Vodacom Premier League 'VPL' Simba SC dhidi ya Polisi Tanzania, Rekodi Ya Alama 50 Kuwekwa Leo

10' Polisi wanatafuta namna ya kupenya ngome ya Simba huku wakipata kona 3 ambazo hazikuzaa bao

Simba SC 0-0 Polisi TZ
 
Kweli pesa ni sheitwani!!yaan leo naishabikia simba kisa tu nmeweka ka 50000 kangu!!kubet ni zaidi ya kazi walahi!!!simba piga haoo[emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
20' Free Kick kuelekea Polisi, baada ya Kahata kufanyiwa faulo huku mchezaji wa PT akionyeshwa kadi ya njano

Inapigwaaaaaa, inaokolewa

Simba SC 0-0 Polisi TZ
 
22' Go go Goooooooooal, Polisi wanaandika bao la kwanza kupitia kwa Sixtus Sabilo

Simba SC 0-1 Polisi TZ
 
Golikipa wa PT yupo chini, ameamka inapigwa Kona kuelekea PT, inaondoshwa
 
34' Simba bado wako nyuma ya bao moja huku PT wakionekana kutakata eneo la kati

Simba SC 0-1 Polisi
 
Nikisema mashabiki wa Soka la Bongo wengi ni Wapumbavu naonekana nina dharau.

Angalia mashabiki wa Simba uwanjani wanavyowafanyia wachezaji wao uwanjani.
 
39' Kwake Chama, anakwenda sasa katikati ya Uwanja, apigaaaaaa Shutiiiii, lakini golikipa anadaka bila wasiwsi
 
Leo Simba hakuna kitu kabisa. Kushinda ni bahati.
 
45+2' Kona Inapigwaaaaaa na Kahata, lakini wanashindwa kutumia nafasi ile na golikipa kuudaka

Wanakwenda sasa PT, ni faulo chini chini kuelekea Simba lakini wanapoteza

Naaaaaaam mpira ni Mapumziko

Simba SC 0-1 Polisi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…