Vurugu Kituo cha Mwendokasi Kimara Temboni, abiria ashambuliwa

Vurugu Kituo cha Mwendokasi Kimara Temboni, abiria ashambuliwa

Donnie Charlie

JF-Expert Member
Joined
Sep 16, 2009
Posts
16,908
Reaction score
19,123
Vurugu zimeibuka katika Kituo cha Mabasi ya Mwendokasi cha Kimara Temboni, baada ya kile kinachodaiwa kuwa ni ukiukwaji wa utaratibu wa kupanga mstari kwa abiria.

Tukio hilo limetokea leo Februari 25,2025 majira ya saa 8:40 asubuhi ambapo lilianza pale abiria walipovunja mstari rasmi wa upanda wenye magari hayo na kuanzisha mstari mwingine baada ya basi walilokuwa wakilikimbilia kujaa. Hali hiyo ilisababisha mvutano kati ya abiria na maafisa wa usafiri wa mabasi hayo, huku baadhi ya abiria wakidai kuwa hawawezi kupangiwa namna ya kupanda kwenye basi.

Katika purukushani hizo, abiria mmoja alijeruhiwa baada ya kupigwa na maafisa wa Mwendokasi wakishirikiana na dereva wa basi hilo liifika atika kito hicho lenye namba za usajili T 544 DWR.

Mwandishi wa Nipashe Digital, alikuwa mmoja wa abiria katika kituo hicho na kushuhudia tukio hilo. Mmoja wa abiria alijaribu kutuliza hali kwa kuwaomba maafisa hao pamoja na dereva wampeleke abiria huyo waliokuwa wakimshamulia kituo cha polisi badala ya kumpiga. Dereva wa basi hilo alishuka kwenye gari na kumkaba abiria uyo aliyetoa shauri, jambo lililozua taharuki zaidi.

Tukio hilo limezua mjadala kuhusu changamoto za huduma ya Mwendokasi, ambapo abiria wengi wamekuwa wakilalamikia ucheleweshaji wa magari na msongamano mkubwa wa abiria hasa wakati wa asubuhi.

Aidha, kumekuwa na malalamiko kuhusu tabia ya baadhi ya maafisa wa taasisi za umma kujichukulia sheria mkononi na kutumia nguvu kupita kiasi, jambo ambalo linakinzana na misingi ya utoaji wa huduma kwa wananchi.
20250225_112102.jpg
20250225_112100.jpg
20250225_112058.jpg
 
Vurugu zimeibuka katika Kituo cha Mabasi ya Mwendokasi cha Kimara Temboni, baada ya kile kinachodaiwa kuwa ni ukiukwaji wa utaratibu wa kupanga mstari kwa abiria.

Tukio hilo limetokea leo Februari 25,2025 majira ya saa 8:40 asubuhi ambapo lilianza pale abiria walipovunja mstari rasmi wa upanda wenye magari hayo na kuanzisha mstari mwingine baada ya basi walilokuwa wakilikimbilia kujaa. Hali hiyo ilisababisha mvutano kati ya abiria na maafisa wa usafiri wa mabasi hayo, huku baadhi ya abiria wakidai kuwa hawawezi kupangiwa namna ya kupanda kwenye basi.

Katika purukushani hizo, abiria mmoja alijeruhiwa baada ya kupigwa na maafisa wa Mwendokasi wakishirikiana na dereva wa basi hilo liifika atika kito hicho lenye namba za usajili T 544 DWR.

Mwandishi wa Nipashe Digital, alikuwa mmoja wa abiria katika kituo hicho na kushuhudia tukio hilo. Mmoja wa abiria alijaribu kutuliza hali kwa kuwaomba maafisa hao pamoja na dereva wampeleke abiria huyo waliokuwa wakimshamulia kituo cha polisi badala ya kumpiga. Dereva wa basi hilo alishuka kwenye gari na kumkaba abiria uyo aliyetoa shauri, jambo lililozua taharuki zaidi.

Tukio hilo limezua mjadala kuhusu changamoto za huduma ya Mwendokasi, ambapo abiria wengi wamekuwa wakilalamikia ucheleweshaji wa magari na msongamano mkubwa wa abiria hasa wakati wa asubuhi.

Aidha, kumekuwa na malalamiko kuhusu tabia ya baadhi ya maafisa wa taasisi za umma kujichukulia sheria mkononi na kutumia nguvu kupita kiasi, jambo ambalo linakinzana na misingi ya utoaji wa huduma kwa wananchi.View attachment 3249007View attachment 3249008View attachment 3249009
MAMA Anaupiga mwingi safi sana
 
Halafu wako bize wanajenga mfupa mwingine njia ya bagamoyo.

Hivi kwa nini wasingejenga njia sita au nane kabisa mpaka pale bunju.

Mtu kutoka bunju kuja mwenge unatumia dk 8 tu.

Nje ya mada:

Hivi mainjinia wa mwendokasi, kuna ulazima upi wa kujenga vituo vireeefu maeneo ambayo hayana historia ya kuwa na abiria wengi?

Mfano hivyo mnavyojenga lugalo.
 
Daah hakuna kitu kibaya kama kutopata huduma stahiki mapema. Ingekuwa mwendokasi zinatoa huduma kwa wakati, hakuna kusongamana na kusubiri kwa muda mrefu kituoni yote haya yasingetokea. Hata hao wanaokuwa pale eti wanasimamia wapanda basi wasingehitajika maana hao hao mara nyingi ndio huanzisha vurugu na upendeleo.
 
Vurugu zimeibuka katika Kituo cha Mabasi ya Mwendokasi cha Kimara Temboni, baada ya kile kinachodaiwa kuwa ni ukiukwaji wa utaratibu wa kupanga mstari kwa abiria.

Tukio hilo limetokea leo Februari 25,2025 majira ya saa 8:40 asubuhi ambapo lilianza pale abiria walipovunja mstari rasmi wa upanda wenye magari hayo na kuanzisha mstari mwingine baada ya basi walilokuwa wakilikimbilia kujaa. Hali hiyo ilisababisha mvutano kati ya abiria na maafisa wa usafiri wa mabasi hayo, huku baadhi ya abiria wakidai kuwa hawawezi kupangiwa namna ya kupanda kwenye basi.

Katika purukushani hizo, abiria mmoja alijeruhiwa baada ya kupigwa na maafisa wa Mwendokasi wakishirikiana na dereva wa basi hilo liifika atika kito hicho lenye namba za usajili T 544 DWR.

Mwandishi wa Nipashe Digital, alikuwa mmoja wa abiria katika kituo hicho na kushuhudia tukio hilo. Mmoja wa abiria alijaribu kutuliza hali kwa kuwaomba maafisa hao pamoja na dereva wampeleke abiria huyo waliokuwa wakimshamulia kituo cha polisi badala ya kumpiga. Dereva wa basi hilo alishuka kwenye gari na kumkaba abiria uyo aliyetoa shauri, jambo lililozua taharuki zaidi.

Tukio hilo limezua mjadala kuhusu changamoto za huduma ya Mwendokasi, ambapo abiria wengi wamekuwa wakilalamikia ucheleweshaji wa magari na msongamano mkubwa wa abiria hasa wakati wa asubuhi.

Aidha, kumekuwa na malalamiko kuhusu tabia ya baadhi ya maafisa wa taasisi za umma kujichukulia sheria mkononi na kutumia nguvu kupita kiasi, jambo ambalo linakinzana na misingi ya utoaji wa huduma kwa wananchi.View attachment 3249007View attachment 3249008View attachment 3249009
Wanaume wa dar wanapigana, hapo akija mwanafunzi wa sekondari kutoka mikoani hasa Arusha/mara anawachakaza wote hapo
 
Ni hatari!
Huyo jamaa mwingine kaona afadhali atulie zake mtaloni huko.
 
Back
Top Bottom