Vurugu za Bungeni: Tundu Lissu, Anastahili Adhabu Kali?!. Ni Mtundu Toka Shule!.

Vurugu za Bungeni: Tundu Lissu, Anastahili Adhabu Kali?!. Ni Mtundu Toka Shule!.

Ndugu Pasco,

unapomzungumzia kiongozi yeyote wa CCM jua moja kwa moja unamzungumzia mtu aliyetelekeza akili zake kwa makusudi ili aendelee kuneemeka binafsi. CCM inayo watu werevu tatizo linakuja kwamba watu wanaofaa huwa hawapewi nafasi za uongozi kwa namna yeyote ili kukwepa changamoto. kuonyesha udhaifu wa wana CCM afanyayo Anna Makinda hayana tofauti na ya Hamisi Kigwangala ambaye kwa maandishi yake mwenyewe hapa JF, anasema anaweza kudebate na mtu yeyote kwenye issue yeyote. sasa mtu kama huyu akiwa spika unategemea nini? maana haamini katika kutokujua.

Kanuni za bunge kama sheria yeyote ili vifungu vyake husomwa kwa ujumla wake na ni mara chache husomwa kwa umoja wake. Kwa minajili hiyo mtu mwenye taaluma ya sheria kwakwe inakuwa rahisi hasa linapokuja swala la kutafsiri sheria, kamwe asiyejua sheria atayumba tu.

"YOU MAY CHAIN THE TONGUES OF MEN BUT YOU WILL NEVER TOUCH THEIR MIND"
 
Mh. Tundu Lisu ananikumbusha mbali! Mwaka 1961 tukiingia Form 1, haikuchukua muda darasa letu, pamoja na kuwa vinyoya, likajulikana kama "siasa kali" (wakati huo hatujapata uhuru). Bahati mbaya wengi wa vipanga darasani walilazimika kuchukua masomo ya sayansi kwani huo uhuru wa kuchagua haukuwapo sana. Nina hakika mtu kama Tundu Lisu, angesoma wakati huo, labda siasa angeisikia tu kwa mbali...sana sana angeishia kuwa Injinia au dakitari! Linalosikitisha ni kuwa wengi wa viongozi wa baadaye kutoka kundi letu (Wabunge na Mawaziri) ni wale ambao somo la "additional & applied mathematics" walikaa nao mbali kama ukoma. Kweli mambo yalikuja kubadilika!

Duh! Mag3 una wajukuu wangapi sasa?


Dah! Heshima Mkuu. Shikamoo.

Mkuu umehamia digitali kweli?

Hahahaha Mkuu Mag3 naona umezua jambo hapa, watu wanataka kufahamu hadi na idadi ya wajukuu zako.
Bila shaka huu ni uthibitisho tu kwamba JF ina kila aina ya watu ambao pengine mtu asingetarajia, na ndio maana JF inakuwa na nguvu zaidi na ubora zaidi kuliko mitandao kadhaa ya kibongo iliyopo.
 
Last edited by a moderator:
Haina shida waache wa msimamishe tundu lissu aje apige amsha amsha mtaani huku wasisahau kumuongeza na mchungaji peter msigwa hapo maana hao jamaa wakiingia mtaani miezi sita watakuwa wamepiga kazi ya maana sana m4c tutawaacha vijana wanatosha kukimbiza wabunge wote hao wa ccm!!!!!!!!!1
 
mkuu ni wachache sana ambao hawajawahi kuvuta bangi, inategemea hiyo bangi inakusaidiaje, au ilikusaidiaje au ilikupotoshaje, mimi O'level nimeikandamiza sana,
Bangi ikikukataa unateseka sana. Ngoja tusubiri orodha ya WABUNGE wavuta bangi. Bila shaka Madame Spika ataiweka hadharani ili tuwafahamu. Wabunge vijana ni wengi mno na kama wavutaji bunge letu halitatulia.
 
Bangi ikikukataa unateseka sana. Ngoja tusubiri orodha ya WABUNGE wavuta bangi. Bila shaka Madame Spika ataiweka hadharani ili tuwafahamu. Wabunge vijana ni wengi mno na kama wavutaji bunge letu halitatulia.
mkuu unadhani atakaowataja mheshimiwa madam speaker ndo wavuta bangi au yeye ndo anatumika na wavuta bangi?
inawezekana wote ni wavuta bangi ila bangi zinawasaidia tofauti kiakili......
 
walimfanyia fitna sitta, sasa kamasi inawatoka, sitta alikua anajitahidi sana ku-balance mijadala, na sheria na kanuni anazijua kwelikweli, haya mazezeta mawili yalipewa uspika for a reason, to serve their masters, hata mimi nisingekubali hoja muhimu kama ya mnyika kuhusu maji zezeta ndugai linakataa tu lenyewe, kazi yake kuibana serikali, anajisahau yeye anakua part ya serikali, kwanini wapinzani wasikasirike kwa usenge kama huo?

let them reap what they sow,

ningependa zichapike siku moja bungeni, tena waanze na makinda au ndugai
Mkuu Moshe, nakuomba ulitendee haki hili jukwaa, hapo kwenye white!.
Mode please weka vile vi xxxx kwenye hilo neno!.
Pasco.
 
Wanabodi,

Juzi katika kikao cha bunge, Spika wa Bunge, Mhe. Anne Maklnda, alimtaja Mbunge wa Singida, Mhe. Tundu kama ndie Mbunge anayeongoza kwa kuwa chanzo cha vurugu za bungeni, kwa kuongoza kwa utovu wa nidhamu, kuleta fujo na vurugu bungeni, hali ambayo sio tuu inahatarisha hali ya utulivu, amani na usalama wa bungeni, bali pia kumepelekea Spika kufuta baadhi ya ratiba za bunge ambazo zilikwisha ridhiwa na kuingizwa kwenye order paper ikiwemo kupokea hoja binafsi za wabunge, kwa kilichoelezwa kuepuka vurugu zaidi.

Jana kika cha kamati ya Uongozi kimekaa kujadili hali hiyo na matokeo yake, tutayapata kesho asubuhi baada ya kipindi cha maswali ya papo kwa papo na maswali na majibu! ni hakika rungu la kiti, lazima litamshukia Mhe. Tundu Lissu!.

Swali la kwanza la kwanza ambalo wengi mtapenda kujiuliza ni, ni jee ni kweli, Mhe. Tundu ni mtundu na ndie chanza cha utovu wote wa nidhamu wa bunge hili la kumi?, kama anavyoelezwa na Madam Speaker?, au huo utundu wa Mhe. Tundu, sio utundu bali uzingatiaji wa kanuni za Bunge, kufuatia Mhe. Spika, kuonyesha udhaifu mkubwa katika kuliendesha bunge kwa kutokuzingatia, sheria, taratibu na Kanuni?.

Kwa vile mimi ni mmoja wa watu tunaomfahamu Mhe. Tundu, Tangu akiwa Shuleni, naomba kuchukua fursa hii kumfariji Mhe. Spika, kwa kumuomba asiumize sana kichwa chake kuendelea kubishana na Mheshimiwa Tundu Lissu kuhusu kanuni za bunge, wala wasipoteze muda kumuadhibu kwa jambo ambalo liko wazi kabisa na udhaifu unajulikana tangu chanzo chake, ulipo na labda utaendelea kuwepo, hata akiadhibiwa vipi, kwa sababu Mhe. huyu ni mbishi hakuna mfano!, haswa pale anapokuwa na uhakika kuwa yuko right!.

Nashauri Mhe. Spika, lazima ufike mahali, umkubali huyu jamaa kuwa lile jina lake la Tundu, sio jina tuu, huyu bwana analiishi jina lake kwa kuwa ni mtundu kweli pale kanuni zinapopindishwa ili kutoa mteremko kwa upande fulani!.

Nimebahatika kusoma na Mhe. Lissu shule moja kule Ilboru, (sio darasa moja) miaka hiyo enzi za Mkuu mmoja aitwae Bino!. Huyu Bino alikuwa ni mwalimu mkuu bingwa wa nidhamu, ila kwa Tundu, alinyanyua mikono juu na kwisha kuishusha juu baada ya kuthibitika kuwa japo Tundu alikuwa "toto tundu", ila pia ndie aliyekuwa kipanga wa darasa lake!, kwani pepa alikuwa akizifumua, utadhani mtihani katunga yeye!.

Tundu Lissu alijiunga shule ya vipanga ya Ilboru akitokea Galanos, wakati huo akiitwa Antipasi Tundu, na alikuwa ni mtoto mtundu kweli!. Wakati huo sisi Wasukuma tukiitwa "Wasukusu", wenyeji wakiitwa "wamenye" huku jamaa wa Singida wakijiita watu wa "Singapore", uji ukiitwa "sumu", na nje kulikuwa na duka la kwa "Akwii".

Utundu wa Tundu Lissu ulkikuwa ni kwenye mishe mishe tuu hizi za zile, haijulikani alikuwa akisoma saa ngapi, ila pepa zikija, anafumua ile mbaya!. Moja ya maeneo ambayo jamaa alikuwa ni ni mtundu au tusema ni mbishi, ni kwenye school debate!. Jamaa akishakuwa na uhakika yuko on the right track, ni mbishi hakuna mfano!. Hata nami nilikuwa na matatizo yangu tangu shule, yale matatizo ya kawaida ya Chapa Ng'ombe, unapokutana na vibinti vya Vyeupe vya Kiarusha pale Mlimani Ilboru, ukijumlisha na lilke baridi la kule, tena wakati huo, "bwawa halijaingia luba!'...

Tundu lissu kama livyoingia Ilboru, vivyo hivyo ndivyo alivyoondoka na wani kali, akaenda UDSM na sisi vilaza wengine tuykaishia vile vyuo vya mashenzini!. Tulipoteana kwa kipindi cha miaka 10!, tulikuja kukutana tena mjini Atlanta, yeye akiwa na yeke nami na yangu, ndipo akanieleza yuko LEAT, na huko aliichachafya serikali vivyo hivyo kama anavyo mchachafya Madame Spika, kwa kumsubu bila huruma!.

Pamoja na utundu wote huu wa Mhe. Tundu Lissu, wakati tukisubiria kusikia ni adhabu gani itamfika hapo kesho, kuna maswali matatu tujiulize!.
  1. Jee ni kweli Mhe. Tundu Lissu ni mtundu kihivyo na ndio anayeongoza kwa utovu wa nidhamu hadi kustahili adhabu kali?.
  2. Au ni Spika ndiye dhaifu hadi kushindwa kumdhibiti Tundu Lissu na utundu wake?.
  3. Baada ya kuthibitisha, Mhe. Tundu Lissu alikuwa ni mtundu toka shuleni, jee nani wa kubadilika kati ya Mhe Tundu Lissu na wabunge wa upinzani, wakae kimya wakati sheria, taratibu na kanuni, zikikiukwa, na kupindishwa?, hivyo kumpatia fursa Mhe. Spika kujiendeshea bunge anavyotaka, ili kudumisha utii, na nidhamu, bunge liwe la amani?.
  4. Hivyo Mhe Spika kuwathibitishia Watanzania kuwa hata yeye ambaye ni Spika wa majaribio ya "jinsia" "ameweza" kuliendesha bunge vizuri tuu, ambalo ni mhimili mmoja wa dola, hivyo jee, 2015, tukamilishe majaribio ya "jinsia" kwa mihimili miwili iliyobakia?, ili nchi yetu iwe ni nchi ya usawa halisi wa kijinsia?.

Wasalaam

Pasco.
(Skulu Meti wa Toto T).

mkuu, Tundu kasoma A'level Galanos. Ilboru kasoma O'level. Sasa alihama kutoka Galanos kwenda Ilboru kivp?. Tuliosoma pale Galanos japo hatukumkuta ila rekodi zinaonesha amesoma HGE pale. Naona umechapia kidogo mkuu.
 
Acha kupotosha watu wewe hujui Tundu ni litobo lililowazi.Halafu mtu mwenyewe anapenda kulialia mnajidai kumsifia

View attachment 82223

02_11_c13mja.jpg
 
Mkuu Mpango, Ilboru ile ilikuwa ya vipanga wa kutoka kwenye umande na sio hii ya sasa ya spoon fed vipanga toka academy!.

Leat ni Chama cha Wanasheria wa Mazingira, wamefight sana ushenzi uliofanywa Loliondo, Yaeda Chini, sumu za Barick kule mto Tigiti na ushenzi mwingine wote tunaofanyiwa kwa jina au la hifadhi, au uwekezaji!.

Kuhusu sisi Watanzania, ni watu watulivu, watu wa upendo na mshikamano, hivyo viongozi wetu wanatutake for granted, hata wakifanya chochote, sisi ni yes man!, kuna wakati sikumbuki ni nchi gani, mkate ulipanda bei by 20%, maandanano nchi nzima, waziri mkuu wa nchi hiyo aling'olewa!. Sisi mtu anakufa mikononi mwa polisi picha zinasema kila kitu na wote wametulia tuu as if nothing happened. 1976 nikiwa mdogo bado, Mzee wangu aliwajibishwa kwa ile kesi ya mauji Mwanza, kuanzia Waziri wa mambo ya ndani na wa usalama, walijiuzulu, IGP, Boss wa TISS, walistaafishwa!, RPC, RSO, OCD, DSO walipandishwa kizimbani!. Leo tangu ile ya Maandamano Arusha, mtu kapigwa risasi stend, polisi wakatengeneza a make belive video kuwa wamewaua watu waliokuja kuvamia kituo cha polisi!, ya Mwangosi ndio usiseme, no one amewajibika as if nothing happened nasi tunawashangilia na 2015, tunawapa term nyingine tena!.

Tatizo sio viongozi wetu, tatizo ni sisi Watanzania, sisi ni mandondocha kabisa!, hatuchagui viongozi kwa sifa kwa sababu hata JK tulipomchagua kwa ile landslide tulimchagua kwa sifa zipi?. Spika Anne aliletwa ili kumkomoa Six awekwe bench ili kutoa fursa ya kumsafisha EL na dodoki litapita 2014!. Eti sifa kuu ni "gender!". Nimeshazisikia fununu kuwa kwa vile kuna mafahali wanapigana vikumbo kuigombania magogoni, kuna sketi nyingine inaandaliwa, ili kumleta a compromised candidate chama kisimegeke!. Ndani ya CCM, 2015 ni zamu ya Zanzibar, Shein is the man!, ila wanahofia wasiitoe magogoni kwa sadakawe kwenye upepo wa M4C!.

Amini nakuambia jinsi tulivyo mandondocha, hiyo 2015, hata tukiletewa sketi nyingine, tutaichagua tuu!, na ni CCM tena!.

Pasco.

Unamawazo mgando kaka Pasco, huyo Makinda pekee ndiye brain behind the bunge bovu?
Ndugai, Lukuvi, Mwanasheria mkuu , wasira nk hawa pia ni skirt?
Au bado uko huko, hujatoka bado???
 
mkuu unadhani atakaowataja mheshimiwa madam speaker ndo wavuta bangi au yeye ndo anatumika na wavuta bangi?
inawezekana wote ni wavuta bangi ila bangi zinawasaidia tofauti kiakili......
Wenye akili nyingi darasani wakilivuta wanakuwa ni walipukaji sana. Kwa trend ilivyo Bungeni sasa, wavutaji ni wengi.
 
hapo kwenye bluu nimeshakukataza tokea jana husikii,kipindi cha sitta mijadala mizito kama epa na richmond aliruhusu ijadiliwe na ccm wenzake wakasulubiwa vya kutosha!!!idadi sio ishu we msukuma,slaa peke yake alikuwa analiyumbisha bunge zima,sitta hakuwa mbabaishaji,kanuni zote zilikuwa kichwani,..yani kumlinganisha sitta na makinda ni matusi makubwa kwa mzee sitta

Mkuu,
Huoni kama maelezo yako yanajichanganya............Kwanza unamsifia Mh.Sitta, halafu hapo hapo unasema alikuwa anayumbishwa na Dr. Slaa, tena huoni soni, kama Mh. Sitta alikuwa anayumbishwa na mtu mmoja, kwa nini usione kama kulikuwa na tatizo kuliko la Mh. Makinda kuyumbishwa na watu wengi wasomi walioingia bungeni ........Sasa sijui nielewe lipi............jaribu kujenga hoja inayoeleweka.

By the way, wewe ni kabila gani?.
 
Acha kupotosha watu wewe hujui Tundu ni litobo lililowazi.Halafu mtu mwenyewe anapenda kulialia mnajidai kumsifia

View attachment 82223

Mkuu pamoja na chuki iloonesha kwa mheshimiwwa Tundu, kiswahili chako vipi? Likesha kuwa "Tobo" ni lazima liwe wazi. Huwezi sema tobo lililo wazi.
 
walimfanyia fitna sitta, sasa kamasi inawatoka, sitta alikua anajitahidi sana ku-balance mijadala, na sheria na kanuni anazijua kwelikweli, haya mazezeta mawili yalipewa uspika for a reason, to serve their masters, hata mimi nisingekubali hoja muhimu kama ya mnyika kuhusu maji zezeta ndugai linakataa tu lenyewe, kazi yake kuibana serikali, anajisahau yeye anakua part ya serikali, kwanini wapinzani wasikasirike kwa usenge kama huo?

let them reap what they sow,

ningependa zichapike siku moja bungeni, tena waanze na makinda au ndugai
Mkuu Moshe Dayan hapo mwisho kweli umeghadhabika,sijawahi kuona ukifuka moshi kihivyo..hahaa..
Ukweli Unazi wa Makinda na Ndugai utatia kichefuchefu. Jaribu kupitia magazeti ya kenya uone uwajibikaji wa Bunge na taasisi zake under new constitution dispensation..Hadi wameweka wazi Wananchi watoe maoni juu ya Viwango vya mishahara vya Rais,makam, na mawaziri..Natamani kenya ile iwe tanzania..pamoja na udhaifu wao wa ukabila,but the fox are inspiring for real!
 
Last edited by a moderator:
Nilisoma na TUNDU LISSU UDSM ingawa tulikuwa faculty tofauti lakini hakuna mtu ambaye alikuwa hamjui kwa ubishi na kuzungumza sana inapojitokeza migomo chuoni, yeye alikuwa mbele kupambana na utawala wa chuo na serikali.

Anachofanya TUNDU LISSU ndio tabia yake hasa kwa ambao tunamjua muda mrefu, anapobisha haijalishi yuko sahihi au la ubishi wake uko kwa kile anachokiamini.

Kama TUNDU LISSU hakubadilika akiwa mdogo sina hakika kama atabadilika ukubwani. HUYU bwana amepata misukosuko mingi sana katika maisha kutokana na misimamo mikali lakini haijasaidia kumrekebisha tabia.

Mama Spika anatakiwa kutafuta mbinu tofauti na ambazo zimekwishatumika tangu akiwa mtoto kumthibiti bila mafanikio. Akitumia kanuni za kibunge kumthibiti atamuweza kwani ni mwanasheria mwenye kipaji na akili sana wanaomjua wamewahi kumuona akijenga hoja mahakamani ni TUNDU aliyeongoza kwa mabishano ya kisheria. kafanya kazi pale Mahakama Kuu kwa muda mrefu.
 
nasikia mama ni mwasibu(accountant)na Tundu Lisu ni mwanasheria.Lisu katika tasnia ya sheria amefanya mengi sana kabla ya kuwa mbunge,ata serikali ilishawai kumtumia kwenye kesi ya city water ambayo baadaye tulishinda kwenye mahakama ya kimataifa
 
Back
Top Bottom