Voices From Within: Je, wajua yuko Peponi, Mbinguni, Kwa Baba yake? Why kumshutumu, kumsakama na kumsimanga? Aachwe apumzike kwa amani

Voices From Within: Je, wajua yuko Peponi, Mbinguni, Kwa Baba yake? Why kumshutumu, kumsakama na kumsimanga? Aachwe apumzike kwa amani

This is your right. Nikiwa sekondari Tambaza, Mwalimu wangu wa siasa akiitwa Meela, alitufundisha, kwa vile hakuna aliyekufa akarejea duniani kutupa mrejesho kama ni kweli Mungu yupo au hayupo na mbinguni na peponi kupo, it's better to play it safe in order to be on a safe side.

If you believe Mungu yupo, ukifa ukakuta Mungu hayupo, you have everything to gain kwa kuishi kwa hofu ya Mungu and nothing to loose kwa kukuta hakuna Mungu.

Lakini ikiishi kwa kuamini hakuna Mungu, hivyo kuishi bila hofu ya Mungu, siku ukifa ukakuta Mungu yupo, you have everything to loose and nothing to gain!.
You better believe!
cc. Kiranga
P
This is one of the most ridiculous reason to believe in God.
 
This is one of the most ridiculous reason to believe in God.
Kama ilivyo haturuhusiwi kujiuliza kuhusu mwanzo wa Mungu, just God is Alfa and Omega. Vivyo hivyo, no ene needs and reason to believe God, mtu unazaliwa dini fulani, you just believe without any reason.
P
 
This is your right. Nikiwa sekondari Tambaza, Mwalimu wangu wa siasa akiitwa Meela, alitufundisha, kwa vile hakuna aliyekufa akarejea duniani kutupa mrejesho kama ni kweli Mungu yupo au hayupo na mbinguni na peponi kupo, it's better to play it safe in order to be on a safe side.

If you believe Mungu yupo, ukifa ukakuta Mungu hayupo, you have everything to gain kwa kuishi kwa hofu ya Mungu and nothing to loose kwa kukuta hakuna Mungu.

Lakini ikiishi kwa kuamini hakuna Mungu, hivyo kuishi bila hofu ya Mungu, siku ukifa ukakuta Mungu yupo, you have everything to loose and nothing to gain!.
You better believe!
cc. Kiranga
P
Kwani huyo Mwalimu wako ndiyo chanzo cha hii argument? Alibuni yeye? Hii ni Bertrand Russell ndiyo aliandika. Yaani wewe ni mjinga sana kwenye mambo mengi.
 
Kisayansi hakuna kitu kama roho au mtu kuwa na uwepo duniani baada ya kufa. Hiyo kitu hamna. Mtu akifa brain cells nazo zinakufa, na "mind" aliyokuwa nayo kwenye ubongo wake wakati anaishi nayo inakata. Bila ubongo hakuna "mind". Na ubongo ni cells zinakufa hata bado mtu yupo hai, achilia mbali akifa kabisa.
 
Labda pepo ya shetani🐒🐒🐒
16409521842520.jpg
 
Kama ilivyo haturuhusiwi kujiuliza kuhusu mwanzo wa Mungu, just God is Alfa and Omega. Vivyo hivyo, no ene needs and reason to believe God, mtu unazaliwa dini fulani, you just believe without any reason.
P
Kuamini hata ukiamini mavi yako ni Mungu, sawa tu, hiyo ni haki yako ya kikatiba.

Lakini ukija hapa JF na kuanza kusema kuna Mungu, na mavi yako ni Mungu, tuyale tupate uzima wa milele, hapo itabidi tukuhoji ututhibitishie.

Sasa, wewe unakuja kutupa mavi tule, halafu tukikuuliza imekuwaje mavi yawe Mungu, unatuambia tuamini tu?

Lazima tukuone una some loose nuts somewhere.

Amini Mungu yeyote unayemtaka, sitakubughudhi.

Ukishaanza kuhubirihubiri, ushajitoa kwenye faragha ya kuamini Mungu, umejiweka wazi kuthibitisha na ku justify Mungu wako yupo kweli.
 
Upo sahihi asilimia 100 kaka Pascal.. Mambo ya rohoni hayatazamwi kwa macho ya mwili na nyama.. Wewe umesikia sauti ya ndani.. Ila wenye Karama ya kuona mambo ya Rohoni wameahaona kitambo kuwa The Great JPM amepumzika mbinguni kwa Baba Mungu..
 
PASKALI nimesoma andiko lako kwa tafakuri kubwa sana! Unaweza kuwa sahihi kwa sauti yako ya ndani ambayo iko juu ya uwezo wako kuweza kui control.. Lakini tukija kwenye uhalisia wa maandiko kwa imani ya mhusika ni kwamba wafu bado hawajafika peponi bali wote wako kaburini wakisubiri kiama ama mwisho wa dunia ambapo kila mtu atapewa hesabu yake
Niliwahi kuandika hapa kwamba zana ya pepo/peponi na Jehanum kuzimu iko pale kaburini, kwamba wale waliotenda mema roho zao ziko pale zimelala kwa utulivu lakini wale waliotenda mabaya (kwa tafsiri yoyote ya ubaya) roho zao zinahamanika na kuhangaika huko na huko, hiyo ndio tafsiri ya kuzimu/jehanum

Kwa upande wa karma.. Hii sote tunajua haikopeshi.. Tendo kwa tendo ..ubaya kwa ubaya na wema kwa wema.. Hivyo inategemea nani anaamini kwenye nini ndio atamuweka mhusika huko..

Kuna hili la mizania ya haki.. Hili hupimwa kwa matendo ya mtu mabaya na mazuri..Asili ndio huhukumu., hapa si dini bali ni asili, asili itakuchagulia njia yako kutokana na maisha uliyoishi kabla ya kifo

Hapa kuna ishu ya uumbaji ambayo kupitia mikono yake kwa tafsiri yoyote ile uumbaji huo uliumia, uliteseka na pengine kudhulumiwa haki ya kuishi.. Hapa ishu ni zile sauti zinazolia na kusononeka kwa namna yoyote ile.. Hapa ndio muunganiko wa mizania ya haki na asili hutokea... Kuna vitu viwili ambavyo kiimani vinapaswa kutendewa kwa tahadhari kubwa mno navyo ni uumbaji/uhai na ardhi.. Kwa waamini vitu hivi tumeonywa tusivichezee..!

LA mwisho ni hili la kuonya wadau wasiendelee kumsakama marehemu kwakuwa tayari alishafanya kitubio na yuko peponi..brother sidhani kama maneno yao yatakuwa na athari zozote kwenye hili.. Japo sasa kama ni kweli bado hata baada ya kufa watu wanaendelea kumsema vibaya basi lazima tutambue kuna tatizo kubwa mahali kuhusiana na yeye..!
Mshana wanachelewa wapi kukupa PhD ya heshima wanapewa wajinga wajinga tu akina msukuma?
 
Wanabodi,

Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa huwaletea makala zangu za Kwa Maslahi ya Taifa. Mada ya leo ni a bit abstract, ambapo Nimesikia sauti ya Voices From Within ikiniambia JPM yuko Mbinguni kwa Baba, hivyo nauliza swali, jee wajua kuwa JPM yuko peponi, Mbinguni, Kwa BABA YAKE?

Why watu wengine waendelee kumshutumu, kumsakama na kumsimanga?. Kwa nini asiachwe ajipumzikie zake kwa amani!. Mtu ameisha tangulia mbele ya haki, kwanini watu waendelee kumsema sema kwa ubaya.

Mimi mwana jf mwenzenu ni Mzee wa Sauti za Ndani "the inner voice", unafanya kitu fulani na mara unasikia sauti from within ikikuambia jambo fulani.

Angalizo kuhusu Abstract Topics.

Issues na mtu akiisha kufa, we all knows what happens to the body, but roho huwa inakwenda wapi, no one knows for sure, hivyo tunategemea mafundisho ya dini zetu.

Kuna sisi dini za wana wa Nabii Ibrahim, Wakristo na Waislamu tumefunzwa kuhusu mbinguni, peponi, ahera, jehanam ya moto wa milele, na kuna siku ya mwisho siku ya hukumu ya mwisho ya kiama atakapo rudi Mwana wa Adamu, ambapo kutakuwa na ufufuko wa miili na uzima wa milele.

Kuna wenzetu wa Buddhism na Hindu ambao ni waumini wa karma, wao wanaamini kwenye after life na incarnation.

Hakuna yeyote awaye yote aliwahi kufa akayashudia hayo na kurejea duniani kututhibitishia mbingu ipo, peponi kupo na motoni kupo, wala waumini wa reincarnation no one can say for sure alikuwa nani before, zaidi ya ushahidi wa deja vu, hakuna uthibitisho wowote wa reincarnation Ila kwa vile na mimi niliishi India, I know for sure karma ipo and it's for real!

Hivyo hii mada ni mada ya imani, kama wewe huamini, please keep your faith nakuomba usibeze imani za wengine, ukijiona huamini, nakuomba jipitie zako kimya kimya, tuache sisi waumini.

Leo asubuhi nilikuwa nasoma michango ya wachangiaji wa bandiko langu hili.

Kuna mtu akachangia kitu, katika kumjibu nikatumia link hii

Sasa ni wakati nasoma bandiko lenyewe, na naomba nililete hapa bandiko lenyewe lote kwa faida ya wavivu to follow links.


Ndipo nikaisikia sauti, voices from within kuwa JPM yuko peponi, ahera, mbinguni kwa Baba!

Kwa kawaida ya sauti, huwa inakuambia tuu kitu na haikupi sababu, hivyo naomba msiniulize sababu, hapa kazi yangu ni moja tuu kuwaeleza kile nilichosikia Leo ni JPM yuko peponi!

Hivyo baada ya kuisikia hiyo sauti nikamsikiliza tena JPM kwa makini sana katika video hii
Nimejirisha bila chembe ya shaka, huyu mtu yuko mbinguni kwa Baba yake!

Hapa simaanishi kuwa JPM yuko peponi kwasababu he is perfect kama malaika, no!. JPM was a human being hivyo he is not perfect and no one is perfect, kilichofanya hiyo sauti ni despite his human mistakes JPM alitubu kabla ya umauti na kusamehewa makosa yake yote, na ndio maana nimeambiwa, sasa he is in heaven now!.

Kwa bandiko hili, sasa ningewaomba watu humu, kutoendelea kumsakama, kumshutumu, kumsimanga na kuendelea kumsema vibaya, na badala yake tumwache apumzike kwa amani. Kama Mungu mwenyewe amemsamehe na kumuita kwake, who are you kuendelea kumsema sema vibaya?

Mungu Ibariki Tanzania

Paskali.

sawa mtabiri manyota.. haya twambie na wewe utakuwa wapi ukinyakuliwa kama alivyonyakuliwa MEKO..
 
Pascal Mayalla said:
Je, wajua yuko Peponi, Mbinguni, Kwa Baba yake? Why kumshutumu, kumsakama na kumsimanga? Aachwe apumzike kwa amani

Je shetani naye anaweza kutubu akasamehewa? Je siku shetani akitubu na akaweza kusamehewa ina maana hakutakuwa tena na dhambi duniani?

Ona sasa ulivyonilazimisha kuuliza maswali ambayo sitakiwi kuuliza wala kupata majibu yake. Huko aliko shetani lazima hata yeye kashtuka, ama kashtukizwa?

Ndugu zangu nawaomba hizo sauti zenu from within ni vizuri kukaa nazo huko huko within. JPM kuwa peponi kunaweza kumfikirisha sana hata shetani mwenyewe!
 
Je shetani naye anaweza kutubu akasamehewa? Je siku shetani akitubu na akaweza kusamehewa ina maana hakutakuwa tena na dhambi duniani?
Mkuu Mag3, kiukweli kila nikikutana na mchango wangu kwenye nyuzi yangu yoyote huwa nafarijika sana kwasababu jf was meant to be home of great minds, wewe ni among the few real and true GT humu na una hoja za msingi sana.

Mwanzo shetani alikuwa malaika mkuu akaasi ndio akawa shetani, siku akitubu itakuwa ni furaha kuu mbinguni mwenye dhambi mmoja akitubu. Hili nimelizungumza vizuri hapa Malaika akijiunga na mashetani, anageuka shetani? Shetani akijiunga na malaika anageuka malaika?! na hapa Elections 2015 - Nani hatari zaidi kati ya malaika aliyegeuka shetani, Au shetani aliyegeuka malaika?!
Ona sasa ulivyonilazimisha kuuliza maswali ambayo sitakiwi kuuliza wala kupata majibu yake. Huko aliko shetani lazima hata yeye kashtuka, ama kashtukizwa?
Haya ndio type ya maswali mimi ninayo yapenda.
Ndugu zangu nawaomba hizo sauti zenu from within ni vizuri kukaa nazo huko huko within. JPM kuwa peponi kunaweza kumfikirisha sana hata shetani mwenyewe!
Tumefunzwa tusihukumu tusije kuhukumiwa!, Tuacheni ramli chonganishi: Tusihukumu tusije tukahukumiwa. Karma ndio pekee hutoa hukumu ya haki hapa duniani! siku ya mwisho unaweza usiamini Osama, Saddam na Gadafi kuingia peponi halafu Bush, Blair na Osama ukawakuta motoni!.

Shetani watu wanamchora tuu vibaya, mnaweza kukuta triple 666 ni yule mzee wetu wa lile dhehebu kubwa kuliko yote!. Nasisitiza tusihukumu, no one knows alizungumza nini na muumba wake kabla roho haijachukuliwa.

Kuna watu mmeaminishwa ukifa unashukia kuzimu kusubiria ile siku ya kiama ya ufufuko wa miili na hukumu ya mwisho!. Its not!.

Ukifa tuu, mara baada ya mwili kupandishwa, unakwenda hukumuni na pale wanatumia mzani kupima mema na mabaya, mema yakizidi unaingia peponi hata kama ulifanya uovu mkubwa kiasi gani, ukafanya wema mkubwa kabisa kuliko ule uovu, unaingia mbinguni.

Siku za mwisho za Blaza alikuwa mtu mwema sana akitembea na mabulungutu ya minoti!, kusema ukweli kwa baadhi ya makabila hata usome vipi, ushamba haukutoki, tena zile za kutembea na mabulungutu ya fedha na kugawa zilikuwa ndio zangu!. Nilikuwa nikishuka kijijini kumcheki Maza, kijiji kizima kinajua!. Na huku mjini kwa ajili ya yale mambo yetu yale, kiukweli watu wamefaidika sana!.

Nikitolea tuu mfano kuwa ni mimi ndio nimempoteza Ben Saanane, Azori Ganda, Lujwabe na kuamuru zile pyu pyu za Lissu na ile miili kwenye viroba!.

Uovu huo unategeneza a negative karma forces ili kuufidia uovu wangu napata mapigo.

Nikaamua kubadilika kuwa mwema, nikaanza kutembea na mabulungutu ya minoti na kuwagawia masikini, fungulia mahabusu wenye fedha, samehe wafungwa hata wabakaji. Ile negative karma inakuwa reversed into positive, hivyo wema ulioufanya ni mwingi na mkubwa kuliko ubaya, then kwa vile ulikula kichwa, hivyo karma ni lazima ile kichwa, hivyo wakati karma inakula kichwa chako, uko kitandani unagalagala kupigania uhai wako, utatambua kuwa zile powers, pesa, madaraka, mamlaka, cheo, and everything is nothing!, unajutia uliyoyatenda, unatubu dhambi zako kwa mola wako, unajikabidhi Roho yako ichukuliwe, Mungu ni mwenye huruma na anasamehe 7×70!.

By the time Ziraeli mtoa roho anakufikia, anakukuta wewe ni clean kabisa, anaichukua roho yako, roho inaacha mwili, anaikabidhi kwenye mzani wa kupima mema na mabaya, mema yakizidi, naingia peponi!.

Hivyo Mkuu Mag3, nakuomba uniamini!. Hizi the voices within, some ni sauti yake YEYE mwenyewe and they never be wrong!, huyu jamaa yuko peponi!. Voices From Within: Je, wajua yuko Peponi, Mbinguni, Kwa Baba yake? Why kumshutumu, kumsakama na kumsimanga? Aachwe apumzike kwa amani

Japo humu jf tunadharauliana sana, mimi nimeamua kila nikisikia sauti naileta humu, 2025 tutaheshimiana sana maana ni mimi nimeshauri Watanzania, tuunge mkono 2025 ni zamu ya Mwanamke, ila sio lazima awe yeye bali yule aliyepangiwa na 'YEYE', kama ni yeye aliyepangiwa, then ni yeye! lakini nikaisikia hii sauti Voices From Within: Japo 2025 Tumepanga Twende na Mwanamke, 2025 Mama Akabidhi Kwanza Mwanamume, Kisha 2030 Ndipo Aje Mwanamke, sasa tusubiri 2025 tutaheshimiana tuu!.

Unaweza kuziangalia baadhi ya trends zangu za kauli umba "Ombeni Mtapewa", "Tafuteni Mtapata", "Bisheni Hodi Mtafunguliwa" Je Wajua Kuna "Kauli" na "Kauli Umba" Ambazo Huumba?. Shuhudia.., angalia zipi zimetokea!.
Vijikauli vidogo vidogo hivi kutoka kwa watu wa dogo who are nobody, sio vya kupuuzia, na mtu akiforce king, karma haina mswalie Mtume, wala hatujui au kujali nani ni nani, inakula tuu kichwa!.

P
 
Yes kabla ya kufariki aliongozwa sala ya toba tena na mlokole, ngoja niishie hapa siwezi Anika kila kitu, yupo zake mbinguni,
Mkuu Mnaso, asante kwa taarifa hii, tena inawezekana kilicho muingiza peponi ni hii sala ya toba toka kwa mlokole na sio yale mafuta ya mpako wa mwisho toka askofu Mkuu wa dhehebu lake.
Ukimuheshimu Mungu naye atakuheshimu, atakufanyia nafasi ya kutubu wakati wa kufa kwako. Mwenzetu alipata hiyo neema na haijalishi aliyofanya humu duniani.
Amen.
Yeyote anayechekelea kufa kwa huyu baba means hana moyo wa kusamehe na usiposamehe Mungu hatakusamehe, imeandikwa hivyo na ndivyo ilivyo. Kwa jinsi mioyo yenu ilivyo migumu mtakufa vifo vibaya vya kustukiza hata msipate neema ya kutubu.
Asante kuwaeleza watu hili!. Kuna wenzetu humu wana moyo wa ibilisi shetani Lucifer mwenyewe. Angalizo kwa Wana JF: Tuwaepuke "Prophets Of The Doom", kauli zao huumba!
Mwenzetu alijua kabisa anakufa na akakubali kuongozwa Sala ya Toba.
Naomba hili lifanye siri usiliseme tena, lina kiuka the right to privacy ya marehemu!. Kwa vile huyu ni Mkatoliki na amezikwa Kilatoliki, hii inamaani alianza kwanza kufanyiwa sala ya toba akaokoka, ndipo yakafuatia mafuta ya mpako wa mwisho ya Katoliki!, ila kilochomuingiza peponi ni ile sala ya toba na sio yale mafuta!.

Mimi pia ni Mkatoliki, kanisa letu lina vitu fulani vya kijinga jinga ambavyo havitendi haki.
  1. Zamani waligoma kufungisha ndoa kanisani na Muislamu, siku hizi wanakubali ila unatakiwa usile ostia bila kuungama kwanza!.
  2. Ukioa mtu wa dini nyingine yoyote isiyo Katoliki, watoto lazima wawe Katoliki.
  3. Mtoto akizaliwa nje ya ndoa wanagoma kumbatiza, mtoto anakosa gani?!.
  4. Ukiwa hushiriki Jumuiya ndogo ndogo, siku ukifa hawakuziki!.
  5. Ukifa huku ulikuwa na nyumba ndogo, wanakugomea kukuzika!.
  6. Ukijulikana umehamia makanisa ya wokovu unatengwa!, hivyo hiyo issue ya sala ya toba ifanye siri, ili tukikamilisha cannonization ya Nyerere akiishatangazwa Mwenye Heri, tuanze ya Mkapa kisha Magufuli!, siri hii ya sala ya toba ikitua on wrong hands, JPM will never be a saint!.
P
 
Kwani Kuna mtu kasema amepumzika kwa vulugu?.
Ndiyo!! wapo tena wengi tu! km hivi;

wanasema anasota rupango ya kuzimu kwa kuwapora watu haki zao kupitia vyeti fake!...hata km ilikuwa kweli ilipaswa walipwe haki zao sababu waliitumikia serikali na waliruhusiwa kufanya kazi hizo kwa mifumo yao mibovu!

Kuwakamata watu hovyo mpaka kusababisha hofu kuu wengine wakafa kwa hofu....Mfano mamake kabendera!.Ben saa nane!.....yule tajiri Muhindi! Gwajima na kundi lake nk!

Mayanga cons. comp ni yake!! ilivurunda sana na kuiba hela nyingi zasirikali maksudi!

Muongo muongo!! alisema hakopi kumbe alikopa kuliko yeyote!

Kuchukia watangulizi wake bila sababu za msingi! bila wao asingekuwa hivo lkn hakujali hilo wale walikuwa km wazazi wake, kwanza kabisa walikuwa ma-boss wake alipaswa kuwanyenyekea! km Mnangagwa anavo muheshimu Grace!.......Chiruba alikufa mapema bila heshima, sababu tu alimchukia Kaunda!

Kingine alikuwa na kiburi hakutaka kwenda kuchukua hirizi UNGA! sababu tu alilewa kutembea na Ma-body guard!

alikuwa mkurupukaji....anaweza akalala akakuota tuu! ujue kazi huna!..anakufukuza bila staha!.....''nendaaa, tokaaaa! tokaaa!!,,,kwendraaa! ....tumbafuuu!
 
Back
Top Bottom