Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

voda - voda 8000 sec, voda kwenda mitandao mingine 300 sec. ..kwanimw usihamie airtel? Nilichelewa sana kujiunga na BABA LAO.


Zaidi ni kifurushi cha 7000 kwa wiki...

Unapewa sek 21000 kupiga voda kwenda voda na sek 420 mitandao yote...

Vodacom, kazi ni kwako.
 
Unadhani zile FEKON wanagawa akina Lwaigwanan Lowassa hela inatoka wapi? Kinachoniuma hela naibiwa na kodi hawalipi serikalini.
 
Unajiunga ktk promosheni zao, wanakuambia piga namba fulani kisha aidha ujiunge na cheka time au internate masaa 24, unaambiwa subiri ujumbe mfupi utajibiwa.

Unasubiri weee! Hakuna kitu, ukiangalia salio limekatwa! Na hakuna huduma hiyo wala nini! Ni kwa nini hamtuhurumii wateja wenu?
 
Vodacom wamekithiri ktk wizi...

1. Nilijiunga na kifushi cha Cheka, 7000 kwa wiki... Kesho yake kuangalia kifurushi kimekwisha.... Wakati sikutumia sana.

2. Ktk bango lao la kutoa na kutuma pesa kwa Mpesa wameandika kuwa, kutuma fedha kwa wateja wasiosajiliwa kutoka 400,000 mpaka 499,999 wanatoza 7000... Wiki iliyopita nilituma 490,000 wakanikata 7800.. Ikiwa ni ziada ya 800.

3. Kutuma pesa kwa wateja wasiosajiliwa, kutoka 20,000 mpaka 49,999 wanatoza 1,600... Nilituma 20,000 wakanitoza 1,800... Ikiwa ni ziada ya 200.

.
 
Mods unganisha na ule mwingine
Invisible
 
Last edited by a moderator:
Mimi nimeshaihama kabisa hawafai ni waizi kweli,na inasemekana ina mkono wa viongozi wengi sana na chama fulani cha siasa nacho kimo,mwisho wao unafika lakini,kipindi hiki watanzania wengi ni waelewa jamani na tunafuatilia mambo.
 
Vodacom wamekithiri ktk wizi...

1. Nilijiunga na kifushi cha Cheka, 7000 kwa wiki... Kesho yake kuangalia kifurushi kimekwisha.... Wakati sikutumia sana.

2. Ktk bango lao la kutoa na kutuma pesa kwa Mpesa wameandika kuwa, kutuma fedha kwa wateja wasiosajiliwa kutoka 400,000 mpaka 499,999 wanatoza 7000... Wiki iliyopita nilituma 490,000 wakanikata 7800.. Ikiwa ni ziada ya 800.

3. Kutuma pesa kwa wateja wasiosajiliwa, kutoka 20,000 mpaka 49,999 wanatoza 1,600... Nilituma 20,000 wakanitoza 1,800... Ikiwa ni ziada ya 200.

.

Voda ni majanga cku hz
 
Kuna wizi mkubwa kwa fedha za salio za wateja unaoendelea sasa hivi katika mtandao wa Vodacom.
Kwa vile hili si jungu bali ukweli nimisha report wizi huo katika kitengo cha malalamiko TCRA kwa hatua zaidi.

Nimeweka salio la Tsha 10,000 mchana wa leo kwa Mpesa ref Y23SY687 na baada ya muda mfupi nikakuta salio langu la maongezi ni sifuri.

Nikanunua vocha na kutumiwa tshs 10,000 na hela yote imekatwa tena.

Wateja wa Vodacom jihadharini, kuna mwizi kaingia mtandaoni Vodacom

.

Habari ndugu mteja,tunaimani tumeelewana kama tulivyozungumza kwa njia ya simu asubuhi ya leo hii,pole sana.
 
Kuna kitu nadhani watu wengi wanaolalamika kuwa wanaibiwa mnakosea. Kama unatumia smartphone na hujajiunga na bando la internet ni lazima pesa yako itaendelea kuliwa taratibu hadi iishe. Cha msingi kama wewe hutumii inernet nenda kwenye mobile network then iweke off! Otherwise applications ambazo zinafanyakazi katika background zitamaliza pesa yote.

Umesema kweli
 
bila shaka huyu ni m1 wao (mfanyakaz wa voda) anaandika utumbo tu tofauti na malalamiko ya wadau hapa.watch out wa2 wana machungu...

ungekuwa na machungu ungeshahama mtandao wewe? acha ufalaa!! kwanza unajua maana ya SMARTPHONE wewe? au unakurupuka tu unadhania kwa sababu na wewe una simu basi tunafanana?
 
...

...

...

UPDATE
=====
VODACOM wamefanya ustaarabu wa kunipigia baada ya kuona detail ya transaction hapo juu, na kuiona kwenye mtandao wa Jamiiforums.
Kimsingi wameapologise kwa mtafaruku uliotokea lakini wamenieleza nifike ofisini kwao kuona aian ya simu ninyotumia isije ikawa data apps ziko wazi.
Na kweli baada ya maongezi ya kuchunguza, mobile data setting ilikuwa ON, na mimeizima sasa.

Hata hivyo ni vema nitaenda kupata maelezo ya kuyeyuka kwa salio langu , karibu 20,000, kwa siku moja.
Wanabodi mtajulishwa inawezekana kuna wenye tatizo kama langu.

Hili ndilo la msingi, kumbe wanapitaga humu.

Sasa hiyo haitoshi, inabidi waweke na watu wao humu ili kama kuna kitu chochote tuwe tunawauliza. Tuna mengi sana ya kuwalalamikia hawa jamaa.
 
ofisi za zipo ubungo plaza wanafanya kazi kama ya kimahakama kuna kipindi niliwasilisha malalamiko tcra walichukua hadi miezi mitano hawajashugurikia

Ofisi za TCRA zipo Mawasiliano Towers Sam Nujoma Road !!!!
 
Mitandao yote ni wezi, kwani TCRA wameshindwa kuwabana, kazi yao wanajua kusafiri nje ya nchi kupata per diem!
 
Back
Top Bottom