Je shetani naye anaweza kutubu akasamehewa? Je siku shetani akitubu na akaweza kusamehewa ina maana hakutakuwa tena na dhambi duniani?
Mkuu
Mag3, kiukweli kila nikikutana na mchango wangu kwenye nyuzi yangu yoyote huwa nafarijika sana kwasababu jf was meant to be home of great minds, wewe ni among the few real and true GT humu na una hoja za msingi sana.
Mwanzo shetani alikuwa malaika mkuu akaasi ndio akawa shetani, siku akitubu itakuwa ni furaha kuu mbinguni mwenye dhambi mmoja akitubu. Hili nimelizungumza vizuri hapa
Malaika akijiunga na mashetani, anageuka shetani? Shetani akijiunga na malaika anageuka malaika?! na hapa
Elections 2015 - Nani hatari zaidi kati ya malaika aliyegeuka shetani, Au shetani aliyegeuka malaika?!
Ona sasa ulivyonilazimisha kuuliza maswali ambayo sitakiwi kuuliza wala kupata majibu yake. Huko aliko shetani lazima hata yeye kashtuka, ama kashtukizwa?
Haya ndio type ya maswali mimi ninayo yapenda.
Ndugu zangu nawaomba hizo sauti zenu from within ni vizuri kukaa nazo huko huko within. JPM kuwa peponi kunaweza kumfikirisha sana hata shetani mwenyewe!
Tumefunzwa tusihukumu tusije kuhukumiwa!,
Tuacheni ramli chonganishi: Tusihukumu tusije tukahukumiwa. Karma ndio pekee hutoa hukumu ya haki hapa duniani! siku ya mwisho unaweza usiamini Osama, Saddam na Gadafi kuingia peponi halafu Bush, Blair na Osama ukawakuta motoni!.
Shetani watu wanamchora tuu vibaya, mnaweza kukuta triple 666 ni yule mzee wetu wa lile dhehebu kubwa kuliko yote!. Nasisitiza tusihukumu, no one knows alizungumza nini na muumba wake kabla roho haijachukuliwa.
Kuna watu mmeaminishwa ukifa unashukia kuzimu kusubiria ile siku ya kiama ya ufufuko wa miili na hukumu ya mwisho!. Its not!.
Ukifa tuu, mara baada ya mwili kupandishwa, unakwenda hukumuni na pale wanatumia mzani kupima mema na mabaya, mema yakizidi unaingia peponi hata kama ulifanya uovu mkubwa kiasi gani, ukafanya wema mkubwa kabisa kuliko ule uovu, unaingia mbinguni.
Siku za mwisho za Blaza alikuwa mtu mwema sana akitembea na mabulungutu ya minoti!, kusema ukweli kwa baadhi ya makabila hata usome vipi, ushamba haukutoki, tena zile za kutembea na mabulungutu ya fedha na kugawa zilikuwa ndio zangu!. Nilikuwa nikishuka kijijini kumcheki Maza, kijiji kizima kinajua!. Na huku mjini kwa ajili ya yale mambo yetu yale, kiukweli watu wamefaidika sana!.
Nikitolea tuu mfano kuwa ni mimi ndio nimempoteza Ben Saanane, Azori Ganda, Lujwabe na kuamuru zile pyu pyu za Lissu na ile miili kwenye viroba!.
Uovu huo unategeneza a negative karma forces ili kuufidia uovu wangu napata mapigo.
Nikaamua kubadilika kuwa mwema, nikaanza kutembea na mabulungutu ya minoti na kuwagawia masikini, fungulia mahabusu wenye fedha, samehe wafungwa hata wabakaji. Ile negative karma inakuwa reversed into positive, hivyo wema ulioufanya ni mwingi na mkubwa kuliko ubaya, then kwa vile ulikula kichwa, hivyo karma ni lazima ile kichwa, hivyo wakati karma inakula kichwa chako, uko kitandani unagalagala kupigania uhai wako, utatambua kuwa zile powers, pesa, madaraka, mamlaka, cheo, and everything is nothing!, unajutia uliyoyatenda, unatubu dhambi zako kwa mola wako, unajikabidhi Roho yako ichukuliwe, Mungu ni mwenye huruma na anasamehe 7×70!.
By the time Ziraeli mtoa roho anakufikia, anakukuta wewe ni clean kabisa, anaichukua roho yako, roho inaacha mwili, anaikabidhi kwenye mzani wa kupima mema na mabaya, mema yakizidi, naingia peponi!.
Hivyo Mkuu
Mag3, nakuomba uniamini!. Hizi the voices within, some ni sauti yake YEYE mwenyewe and they never be wrong!, huyu jamaa yuko peponi!.
Voices From Within: Je, wajua yuko Peponi, Mbinguni, Kwa Baba yake? Why kumshutumu, kumsakama na kumsimanga? Aachwe apumzike kwa amani
Japo humu jf tunadharauliana sana, mimi nimeamua kila nikisikia sauti naileta humu, 2025 tutaheshimiana sana maana ni mimi nimeshauri
Watanzania, tuunge mkono 2025 ni zamu ya Mwanamke, ila sio lazima awe yeye bali yule aliyepangiwa na 'YEYE', kama ni yeye aliyepangiwa, then ni yeye! lakini nikaisikia hii sauti
Voices From Within: Japo 2025 Tumepanga Twende na Mwanamke, 2025 Mama Akabidhi Kwanza Mwanamume, Kisha 2030 Ndipo Aje Mwanamke, sasa tusubiri 2025 tutaheshimiana tuu!.
Unaweza kuziangalia baadhi ya trends zangu za kauli umba
"Ombeni Mtapewa", "Tafuteni Mtapata", "Bisheni Hodi Mtafunguliwa" Je Wajua Kuna "Kauli" na "Kauli Umba" Ambazo Huumba?. Shuhudia.., angalia zipi zimetokea!.
Vijikauli vidogo vidogo hivi kutoka kwa watu wa dogo who are nobody, sio vya kupuuzia, na mtu akiforce king, karma haina mswalie Mtume, wala hatujui au kujali nani ni nani, inakula tuu kichwa!.
P