Na wewe usiwe mjinga,aliyekuambia wakala mkuu anapanga commission ni nani!?? Commission unalipwa na kampuni ya simu moja kwa moja. Na kwenye hilo,wakala mkuu hana hata ushauri. Halafu hii ni biashara km biashara zingine tu,hulazimishwi kufanya. Mimi hiyo ni kazi,naendesha maisha. Na km unataka kuamini na kujifunza hii biashara inalipa njoo pm me nakupa number yangu,uje ofisini hata sasa hivi km unaishi dar. Mimi nauli nitakupa 10 elf ili uje hapa useme ukweli. Mkuu unapofungua biashara yoyote,lazima uzingatie location,kwamba hilo eneo hiyo bidhaa inahitajika! Wewe unashangaa mimi kupata milioni!?? Mwaka 2013 niliwahi kupata milioni 3 na laki 1 kwa mtaji wa laki 6. Hapo ilikuwa kabla hatujaanza kukatwa kodi ya zuio.