Viwanja vyote vilivyomilikishwa kimakosa kupigwa mnada ili Serikali ipate hela

Viwanja vyote vilivyomilikishwa kimakosa kupigwa mnada ili Serikali ipate hela

Mung Chris

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2017
Posts
3,391
Reaction score
3,849
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi ametanza rasmi kuanzia July 01 2021, kuanza kwa zoezi la Kitaifa la uhakiki wa umiliki wote wa ardhi kwa kutumia kitambulisho cha NIDA kwa Nchi nzima.

“Tunataka Wamiliki wote hewa waliomilikishwa kimakosa, kiwizi, kiutapeli na kiujanja lazima tuwabaini lazima tujue kwa nini jina lako la kiwanja halifanani na majina ya hati yako ulipataje, tukiwabaini waliomilikishwa kimakosa viwanja vyao tutavipiga mnada ili Serikali ipate hela"
 
Hapa kuna watu watapata hasara ya hatari!
Wengi watapata tabu pia kwa sababu wana utajiri wa ardhi usio na maelezo ambapo itasababisha wahojiwe chanzo cha utajiri utajiri huo...
Afadhali umeliona hilo
 
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi ametanza rasmi kuanzia July 01 2021, kuanza kwa zoezi la Kitaifa la uhakiki wa umiliki wote wa ardhi kwa kutumia kitambulisho cha NIDA kwa Nchi nzima....​

Hii ni mbinu ya kutaka kuwanyang'anya viwanja masikini wawape mabwana zao matajiri! Ngoja mtaona utekelezaji wake.
 
Hapa kuna watu watapata hasara ya hatari!
Wengi watapata tabu pia kwa sababu wana utajiri wa ardhi usio na maelezo ambapo itasababisha wahojiwe chanzo cha utajiri utajiri huo...
Nchi masikini ndo ufikiria kuhoji utajiri wa mtu badala ya kuangalia mchango wake upi kwenye mzunguko
 
HII NI MBINU YA KUTAKA KUWANYANG'ANYA VIWANJA MASIKINI WAWAPE MABWANA ZAO MATAJIRI! NGOJA MTAONA UTEKELEZAJI WAKE.
Sio kweli! Kinachotafutwa na serikali ni kila mtu amiliki mali ambazo zinatambulika kwa jina lake na ziwe kwenye rocord ili kuepusha wenye hela za ujanja ujanja kukwepa mkono wa serikali.

Kumbuka wenye hela zisizo na vyanzo vya kueleweka wanapenda kuzificha kwa kununua majumba na viwanja... Fikiria umefanya dili haramu ghafla ukapata milioni 200, utazipeleka Bank kwa maelezo gani? Lazima ukimbilie kununua viwanja nk
 
Nchi masikini ndo ufikiria kuhoji utajiri wa mtu badala ya kuangalia mchango wake upi kwenye mzunguko
Nani alikwambia nchi zilizoendelea hawahoji utajiri usioeleweka?

Ukiona tajiri fulani kwenye nchi zilizoendelea hahojiwi kuhusu utajiri wake, jua tajiri huyo anapewa baraka zote na serikali yake kwa dili zake haramu anazofanya.
 
Sio kweli! Kinachotafutwa na serikali ni kila mtu amiliki mali ambazo zinatambulika kwa jina lake na ziwe kwenye rocord ili kuepusha wenye hela za ujanja ujanja kukwepa mkono wa serikali...
Sasa kama umenunua kiwanja na hati unayo una makosa gani? Una maana wanatoa pesa zao kununua Ardhi halafu hawapewi hati kwa majina yao?
 
Serikali ya awamu ya 5 itakumbukwa kwa uhodari wake wa kufanya uhakiki usokwisha.

Sent from my SM-A505F using JamiiForums mobile app

Wanatumia fedha za walipa kodi hovyo bila mpango matokeo yake kila leo wanawaumiza wananchi na kodi zisizoeleweka na hazina uhalali!!! We angalia tu jinsi wanavyobadili passports na leseni za magari na vitambulisho vingine; kila leo wanabadilisha ili mradi wawakomoe wananchi kutoa vijisenti vyao!!
Hii yote inatokana na kuwa na miradi ambayo serikali haijui gharama zake mpaka hapo itakapokamilika!!! Wanabakia kubahatisha bahatisha tu.
 
Sasa kama umenunua kiwanja na hati unayo una makosa gani? Una maana wanatoa pesa zao kununua Ardhi halafu hawapewi hati kwa majina yao?





Una viwanja au nyumba tofautitofauti maeneo ya nchi lakini hujawahi kuwa na kazi au biashara iliyokuwezesha kununua viwanja hivyo au nyumba hizo, hujarithi kutoka kwa wazazi wako wala hujawahi kubet ukashinda hizo hela au ulikuwa na biashara kubwa tu iliyokuwa ikikuingizia faida ya kuweza kununua hivyo vitu bahati mbaya ukawa hulipi kodi hivyo serikali ilikuwa haikutambui.
lazima utafilisiwa tu!

Unapokuwa na utajiri basi uwe na maelezo ya kuweza kuonesha namna ulivyoupata utajiri huo
 
Back
Top Bottom