Voices From Within: Japo 2025 Tumepanga Twende na Mwanamke, 2025 Mama Akabidhi Kwanza Mwanamume, Kisha 2030 Ndipo Aje Mwanamke

Kama hujui katiba basi jifunze hata kwa historia, Rais wa Zanzibar anaweza kuwa hata makamu Bara achilia mbali urais wa JMT.
Ivi kwa mfano samia anaweza mfanya mwinyi wa zanzibar kuwa makamu wake ili hali bado ni rais wa zanzibar nikimaanisha anakuwa makamu bara na rais zanzibar kwa wakati mmoja ni swali tu nataka kufahamu?
 
Mbona unajikweza kiasi hiki ?


Bakwata ndio wenye hilo jukumu la kutangaza kuanza kwa mfungo au kumalizika kwake ili kuondoa mkanganyiko.
Sasa wewe aidha wafate au usiwafate, sisi inatuhusu nini? Sisi tunafta Qur'an inasema nini, wewe fata ujuavyo.


Kusema ukweli ndiyo kujikweza? Unanshangaza!
 
P pamoja kwamba wewe ni mtu wa mfumo vipi huogopi kuleta mada kama hizi maana madaraka ni matamu Sana na unaowaambia hicho kitu unadhani wanafurahi ingawa ni Cha kweli?Je hawawezi kuunganisha dots na wewe kujikuta unakua kwenye hatari ?
 
Ivi kwa mfano samia anaweza mfanya mwinyi wa zanzibar kuwa makamu wake ili hali bado ni rais wa zanzibar nikimaanisha anakuwa makamu bara na rais zanzibar kwa wakati mmoja ni swali tu nataka kufahamu?
Mkuu cabo , asante sana kwa swali hili, japo linaonekana kama ni swali lakijinga sana kwa sababu inatarajiwa kila Mtanzania ni lazima aijue katiba, the basics, kuwa rais akitokea upande mmoja wa muungano, VP ni lazima atoke upande mwingine. Samia ni rais kutoka Zanzibar hawezi kumteua Dr Mwinyi kuwa VP.

Ila tulipo ungana, Rais wa Zanzibar ndie VP wa kwanza, halafu PM ndie VP wa pili. Samia akiamua kumrudishia hadhi rais wa Zanzibar kwenye hii setup ya muungano, anaweza. Kwa sasa ndani ya set up ya muungano, rais wa Zanzibar is nothing,ni nobody!. Anaelezwa kuwa atateuliwa na Rais wa JMT kuwa Waziri asiye na Wizara maalum ili tuu aweze kuhudhuria cabinet meetings lakini ndani ya setup ya muungano rais wa Zanzibar is nobody!, na mpaka hapa ninapoandika, katiba ya JMT haitambui GNU, wala wale Makamo wawili wa kule, ila tuu wanatambulika ki protokali kwa heshima tuu. Hivyo sasa maadam Rais wa JMT ni kutoka Zanzibar, huu sasa ndio wakati muafaka kwa hadhi ya Zanzibar ndani ya muungano iwe restored, Katiba ya JMT iitambue katiba ya Zanzibar na ku ya adopt mabadiliko yake. Rais wa Zanzibar awe restored kuwa VP etc etc.
P
 
P pamoja kwamba wewe ni mtu wa mfumo vipi huogopi kuleta mada kama hizi maana madaraka ni matamu Sana na unaowaambia hicho kitu unadhani wanafurahi ingawa ni Cha kweli?Je hawawezi kuunganisha dots na wewe kujikuta unakua kwenye hatari ?
Mkuu Babe la mji , kweli madaraka ni matamu, ila haya mambo ya sauti sii yetu ni over and above us hivyo kuyasema ndiko kusaidia kwenyewe.

Kama JPM angejua he is a one term president kuna mambo angefanya vizuri zaidi kuliko alivyofanya. Kwa mujibu wa katiba yetu, urais wa JMT ni 5 year term with possibility to extend to a second term but not necessarily, ndio maana hata mimi ninasupport kabisa Watanzania, tuunge mkono 2025 ni zamu ya Mwanamke, ila sio lazima awe yeye bali yule aliyepangiwa na 'YEYE', kama ni yeye aliyepangiwa, then ni yeye!
ila unaposikia sauti fulani, sema ulichosikia, ili wenye masikio wasikie
P
 
Shida siyo Uzanzibari wau Uanamke wake, shida ni Uislam wake.

Nnakuhakikishia kila anaempinga mama humu basi utakuta sio Muislam.
Kwahiyo waisilamu hawakosei au ukiwa muislamu huoni ujinga unafanyika!?
Waislamu kama wewe ni majuha mwanzo mwisho, huko mitaani wanao
mpinga kuhusu tozo, mafuta, umeme nao ni wakristo tu!?
Ajuza umezeeka vibaya.
Wale waislamu waliotolewa madarakani egypt, tunisia na nchi za mashariki ya kati
walitolewa na wakristo!?
 
Sawa
 
Asante umebarikiwa kuwa na mungu asiyetaka mambo ya uchaguzi wa rais nchini Tanzania, huenda huyo mungu wako aliona wewe na kundi lako mmezoea kupiga vikumbo kura za wananchi.
Hongera endeleeni kugawana urais huku sisi tukiambulia umasikini uliokithiri, wenzetu walimpata Mungu anayewapa mawazo ya kuitoa nchi kwenye ufukara iwe na nuru nyie mnawaza kupeana urais miaka nenda miaka rudi mkiujenga umasikini.
 
2025 ni mbaal mno, Kwa mfano Nan aweza kutabiri Bei za mafuta kufika December 2022, tutanunua petrol Kwa sh ngap?? Busara itumimike mapema!!!!
 
Mambo ya Nchi ni magumu Sana ni zaidi ya tujuavyo,wachache Sana wanajua na wengi wetu tunaenda kwa mkumbo.Haya mambo hayatokei kwa bahati mbaya ni long term planed na Kuna watu walizaliwa waje watawale kwa Sababu unabii uko hivo na Kila mtawala anaekuja Kuna kazi yake anakuja kuifanya.

Kiunabii wa utawala wa Tanzania baada ya Nchi kutoka gizani ambapo tupo Sasa hivi inaonyesha huyu ajae ndo ataleta mwanga manake Kila kitu kizuri kwa ajili ya nchi hii huyu ndo atakua mtengenezaji wa mifumo yote ili hatiamae chi isimame kwa ajili ya maendeleo.

Ilishapangwa hivo na itakua na hakuna mtu wa kupinga Hilo .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…