Viwanda vya kuunda mabasi vilazimishwe kuzalishia mabasi Tanzania

Mkuu, hii ya kusema hatujafika hizo level haina afya, mbona tulikuwa na kiwanda cha kuunda body za Scania Kibaha?

Au mbona tulikuwa na kiwanda cha kutengeneza matairi cha General Tyre Arusha.

Nakataa mtu ukisema hatujafika level hii, tulitakiwa tuwazidi Kenya na Uganda kwenye hili la kuunda mabasi na by products zake.

Twatakiwa kumpata mbia kwa mfano kutoka China ambao wao sasa wamehamia kwenye EV ambae ataunda mabasi na kutuachia teknolojia yake tukimlipa ada.

Au Ulaya kutoka nch zile ndogondogo kama Hungury ambao nao wana viwanda vya kuunda mabasi watupatie wataalam wa kutufundisha kuunda mabasi kisasa, huo ndo ushirikiano wa kistratejia.

Hivyo tutaweza kuunda mabasi kwa muda wetu na kwa kutumia vijana wetu waso na ajira.
 
Haiwork kwa style iyo tajiri. China anaproduce toothpick kwa less than 50tshs per pack . Bongo tutazalisha kwa zaidi ya 300 the same pack.

Why?
1. Labour cost zetu bado ziko juu sana as compared na wenzetu.
2. Capital cost zetu ni kubwa. Gharama ya Kupata mtaji hapa ni kubwa kiasi kwamba, ni lazima bei ya bidhaa iwe juu kurudisha gharama za mtaji.
3. Market size...
 
Ukisoma vizuri comment yangu Assembly tunaweza na kuna viwanda vya Assembly hapa.

Ila kuunda from scratch si kazi ya kitoto, Nchi zenye uwezo huo unazihesabu kwa mkono,
 
Ndio mkuu.

China waweza hivyo kwasababu ya kukua kwa teknolojia kani ni hiyo teknolojia ndo yawawezesha kupunguza labour cost kwenye production na capital pia.

Usisahau China ana zaidi ya watu bilioni 1 kwa soko la ndani pekee hivyo kwa market size atatushinda.

Sisi twapaswa kuhakikisha vijana wetu majasusi wanakuwa kila sekta na kwenye sekta ya viwanda wanakuwa wakisaka aina mpya ya ubunivu ambao utatuwezesha kutengeneza bidhaa zilezile lakini kwa bei nafuu tukitumia teknolojia ambayo tayari mchina ameachana nayo.
 
Iphone ilikuwa inatengenezewa wapi! Leo inatengenezewa wapi!

Kitu/price nitakayolipa ni Tabaka la Kati na juu litanipiga vita na litashawishi wananchi wawaunge mkono na watawapata wajinga wengi......maana sitaweza kusupply bidhaa nitakazozipiga ban kuingizwa nchini.

Nchi zinazozalisha hizo bidhaa nazo zitanipiga vita.....lakini hii itadumu tu kwa miaka mitatu minne.....na nitachagua nchi chache za kunegotiate nazo kwa akili saana...moja wapo ni China.

Niamini mkuu hakuna siku tutakuwa na uchumi imara kama hatutazalisha atleast 60% ya tunavyotumia. Tutalia na rushwa wee ....mwisho wa siku no production umaskini utatuua.

Sheria za kulinda viwanda vya ndani lazima ziwe makini..... mimi huwa najiuliza kama makampuni makubwa kama Toyota yalipewa support na serikali yakaanguka mara kibao serikali zetu zinashindwa nini hata kufund viwanda vya kutengeneza Diapers? Tuna nguvukazi imejazana kibao mitaani na vyuoni bado tunafundisha vijana maelfu theories Kisha wanajazana mitaani kupiga soga???
 
Diapers zipo nyingi Tanzania, kuna viwanda vingi mno to the point Unweza sema kuna oversupply
 
Diapers zipo nyingi Tanzania, kuna viwanda vingi mno to the point Unweza sema kuna oversupply

Diapers zipo nyingi Tanzania, kuna viwanda vingi mno to the point Unweza sema kuna oversupply
Nimeziona hasa za Drafco ila sikutegemea hadi tuwe na oversupply maana ma- Supermarkets yetu na maduka ya Mangi zimejazana Mapampers mkuu?
 
Nimeziona hasa za Drafco ila sikutegemea hadi tuwe na oversupply maana ma- Supermarkets yetu na maduka ya Mangi zimejazana Mapampers mkuu?
Kama una ingia kwa kishua ndio, ila huku Kkoo kwa vya bei rahisi zipo, kama Bumpies juzi juzi hapa walikua wana "brag" wana wafanyakazi 1,000.

Issue ni quality, mtoto akilala usiku usipombadilisha asubuhi lazima godoro limerowa kidogo.
 
Kama una ingia kwa kishua ndio, ila huku Kkoo kwa vya bei rahisi zipo, kama Bumpies juzi juzi hapa walikua wana "brag" wana wafanyakazi 1,000.

Issue ni quality, mtoto akilala usiku usipombadilisha asubuhi lazima godoro limerowa

Kama una ingia kwa kishua ndio, ila huku Kkoo kwa vya bei rahisi zipo, kama Bumpies juzi juzi hapa walikua wana "brag" wana wafanyakazi 1,000.

Issue ni quality, mtoto akilala usiku usipombadilisha asubuhi lazima godoro limerowa kidogo.
Unadhani kwamba hawana teknolojia ya kutengeneza quality nzuri au wanajua fika nani ni mteja wao na wakiitengeneza diapers ya quality nzuri hawawezi kushindana na brands zingine!! I don't know am just asking.!
 
Mabasi gani yanatoka Kenya miaka ya Leo? Yutong, higher, zhongtong yote ni Mchina.
 
Unadhani kwamba hawana teknolojia ya kutengeneza quality nzuri au wanajua fika nani ni mteja wao na wakiitengeneza diapers ya quality nzuri hawawezi kushindana na brands zingine!! I don't know am just asking.!
Targeted market mkuu inataka vitu vya bei rahisi, ila pia elimu, na culture yetu ya "mawinga" inasababisha hivi.
 
Matrekta yanaunganishwa Kibaha. Vyupi kutoka China si kigezo cha kutokuhamasisha ujenzi wa assembly plant ya mabasi ikawepo Tanzania. Hata Marekani wanaagiza notebooks kutoka China pamoja na kuwa wana viwanda vikubwa.
kila kitu mnatolea mfano Marekani....hv mnajionaje? Nasemaje, pimeni tako zenu wenyewe kisha mtengeneze vyupi vyenu wenyewe kwanza, mnategemea mchina akadirie ukubwa wa misambwanda ya wake zenu kisha awashonee chupi, yatawafika ya kuwafika.
 
Changamoto kubwa ni fikra tegemezi kuanzia kwa wananchi hadi viongozi.
Kwa kukua kwa teknolojia ya mawasiliano ilivyo sasa, tunatakiwa kushawisi watu wetu waige na kutengeneza vitu vingi sana badala ya kuwapa wageni kipaumbele.
Hoja yako ya kuwalazimisha watengenezaji haiwezelani na ni ya hovyo kwa sababu biashara ni huria.
 
kila kitu mnatolea mfano Marekani....hv mnajionaje? Nasemaje, pimeni tako zenu wenyewe kisha mtengeneze vyupi vyenu wenyewe kwanza, mnategemea mchina akadirie ukubwa wa misambwanda ya wake zenu kisha awashonee chupi, yatawafika ya kuwafika.
Naamini kuna nati kidogo zimelegea hapa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…