Vodacom Premier League 'VPL' Simba SC dhidi ya Polisi Tanzania, Rekodi Ya Alama 50 Kuwekwa Leo

Vodacom Premier League 'VPL' Simba SC dhidi ya Polisi Tanzania, Rekodi Ya Alama 50 Kuwekwa Leo

Timu imezidiwa kocha hajui na wala haelewi anachokifanya Simba inacheza mpira utadhani ni Mlalapua Rangers
 
45+2' Kona Inapigwaaaaaa na Kahata, lakini wanashindwa kutumia nafasi ile na golikipa kuudaka

Wanakwenda sasa PT, ni faulo chini chini kuelekea Simba lakini wanapoteza

Naaaaaaam mpira ni Mapumziko

Simba SC 0-1 Polisi
Mkuu mbona kama tumeshikwa kiaina na hawa jamaa, tukipoteza mpira kwenye half yao wanakimbia sana kuelekea kwetu mpaka naona kuna hatari kubwa, wana kasi mno katikati
 
Ili tushinde hii mechi inabidi tuwapoteze PT kwenye eneo la katikati.
 
Wana Simba tujiandae Kisaikolojia huenda Mchezo huu wa leo ukawa mgumu Kwetu na tukakoswakoswa Kufungwa na tukatoka Sare. Siku ya leo kidogo Kinujumu / Kinyota Kwetu imekaa vibaya. Tukishinda basi itakuwa ni Furaha Kwetu lakini nasisitiza tuwe makini na hii Mechi ya leo.
Kumbe mara nyingi GENTAMYCINE unakuwa sahihi kuwatukana baadhi ya wapuuzi wasiokuelewa. Nimeshangaa kwenye comment yako hii umezungumza jambo la msingi sana, na mimi kama Mwanasimba mwenzio nimekuelewa ila kuna mazwazwa kadhaa wameishia kukukejeli. Sasa imedhihirika kuwa ULIKUWA SAHIHI na WALIOKUKOSOA NDO HAWANA WALIJUALO.
 
Kipindi cha pili kinakaribia kuanza huku taa za uwanja zikiwa haziwaki baadhi ya sehemu

Naaaaam kipute kimeanza...Ametoka Shiboub ameingia Ajibu
 
57' Bocoooooo Goooooooooooooooooooaaal

Simba SC wanasawazisha bao kupitia kwa Papaa John Boco, baada ya movie kali kuelekea lango la polisi

Simba SC 1-1 Polisi
 
Back
Top Bottom