Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Ninashida kuongea na huduma Kwa wateja namba 100 hakuna option hiyo
 
Vodacom nitafanya nirudushe namba ambayo sujatumia mwaka na nusu

Inaonekana bado ipo kwa jina langu ila imefutwa
 
Nimechoshwa na hizi sms zenuu! Hamuwezi kuona ni kero kea wateja!?

Na siko interested na hayo ma sms yenu! Mnaboa sana kila siku! Hamna wateja wengine wa kuwatumia tofauti na mm! Mda ule ule kila siku kama vile mmeniwekea alarm mm!?

Aka! Pesa fasta! Imekuwa pesa fasta! Mnaboa!
 
Vodacom Tz kuna nini. Mbona kitengo chenu cha Mpesa hakijibu malalamiko?.. Unaroa malalamiko kwa message kupitia huduma kwa wateja wanajibu watakupigia. Siku mbili unasubiri kimya. Kuna nini?.

Unaongea na huduma kwa wateja hujamaliza kuongea wanakata simu. Kunani VODACOM?.
 
Vodacom huu utaratibu mmezidisha sasa!

Mtu ananunua sms za mwezi labda 1000sms anatuma hata 50 mnatuma ujumbe eti umetumia 75%. Nilidhani ni kwangu tu lakini mtu leo kanitumia ujumbe kuwa hivi voda wamechanganyikiwa, nimenunua sms 300 natuma si zaidi ya 20 napokea ujumbe wa kutumia 75%.
 
Habari:
Nimewahi kupita nchi kadhaa, Vodacom inakuwa roam bila shida,Je Somalia mbona inakstaa kuunganisha na mtandao wowote, nahitaji kutumia huduma ya M-pesa huku pamoja na huduma nyinginezo,Je mta niwezesha Je kuunganisha.

Huku Mogadishu-Somalia?
 
Vodacom ni mtandao muhimu sana kanda ya ziwa.

Ziko kasoro MF:- Vifurushi kuwa ghali sana makato ya huduma za M Pesa na vifurushi vya data gharama juu data kidogo.Lekebisheni vutia toa huduma ya rafiki kwa mteja wengi wamebaki na huduma za kupiga na kupokea simu tu.
 
Hawa Vodacom nashindwa kuwaelewa kabisa leo hakuna huduma ya kuongea na mhudumu kabisaa duuu
 
Line yangu inaandika NOT REGISTERED ON A NETWORK tatizo nini ? nitatue vipi?
 
Mtandao wenu recently umekuwa slow sana, ile edge ya advantage mliyokuwa nayo dhidi ya wenzenu katika issue ya speed ya internet mnaipoteza, halafu siku hizi ilifika usiku saa sita kwenda mbele internet yenu haipatikani kabisa. Hivi nyie hamjui kuwa kuna watu wanatumia internet hadi usiku wa maneno kwa ajili ya research, business, na vikao na watu walioko upande wa pili wa dunia?
 
Hivi niwaulize vodacom. Huu utaratibu wakuturushia jumbe zinazohusu kamari
nikwanini msituulize kwanza?
wengine imani zetu haziruhusu.kiujumla mnaniboa saaaaana
 
Voda kipindi mnaanza mlikua safi sana.
Sasahivi sijui mmezidiwa wateja?sijui nipesa zimekua nyingi?sijui tatizo ni nini?
Eti voda imekua yakwenye lami tuu ukiiacha lami kilometa tatu voda kwaheri
 
Anaejua hili naomba anisaidie maana naona wahusika hawajibu!

naomba kujua maana ya hii namba, mfano:

pokea kiasi cha Tsh300,000.00 kutoka kwa 216803 BAHATI BAHATI (kwenye blue)
 
Vodacom wezi sana na simu mnazo uza kwa promosheni mkiahidi kuto GBs za bure mwaka mzima kumbe siyo kweli.

Jamani msinunue izo simu zinasumbua na hizo mb hamtapewa watakuzungusha tu wakikuambia nunua kifurushi cha kijiweni Mara tumia alfutatu hawana lolote zaidi ya wizi na ubabaishaji.
 
Back
Top Bottom