Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Mtandao wenu hapa Kinyerezi upo chini sana, kupiga simu ni kwa shida, internet ndio kabisa huwezi kufanya chochote. Njoni mshuhudie wenyewe kwani nimekuwa natoa taarifa hizi mpaka nimechoka sasa imebidi niwahame. Ukiwa Kinyerezi mwisho ukielekea kaskazini mashariki kilometa 1 tu unapoteza mawasiliano. Kwanini msijenge mnara eneo hili? Kitu gani kinawashinda, mbona tigo, airtel wote wana minara eneo hili. Chukueni hatua, mnapoteza sana wateja eneo hili
Habari Franakim, tumeshawasilisha suala hili kwa mafundi wetu kwa utatuzi. Tunaomba radhi kwa usumbufu unaojitokeza.
 
Hili la VODA KUKATAA kuweka bando ya SH 1000 (INTERNET BILA KIKOMO) WAKATI HIYO PESA IMO INASHANGAZA KWELI
Habari Gamba, hili hutokea endapo mteja ametumia Intaneti bila kuwa na kifurushi na ameacha pages ziko wazi kisha anajaribu kujiunga na kifurushi, katika hali hii inakuwa kwamba simu inasync mtandaoni hivyo salio hilo hilo haliwezi kukubali kujiunga. Anachotakiwa kufanya ni kuhakikisha amefunga pages zote au kufunga huduma za Intaneti ''Mobile Data'' ajiunge kisha afungue baada ya kununua kifurushi. Ahsante
 
Vodacom Tanzania kama mtu ameweka mia tano kwenye simu ikatokea kwamba hiyo miatano amekwata bila yeye kuitumia je? hiyo hela hurundishwa.

asanten san
 
Last edited by a moderator:
kwanini kuunga kifurushi cha mitandao yote kinasumbua sana hata kams salio lipo utaambiwa halipo hivi kweli mmejipanga kweli .
 
Habari Franakim, tumeshawasilisha suala hili kwa mafundi wetu kwa utatuzi. Tunaomba radhi kwa usumbufu unaojitokeza.

mbona hapa ihanda -mbozi hatupati internet ya uhakika pia tigo wana 3g network lakin vodacomo ni edge tu hebu tusaidieni hili wateja wenu tigo wanawapiga bao.
 
Kwanza nianze kwa kuwapongeza kwa kujitokeza ktk jamiiforum kujua matatizo/changamoto zinazowakabili kupitia maoni yetu sisi wateja.
Nipo Rungwa, wilaya manyoni. Sisi hapa tunatumia mnara ambao ni kero kubwa sana kwa kweli. Mawasiliano hukutika na kupotea kabisa mara nyingi kipindi cha mvua. Ila tangu jana aubuhi saa 12 mawasiliano yamekatika kabisa hadi sasa hivi ninapowandikia hii taarifa. Pia hata kama mtandao upo, basi mawasiliano ni shida sana, kiasi kwamba kuelewana na unayewasiliana naye ni taabu. Tumeshazoea kuongea kwa sauti kubwa hapa Rungwa kana kwamba labda unayempigia hakusikii vizuri kwa sababu ya sauti. Tafadhali sana Vodacom makao makuu mtusaidie kutatua hili tatizo maana ndio mtandao pekee hapa kwetu. Kazi njema
 
Ndugu mteja,

Una tatizo lolote unapotumia mtandao wetu? Una ushauri wowote ili tuiboreshe huduma yetu?

Tafadhali itumie mada (thread) hii ili tukusaidie kwa urahisi.

Unapokuwa na tatizo, ili tukusaidie kirahisi zingatia haya:

- Ni tatizo gani? (M-PESA, SMS, Calls, Internet, usajili, kukatika kwa mawasiliano n.k)
- Maeneo gani? (Tukifahamu location, inakuwa rahisi kukuelekeza wapi uende ili upate physical assitance toka kwa vendor wetu aliye karibu nawe)
- Tatizo limeanza lini na limejirudia au kuendelea kuwa kero kwako kwa muda gani?
- Kama ni ushauri, zingatia ya juu lakini tutafurahi tukijua kwanini unapendekeza unachopendekeza
- Kama ni pongezi, zingatia ya juu na tungependa pia upendekeze lipi tufanye kuzidi kuiboresha huduma kwako.

Karibu

Vodacom Tanzania

Nimelalamika mpaka nimechoka kusema sasa basi nyie bingwa
 
tunauliza maswali hapa mnajibu baadaya mwezi hii thread si muondoe tu ijulikane kuliko ubabaishaji
 
Kwanin msiweke alert ya kumjulisha mtu kama salio limeisha??? Na msilete siasa za haiwezekan..mbona tigo wanajulisha zikiwa zimebaki 2MB!!! Au nyie mnaleta UJAMBAZI TU??
wakuwekee alert wakose kukuibia?
 
Mbona hamuweki 3g mitambo Marangu wenzetu wa tigo wanatunyanyasa sana mpaka tunawaza kununua line za tigo sasa by the way Marangu ni centre ya kitalii fanyeni mipango hiyo maisha yawe ni murua..
 
Kuna tatizo kubwa la mtandao huku chuo kikuu cha dodoma hasa college ya humanities unaweza k utuma sms asubuhi mtu akaipata kesho yake je tatizo ni nini? Tunawaomba mfike na kulitatua kwani imekua ni kero kubwa sana
 
Ile bundle ya 5gb kwa mwezi ilikua very fast and efficient. This new unlimited thing is just not working.
 
Vodacom mtandao wa kijinga sana, kuanzia tarehe 1 naanza kutumia Tigo,maana nimehitaji huduma yao ya mpawa lakini sijafanikiwa utafikiri ni maombi ya kazi, nimepiga ccare, nimeenda kny maduka yao na nimetuma shida yangu kny ukurasa wenu hp JF. Nimeamua kubwaga manyanga.
 
jina: Frank john ngowi
tin:.116-495-104
lessen ya biashara:b01496459-namba ya stakacth 0178618
kitambulisho namba. D 0317653
store no: 072481
till no. 221135
mgt:221157

jina la wakala mkuu: Manyika ezekiel mboya (0762913448)

vilevile nilikuja vodacom mliman city tarehe 25/09/2014 huyo anaetumia line yangu akambiwa atoe fetha zake mpaka tarehe 1/10/2014 nirudi tarehe 4/10. Leo anapigiwa simu anasema hajapigiwa. Haki zetu ziko wap usoni mwa vodacom??

ref this msg
 
Nyie jirekebisjen yangu sa mmoja na dk kumi nimenunua umeme hakuna majibu y? Kkama
N km tigo unanunua umeme mesej inayorud ni token za umeme sio huu upuuz wenu wa muamala umetumw tanesko halafu baada ya wiki ndo mnarudisha hela?. Tigo ukiona habari za muamala ujue kunashida na hela inarejeshwa ili uendelee kujarib achen upuuz mnakaa na pesa yangu dakika arobain mnajua nlipoitoa rudishen nkaninue na Tigo pesa Nina mambo ya kufanya
 
Rudishen hela yangu nkatafte huduma kwingine kabla vibanda havijafungwA na Wapuuzi wenzenu tanesco hawajakata umeme nikashindwa kunyosha nguo za kaxini Masaa mawili yanakaribia ntawasue hamnipi Huduma na hela hamrudishi
 
Rudishen hela yangu nkatafte huduma kwingine kabla vibanda havijafungwA na Wapuuzi wenzenu tanesco hawajakata umeme nikashindwa kunyosha nguo za kaxini Masaa mawili yanakaribia ntawasue hamnipi Huduma na hela hamrudishi

Ha ha ha, naona wamekukwaza kweli mrembo.
 
Back
Top Bottom