Utotole
JF-Expert Member
- Oct 28, 2010
- 6,607
- 4,263
Kuna huyu binadamu anaitwa Redondo ndiye alinifanya nipende sana mpira
Unamaanisha vitu kama hivi?
Last edited by a moderator:
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kuna huyu binadamu anaitwa Redondo ndiye alinifanya nipende sana mpira
Nipishe Mimi Huna Unachokijua, Nenda UKAUKWEKE Ukalale.
ungekuwa unatutajia na majina mkuu ungetusaidia sana
Hiyo ya kina Pele,didi,revelino,gari ncha ni kikosi cha brazil mwaka 70 kinachukua ndoo kwa kumfunga Italy, wanakwambia hakuna kikosi bora cha brazil kana hicho bila kumsahau tostao.
umemtaja hussein marsha alikuwa pamba kisha simba.
ukasahau method mogella alikuwa simba kisha yanga.
Athumani china kiboko ya hamis gaga unamkumbuka?
Marcos Senna España, Makelele.
artulo vidal yuko njema sana
Duuh!! Huyu hata sikuwahi kumsikia.Nimependa sana uchezaji wake anapiga mashuti ya mbali kama Claudio Marchisio.
Mkuu, huyu kwenye mashindano ya dunia mwaka 2006 alikuwa anatoka mwanzo katika wachezaji 11. Aliwashangaza wengi sana kwani pale katikati hata akina Iniesta na Xavi ilibidi tu wamuache afanye kazi chafu zote. Ulikuwa pale katikati humpiti kirahisi kama siyo kwa MBINDE.
Mwaka 2008 wakati Spain wanashinda kombe la Ulaya, Senna aling'ara sana.
Alikuja akaumia mguu na hiyo ikawa imempoteza na akabaki kucheza ligi ndogondogo tu. Too sad.
The Brazil-born midfielder is happy to do the dirty work for his team, as Spain dream of their first trophy in 44 years. Senna steals show | Football | The Guardian