Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Iv Vodacom Tanzania mbona mmekuwa Wezi kias cha Kunifanya nitupe Lain yangu ya Voda na Kuhamia Tigo?
Mb zenyewe za Mawazo..
Salio Mnaiba
M-pesa Bado nayo mnachakachua..


Niwatakien Wizi mwema!
 
Nimejiunga na kifurushi cha data cha mwezi unlimited, lakini baada ya kutumia MB 5120 naletewa ujumbe kuwa "Endelea kutumia kwa kasi ndogo hadi tarehe ya mwisho. Hivi nini maana ya unlimited?
 
Sina hakika kama na huku nako kama kutasikilizwa au ndio liwalo na liwe, labda mnamo tarehe 20.02.2015 saa sita mchana nilipiga simu kituo cha huduma kwa wateja na kupewa majibu mepesi mepesi na mtoa huduma kisha nikakatiwa simu huku akaunti yangu ikilambwa kiasi cha shilingi 100 kwa huduma mbovu mbovu, sikukata tamaa nikapiga tena simu kulalamika kwa mambo mawili, la kwanza sasa likiwa kukatiwa simu na mtoa huduma ninayechangia kumlipa mshahara na la pili likiwa tatizo langu la msingi, na la tatu ni kudai shillingi 100 niliyotozwa bila kupata huduma yeyote, jamaa akanipatia majibu kuwa watashughulikia yote ndani ya saa 24, kesho yake nikapigwa simu ya kutaka kujua km nimehudumiwa vizuri au la, nikasema la, nimekuwa nikifuatilia jambo hili kwa muda mrefu bila mafanikio yeyote sasa naomba mwongozo mtu wa kutatua au ndio mpaka TCRA?

Nimetoka kuongea na mtoa huduma mmoja hivi punde, kweli ni kichefu chefu wallahi
 
Wajameni Vodacom,

Waoneeni huruma watanzania. Mmeleta utapeli mwingine wa JAY Millions. Mimi ni mteja wenu, hebu nijulisheni hadi leo watanzania wangapi wamenufaika na promosheni hiyo? Kwenye tangazo mnasema kuna mshindi wa zawadi mojaya Sh. Milioni Mia moja 100,000,000.00 kila siku, washindi 10 wa Sh. milioni kumi kila siku 10,000,000.00 na washindi 50 wa milioni moja moja na washindi wa salio la elfu moja.

Naomba kujuzwa hadi sasa ni watanzania wangapi wameshinda Milioni mia moja, wangapi milioni kumi, na wangapi milioni moja? Mimi nakumbuka mshindi mmoja tu wa milioni mia moja kutoka Iringa. Cha kushangaza mshindi huyo ambaye alikuwa anafanya kazi ya kuuza baa, amehama alipokuwa anafanyia kazi lakini aliko sasa ni masikini wa kutupwa.

Hizo pesa alizoshinda mwaka jana zimeishaje katika kipindi kifupi hivyo?
 
Ombi: Wakazi wa Kata tatu za Malambo,Piyaya na Engarasero Wilaya ya Ngorongoro Mkoa wa Arusha tunaomba sana huduma yanu.Eneo husika lina wakazi wengi,Shule na Taasisi nyingi na ni eneo la Utalii pia.
 
Vodacom kiukweli wanachosha. Hasa huku vijijini kwetu, kitu kidogo wanakwambia mpaka uende voda shop.
 
Vodacom mtulaisishie uduma yakupiga sm voda kwenye mtandao yote tnz me nipo Mozambique na huduma akuna
 
Tunaomba kupunguza idadi ya SMS na kuongeza mb maana hatuna muda wa kuandika meseji ila tuna muda wa kuingia kwenye internet
 
Mbona sioni majibu mnayojibu walalamikaji na watoa maoni? Au na ukurasa huu ni geresha?
 
lini mtaacha wizi hasa wa salio .na mb siku hata aijawa serious mmeshafanya yenu dah
 
Mods, futeni tu hii thread maana haina maana yoyote. Hao Voda toka wameianzisha wala hawajitokezi kujibu malalamiko ya wateja yanayotolewa hapa.
 
Vodacom ni nini maana ya kifurushi chenu cha ulimited bundle kwa siku?
Nimejiunga na kifurushi cha ulimited bundle kwa siku sasa baada ya ku download nimepata msg kutoka Voda inanitaarifu kuwa nimebakiza Mb 700 tu niendelee ku surf mpaka muda utakapo expire.
sasa nauliza huu siyo udanganyifu kuwa mna vifurushi vya unlimited wakati u kweli ni kuwa mnalimit Mb zenu?
 
You have reached 700MB. Continue surfing at lower speed till expiry date. Monthly UNLIMITED internet bundle at Tsh. 25,000. To buy, dial *149*01#.
 
Du!! Voda mwenyewe yuko wapi? naona maswali tu majibu hamna hata mimi niltaka kuulza swali lkn naona wakujibu amelala
 
Nyinyi voda tatizo lenu ni pale nikijiunga na kifurushi kwa mfano cha wiki then kikiisha Kabla wiki haijamalizika siwezi kujiunga na kifurushi tena mpaka wiki imerizike hiyo kwangu inanikera sanaaaa
 
Acheni ubaguzi! Kwanini offer ya kifurushi cha university iwe mlimani tu; watanzania wote ni wamoja sambazeni vyuo vyote
 
Back
Top Bottom