Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)


Ulipoanza Kuutumia Mtandao wa Vodacom ulituambia ( ulitushirikisha ) hadi leo hii unauhama rasmi ndiyo unatushirikisha hivi?
 
 
Vodacom now nawashitaki mahakamani kwanini umeniibia salio langu LA simu Mara kadhaa Kwa kuniunga kwenye huduka ambazo sijawahi hata kufikiri kurequest nizitumie? Kama huu ushuzi mlio anzisha uitwao UNSUB?

Hakika mmezoea sasa tutakutana mahakamani Kwa fidia ....nimechoka na usumbufu huu

Vyuma vimekaza harafu hivi hivi mnanyakua visalio Kwa vihuduma vya ajabu ajabu.....hivi Mimi MZEE wa miaka 47 UNSUB ya nini? Harafu ndiyo nini? Hata maelekezo hakun...

Nandaa malalamiko

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole sana mzee
 
Tarehe 24/02/2020 niliamisha pesa kutoka M-Pesa kwenda kwenye M-Pesa MasterCard ili niweze kufanya malipo kiasi Cha TZS 35,000/= lakini akikuweka kwenye M-Pesa MasterCard na pesa ilikatwa katika account yangu ya M-PESA. Nikawasiliana nao mara ya kwanza wakanipa pending paka masaa 72 itakuwa tayari, yakasisha hakuna matokeo, nitawasiliana nao Tena wakaniweka pending paka Masaa Tena 72 hakuna matokeo nitawasiliana nao mara tena nikawaambia basi wasitishe huo muamala tu pesa iludishwe kwenye account yangu ya Mpesa wakasema hiyo haiwezakani. Wakanambia tena nisubiri tena masaa 72.

Yamekamilika leo paka sasa hakuna Pesa iliyowekwa kwenye M-Pesa MasterCard au kurudishwa kwenye account yangu ya M-Pesa.

Je, kuna mwanaJF ambaye alishakutana na changamoto kama hii na alifanyaje tushee kidogo mawazo juu ya hili. Mpaka nimeshapoteza imani sasa ya kutumia M-Pesa MasterCard. Bora kutumia card za bank. Sijawahi pata upuuzi kama huu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kweli hata mimi imenitokea mara kadhaa na juhudi za kuongea na customer care hazikuzaa matunda sasa nimeachana nao.
Hapo Vodacom Tanzania namba ya huduma kwa wateja ni majanga, wanataka mufanye mawasiliano kwa mitandao ya kijamii au kuna menu chache za sauti ambazo kuna matatizo kibao hayapo kwenye category za menu zao, sasa ilitakiwa uongee na mhudumu moja kwa moja haupati nafasi hiyo.

Nabaki najiuliza hawa vodacom hawajui kuna watu wengi wapo vijijini na vitochi hawawezi kutumia hiyo mitandao ya kijamii.
Na kuna wengine wanapiga simu huku wanaendesha gari (wamevaa head set au wanatumia hands free mode), kutokana na mazingira hayo hawawezi ku-chat huko kwenye mitandao ya kijamii.

Sijui hapo Vodacom kaingia kiongozi mbongo au wamejaa wabongo vitengo vyote?
 
Vodacom mna shida gani?Huku kasulu niliko hakuna intanet siku ya 4,inaonekana E tu!Nini kinaendelea?
 
Huduma kwa wateja kwa kupitia namba 100 ipo ovyo kweli. Haitupatii kile mteje unaitaji au kutarajia unapopiga. Maelezo na maelekezo hayatoshelezi kutatua shida tulizo nazo, iki mlicho fanya sio uboreshaji ni kuaribu.
 

Ahsanteni kwa hii PAGE. Kuna wizi sasa hivi umejitokeza kwa MAWALA WA M-PESA. Sasa sijui na wao wanajua hama lah! Jana kuna ndugu yangu kaenda kwa WAKALA kutoa pesa, akaomba namba ya WAKALA akapewa na yule WAKALA, Baada ya kuingiza Namba ya WAKALA na kufanya utaratibu wote wa kutoa pesa, jina likaja la yule WAKALA. Ndugubyangu akamuuliza WAKALA kuwa jina lako unaitwa ERICK KIMALIO? WAKALA akajibu ndiyo. Na ndo jina lake.

Baada ya hapo akathibitisha kutoa pesa. Ila tu baada ya kuthibitisha jina likaja jingine na Namba ya WAKALA nyingine na siyo ya yule ERICK KIMALIO.

Tumeangaika sana kuwapigia simu ila ikashindika kupata msaada. Kuna mda tulipiga simu kwa kutumia Simu yangu, Dada mmoja muhudumu wa VODACOM akatuambia tumsomee Namba ya risiti ya Muamala aliyofanya, tukamsomea akasema kuwa huo Muhamala haupo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
tumechoka kulalamika kila siku, maoni yetu na ushauri wetu haufanyiwi kazi, ni kama mumetuchoka tuna hasira sana na iko siku tutafanya maamuzi magumu
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…