Vunja Bei adai kupata hasara ya zaidi ya Tsh Milioni 300 Jezi za Simba

Vunja Bei adai kupata hasara ya zaidi ya Tsh Milioni 300 Jezi za Simba

Kurunzi

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2009
Posts
9,753
Reaction score
10,747
WAKATI wanachama na mashabiki wa Simba wakianza kusahau machungu ya pilikapilika za kugombea jezi mpya za klabu hiyo, mwenye dili na uzi za Simba, Fred Ngajiro ‘Vunjabei, amevunja ukimya na kufichua hasara ya kupoteza Dola 150,000 (zaidi ya Sh349 milioni).

Vunjabei alisema hasara hiyo imetokana na kubadilisha mfumo wa jezi za awali baada ya kubadilishwa kwa mdhamini kutoka SportPesa na kuwa M-Bet.

Mfanyabiashara huyo alisema, mkataba mpya ulipokuja alikuwa ameshadizaini jezi za mdhamini wa awali, hivyo kumtia hasara ya kiasi hicho cha fedha za kuweka mdhamini mpya.

“Simba waliponipigia simu kuniambia juu ya kusitisha uzalishaji wa jezi kutokana na mkataba mpya basi ikanibidi na mimi nipige simu zoezi lisitishwe jambo ambalo limefanya jezi zichelewe,” alisema Vunjabei na kuongeza.
 
Anatafuta pa kujitetea tu na kwani hakubiwa taarifa za Mkataba kati ya simba na sportspesa? Sababu dezaini inafakhika mapema na jersey zinakuwa tayari inabaki kwenye printing tu ambapo huko china wanaweza kufuta na kuprint tena logo nyingine huyu anatupiga tu kamba
 
Huyu kijana amekosea sana kwenda kuzamini jezi pale Simba.. Tena atazidi kula hasara,, uongozi was Simba ni tiamajitiamaji.. Halafu Mashabiki wake Wana njaa sana, sio wanunuaji wa jezi hata...
Kazi Yao ni kutukana tu wakifungwa na Yanga
 
Asiwe na wasiwasi! Mwekezaji wetu atamfidia mapema iwezekanavyo. Maana mzigo wa Mbet ni mkubwa zaidi kuliko ule wa Sportpesa.

Bilioni 26 siyo mzigo wa kitoto! Yaani umezipita mpaka zile bilioni 20 za uwekezaji wa maisha kwenye klabu yetu, kutoka kwa mwekezaji!
 
Asiwe na wasiwasi! Mwekezaji wetu atamfidia mapema iwezekanavyo. Maana mzigo wa Mbet ni mkubwa zaidi kuliko ule wa Sportpesa.

Bilioni 26 siyo mzigo wa kitoto! Yaani umezipita mpaka zile bilioni 20 za uwekezaji wa maisha kwenye klabu yetu, kutoka kwa mwekezaji!
🤣🤣🤣🤣
 
Gem ya simba na yanga ingerudisha mzigo wake ila kufungwa kwa simba ndo basi tenaaa asitegemeee tena kunufaika kupitia jezi.
 
Acha apambane na hali yake, hakuwa makini na biashara yake.

Kuuza jezi bongo kunahitqji timing sana, ile ya simba day, game kabla ya yanga. Na baada ya game kama simba angeshinda.

Sasa kote amefeli
 
Anatafuta pa kujitetea tu na kwani hakubiwa taarifa za Mkataba kati ya simba na sportspesa? Sababu dezaini inafakhika mapema na jersey zinakuwa tayari inabaki kwenye printing tu ambapo huko china wanaweza kufuta na kuprint tena logo nyingine huyu anatupiga tu kamba
Hivi kuna na kuprint tena unafikiri ni bure? Ujui kwamba katika zoezi la kufuta na kuprint tena kuna resource zimetumika hapo!!!!
 
Hivi kuna na kuprint tena unafikiri ni bure? Ujui kwamba katika zoezi la kufuta na kuprint tena kuna resource zimetumika hapo!!!!
Sawa naelewa lakini sio kama anvyotuaminisha yeye jersey za simba ni tofauti na azam ambayo printing yake inakuwa direct wakati wakufuma nyuzi ila ya simba ni kubandika na kubandua kulikuwa hakuna umuhimu wa kusitisha production zile za awali ndizo zingefutwa logo lakini hizi zingine ambazo ndizo mpya wanvepiga logo mpya
 
Asiwe na wasiwasi! Mwekezaji wetu atamfidia mapema iwezekanavyo. Maana mzigo wa Mbet ni mkubwa zaidi kuliko ule wa Sportpesa.

Bilioni 26 siyo mzigo wa kitoto! Yaani umezipita mpaka zile bilioni 20 za uwekezaji wa maisha kwenye klabu yetu, kutoka kwa mwekezaji!
🤔🤔
 
Back
Top Bottom