VoA: Tanzania imepokea mkopo kutoka kwa Korea Kusini na kutoa sehemu ya bahari na madini

VoA: Tanzania imepokea mkopo kutoka kwa Korea Kusini na kutoa sehemu ya bahari na madini

Mimi nalia na Mwanzilishi wa Taifa hili.Aliliacha Taifa na katiba mbovu.Maamuzi makubwa ya nchi yanaamuliwa na Mtu mmoja .USA mkenya alipewa kuwa Rais(Obama) walijuwa kuna mifumo thabiti ya kulinda mali asili zao.
 
The way forward is to warn those would be investors kuwa haya yanafanyika bila ridhaa ya watanzania, kesho tutawafukuza maana wameletwa na swaiba wao na si watanzania

Najua mikataba ya kimataifa si rahisi kuivuja, but let the International community know this. Give them a warning , Wanaharakati/wanasheria wanaweza kuitaarifu dunia kuwa anachokifanya Samia hakina ridhaa ya watanganyika.

Unavunja mikataba kwa kuwaongezea kodi na kutoweka mazingira sio rafik ya ufanyaji kazi wao
 
Mbona ni suala la muda tu na tena hata sio muda mrefu kuanzia sasa tutaifikia debt limit kisha kitakachobaki itakuwa ni kulipa tu madeni...

Mbaya zaidi kwa wakati huo hata miradi yote ya kimaendeleo italazimika kuendeshwa na kodi zenu nyie nyie wanainchi maana hakuna tena kukopesheka na hapo hapo nyie ndio wa kulipa hayo madeni na wakati huo inflation inazidi kupaa tu... manina hapo lazima mama yenu akawauze hata kwa waarabu huko apate hela ya kupunguza madeni
Nasema watajiju
 
PHD kwa masuala ya anga kwa lipi hasa alilolifanya, hivi hizi phd ni za kuomba au ukionekana unapenda basi wanakuelekezea hukohuko ili utegeke kiahisi wapenyeze maslahi yao, nauliza zina impact gani kwa Taifa. hivi Nyerere angekuwa anazipenda angepata ngapi? vituvingine visivyo na tija visitushughulishe.
 
Tanzania na Ethiopia zimesaini mikataba kadhaa na Korea Kusini kwa ajili ya kupata mikopo ya mabilioni ya dola kwa ajili ya maendeleo.

Mikopo hiyo itaiwezesha Korea Kusini kupata fursa ya kuchimba madini muhimu katika nchi za Afrika.

Korea Kusini imeandaa kongamano na viongozi 30 wa nchi za Afrika, ikiwemo Tanzania na Ethiopia.

Kongamano linafanyika wiki hii

Tanzaia imesema kwamba itakopa dola bilioni 2.5 kutoka kwa Korea Kusini katika muda wa miaka mitano ijayo. Mkopo huo utalipwa katika muda wa miaka 5.

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan vile vile amesaini mkataba utakaoiruhusu Korea Kusini kutumia bahari yake na madini yanayotumika katika teknolojia ya nishati safi kama Nickel, Lithium na Graphite.

Ethiopia nayo imesaini mkopo wa dola bilioni 1 utakaolipwa katika kipindi cha miaka minne kwa ajili ya ujenzi wa miundo mbinu, sayansi na teknolojia, afya na maendeleo ya mijini.

PIA SOMA
- Ziara ya Rais Samia Korea Kusini atasaini Mkopo wa Tsh. Trilioni 6.51

- Prof. Kitila Mkumbo akanusha masharti ya Mkopo wa Korea Kusini

Voice of America
For sale.
 
Back
Top Bottom