halali (kidini) na kabla ya jimai walikula na kunywa vitu vya haramu vilivyopelelea mbegu za uzazi tengenezezwa kwayo, akipatikana mtoto hapa tunasema ni mtoto wa haramu.

Mtoto ambae ni zao la zinaa anaweza kuwa si mtoto haramu. Rejea makabrasha yako.

Pia, hata wewe unaweza ukawa ni mtoto harama ikiwa wazazi wako walikula na kunywa vya haramu kabla ya jimai.
 
Majjipolo

Hiyo definition yako ya mtoto "harama" ni fikra zako tu.

"Mtoto wa haramu' ni yule anaepatikana nje ya ndoa. Elewa kuwa hapo inamaanisha baba na mama yake walifanya haramu, uzinzi au uasherati nje ya ndoa halali. Waliofanya haramu ni wazazi sio mtoto aliyepatikana.

Mada ni vituo vya "yatima" sio uharamu na uhalali wa watoto isipokua nimeona nikuweke sawa tu.
 
Huyu bibi leo mmeshuka nae jumla jumla hadi raha.

Hakuna mtoto haramu asee.... Wako huku watu wakiwa watoto walitelekezwa na kukulia kwenye orphanages, leo asome uzi kama huu aone wanam-term kama mtoto haramu, inauma sana asee.
Mtoto wa haramu' ni yule anaepatikana nje ya ndoa. Elewa kuwa hapo ina maanisha baba na mama yake walifanya haramu, uzinzi au uasherati nje ya ndoa halali. Waliofanya haramu ni wazazi sio mtoto aliyepatikana.

Mada ni vituo vya "yatima" sio uharamu na uhalali wa watoto isipokua nimeona nikuweke sawa tu.
 
Mtoto haramu ndo Nini wewe mjinga Sana FaizaFoxy aFoxy

Haramu Ni wazazi na sio mtoto
Mtoto wa haramu' ni yule anaepatikana nje ya ndoa. Elewa kuwa hapo ina maanisha baba na mama yake walifanya haramu, uzinzi au uasherati nje ya ndoa halali. Waliofanya haramu ni wazazi sio mtoto aliyepatikana.

Mada ni vituo vya "yatima" sio uharamu na uhalali wa watoto isipokua nimeona nikuweke sawa tu.
 
Vingi vimejaa watoto waliopatikana kwa njia haramu (watoto wa zinaa na uasherati).

Mpuuzi sana wewe, imani yako isikufanye ukose utu kwa mtoto asie na kosa. Toa hukumu yako kwa mzazi na si mtoto asie na hatia
Wewe unaonesha huelewi hata unachokisona, wapi hapo kwenye mada kalaumiwa mtoto au kabezwa mtoto?
 
Hakuanaga watoto haramu regardless wamezaliwa katika mazingira yapi, binadamu ni binadamu tuu.

Acha kukufuru wewe bibi, hata wewe huwezi jua huenda mama yako alibakwa au alichepuka nje ya ndoa ndiyo ukazaliwa wewe.
Mtoto wa haramu' ni yule anaepatikana nje ya ndoa. Elewa kuwa hapo ina maanisha baba na mama yake walifanya haramu, uzinzi au uasherati nje ya ndoa halali. Waliofanya haramu ni wazazi sio mtoto aliyepatikana.

Mada ni vituo vya "yatima" sio uharamu na uhalali wa watoto isipokua nimeona nikuweke sawa tu.
 
Back
Top Bottom