Vodacom Premier League 'VPL' Simba SC dhidi ya Polisi Tanzania, Rekodi Ya Alama 50 Kuwekwa Leo

Vodacom Premier League 'VPL' Simba SC dhidi ya Polisi Tanzania, Rekodi Ya Alama 50 Kuwekwa Leo

Patashika ya Ligi Kuu Tanzania Bara Vodacom Premier League VPL, kuendelea tena leo February 4, 2020 ambapo, Simba SC, Wekundu wa Msimbazi, wanawakaribisha Maafande wa Polisi Tanzania, mchezo utakaopigwa kwenye dimba la Uwanja wa Taifa.

Mchezo wa leo ni wa kufunga mzunguko wa kwanza kwa timu zote mbili, unatarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua kwa muda wote wa dakika 90.

Simba SC katika mechi 4 zilizopita ameshinda zote huku Polisi Tanzania wakishinda mechi 3 na sare moja hivyo Simba SC, ambao ndo Vinara wa VPL wakiwa na alama 47 wanaingia dimbani wakiwa na lengo la kuvuna alama tatu muhimu ili Kuweka Rekodi Ya Kufikisha Alama 50, kwa mzunguko huu wa kwanza wenye timu 20.

Kocha Msaidizi Suleiman Matola amsema ligi ni ngumu na hakuna mechi ndogo hivyo wamejiandaa kupambana kama walivyopambana katika mechi zilizopita wakiwa na lengo la kushinda ili kujiimarisha pale juu kwenye msimamo.

Naye Kocha Msaidizi wa Polisi Tanzania Ally Mtui, anasema mchezo utakuwa mgumu hasa ukizingatia wapinzani wao kutopoteza mechi nyingi hivyo wanaangalia namna ya kufanya ili kuweza kushinda mchezo huo.

Kumbuka mechi ni kuanzia saa 1:00 usiku, Usikose Ukaambiwa..!

...Line Up Angalia Kwenye Post #20.View attachment 1346355View attachment 1346356

Wana Simba tujiandae Kisaikolojia huenda Mchezo huu wa leo ukawa mgumu Kwetu na tukakoswakoswa Kufungwa na tukatoka Sare. Siku ya leo kidogo Kinujumu / Kinyota Kwetu imekaa vibaya. Tukishinda basi itakuwa ni Furaha Kwetu lakini nasisitiza tuwe makini na hii Mechi ya leo.
 
Utabiri wa kijinga
Wana Simba tujiandae Kisaikolojia huenda Mchezo huu wa leo ukawa mgumu Kwetu na tukakoswakoswa Kufungwa na tukatoka Sare. Siku ya leo kidogo Kinujumu / Kinyota Kwetu imekaa vibaya. Tukishinda basi itakuwa ni Furaha Kwetu lakini nasisitiza tuwe makini na hii Mechi ya leo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asalaam Tanzania, ligi kuu Tanzania VPL kuanza hivi punde..!

Vijana 22 kuumana uwanjani ndani ya dakika 90

Naaaaaaam mpira umeanza Uwanja wa Taifa kusaka alama tatu muhimu karibu sanaaaaaaaa

00' SIMBA SC 0-0 POLISI TZ
 
05' jaribio la kwanza langoni mwa Polisi, lakini golikipa anatokea na kudaka
 
Back
Top Bottom