Vurugu za Bungeni: Tundu Lissu, Anastahili Adhabu Kali?!. Ni Mtundu Toka Shule!.

Vurugu za Bungeni: Tundu Lissu, Anastahili Adhabu Kali?!. Ni Mtundu Toka Shule!.

Mkuu Dark City,
nimeripoti chaguzi 4, hivyo ya 2015 itakuwa ni uchaguzi wa tano kuuripoti. CCM siku zote inashinda sio kwa sababu inapendwa sana, bali kwa mazoea tuu!, nimeisha andika makala zangu mbalimbali kwa nini 2015 ni CCM tena. Chadema itavuna wabunge wengi zaidi huku bara, CUF itapoteza baadhi ya majimbo. Mshindi wa jumla wa urais ataendela kuwa CCM!.

Chadema inayo nafasi ya kushinda kama itakubali "to do things right", kwa sasa kupitia M4C, Chadema, inafanya kazi nzuri, yaani "is doing the right thing!". Ili chapa kipya kiweze kuking'oa "chama kubwa", "chama kongwe", na kuingia Ikulu, "doing the right thing" peke yake hakutoshi!, it got to do "things right", kitu ambacho sikioni Chadema kufanya!, as a result watu wataendeleza mazoea!.

Zile umati za watu kwenye maandamano au kwenye mikutano, sio kura!, nimeisha waambia Chadema humu kwa nini hawatashinda urais 2015 na nini cha kufanya, lakini nimeishia kutukanwa tuu "wee gamba!", mimi nasisitiza kuendelea kusema ukweli no matter what. Let them call me what they may, ila ikifika 2015 mtayaono na baada ya hapo tutaanza kuelewana vizuri!.

Siasa ni kama barabara ndefu, mbovu na ya kona kona, milima, mabonde, mashimo na makorongo!, vyama ni kama magari, wanachama ndio abiria, na viongozi wa vyama ndio madereva!. Kuelekea 2015 ndio safari yenyewe. Kwa huku bara, mchuano ni kati ya CCM, (gari kongwe, injini kongwe chovu, lakini dereva mzoefu, aliyeisha izoea hiyo barabara, miaka nenda, miaka rudi, hivyo anajua aendesheje, wapi apunguze mwendo na wapi aende kasi, wapi kuna korongo wapi kuna bonde, wapi kuna konakali na wapi kuna mlima, etc,etc!) na Chadema (gari mpya na injini bomba ina nguvu kupita gari kongwe na inakwenda mbio kuliko ule mkweche ila ina dereva mpya ambaye hajui njia!, kazi ya dereva mpya ni kutimua mbio, na kuendesha kwa kasi ili awahi kufika!, kutokana na kutojua njia, japo anakwenda kasi zaidi, kwa kuipita gari kongwe kwa mbali, mara kibao hujikuta anapotea njia, hivyo kulazimika kurudi nyuma na kuendelea na safari!.

Kwenye hii scenario, huyu dereva mpya anayo nafasi ya kushinda, sio kwa kitimua mi mbio, bali endapo atakubali au kuwasikiliza baadhi ya abiria wake wazoefu ambao wameishaipita njio hiyo mara nyingi ndani ya ule mkweche, au kutusikiliza sisi watazamaji wa mchuono huo ambao sio abiria wa gari yoyote, ila tuko homo njiani kwa muda mrefu, tunapoona dereva mpya anakosea, huwa tunampungia ishara kuwa huko siko!, au kumpa ishara ya hatari ya mbele, lakini hasikilizi!. Yeye ni mwendo kasi wa mbio tuu huku akishangiliwa na umati wa abiria wake, kuwa aendeleze "mwendo mdundo!.

Safari ya kuelekea 2015 ndio hii inaendelea, sasa hivi tuko half way!, bado hakuna dalili za dereva mpya kujifunza, hebu tusubiri, nasikia kutafanyika zoezi la kubadilishana madereva baadae mwaka huu, hebu na tusubirie timu mpya tuone, hata ikirudi timu ile ile kama itaendelkeza uendeshaji ule ule, basi ni hakika bila mashaka yote, mshindi ataendelea kuwa yule yule, dereva bingwa mwenye ule mkweche!.

Pasco.

Ahsante sana ndugu Pasco,

Nilijua wewe ni mwandishi mkongwe na Mchambuzi, pia Mtambuzi wa mambo ya kisiasa. Kwa hiyo nilitegemea utanijibu kisayansi zaidi na kwa uchambuzi wa kutosha kuonesha tu si kwamba CCM itashinda 2015 bali itatawala milele kama ulivyosema kwenye ile post yako ya nyuma.

Unayoyasema ni kama yale yale ambayo mgombea wako EL aliwahi kuwambia wanataaluma wa SUA mwaka1996, kuwa CCM itatawala milele.... Sina hakika kama naye takuwa bado na mtazamo ule ule ukizingitia jitihada zake zinazidi kuzama gizani...

Kwa hiyo, naomba kama hutajali, utusaidie sie ambao labda tuna euphoria ya mabadiliko, kwa kutupatia uchambuzi wenye emperical evidence kwa nini CCM itashida 2015 na pia itatawala milele. Uliyoyasema kwenye post yako bado yako circumstancial kiasi kiasi kwamba yanakosa hoja za kuridhisha.

Ahsante sana!
 
Last edited by a moderator:
ulichonifurahisha tu kwenye hiyo post yako ni kunikumbusha umenyeni tu
 
ngoja tuone maamuzi yatatokaje. kuna watu huwa wanapenda kujitoa akili, wanapenda kujifanya hamnazo, lakini tunawaambiaje, safari hii mpaka watashika akili. haiwezekani watz tuchezewe na kundi dogo la watu wachache waroho mpaka wameshikwa na pepo la uroho, na ndilo linalowaondoa akili. sasa wasikilize vizuri mtapungwa hayo mapepo ya uroho, ufisadi, wizi mpaka mjitambue, maana yamewakamateni ufahamu, kila upuuzi mnaofanya mnauona kama ni jambo la kawaida.
 
Wanabodi,


Swali la kwanza la kwanza ambalo wengi mtapenda kujiuliza ni, ni jee ni kweli, Mhe. Tundu ni mtundu na ndie chanza cha utovu wote wa nidhamu wa bunge hili la kumi?, kama anavyoelezwa na Madam Speaker?, au huo utundu wa Mhe. Tundu, sio utundu bali uzingatiaji wa kanuni za Bunge, kufuatia Mhe. Spika, kuonyesha udhaifu mkubwa katika kuliendesha bunge kwa kutokuzingatia, sheria, taratibu na Kanuni?.

Nimebahatika kusoma na Mhe. Lissu shule moja kule Ilboru, (sio darasa moja) miaka hiyo enzi za Mkuu mmoja aitwae Bino!. Huyu Bino alikuwa ni mwalimu mkuu bingwa wa nidhamu, ila kwa Tundu, alinyanyua mikono juu na kwisha kuishusha juu baada ya kuthibitika kuwa japo Tundu alikuwa "toto tundu", ila pia ndie aliyekuwa kipanga wa darasa lake!, kwani pepa alikuwa akizifumua, utadhani mtihani katunga yeye!.

Tundu Lissu alijiunga shule ya vipanga ya Ilboru akitokea Singida, wakati huo akiitwa Antipasi Tundu, na alikuwa ni mtoto mtundu kweli!. Wakati huo, Ilboru ilichukua wanafunzi wenyeji wa Arusha, Singida na Shinyanga!. Sisi Wasukuma tukiitwa "Wasukusu", wenyeji wakiitwa "wamenye" huku jamaa wa Singida wakijiita watu wa "Singapore", uji ukiitwa "sumu", na nje kulikuwa na duka la kwa "Akwii".

Utundu wa Tundu Lissu ulkikuwa ni kwenye mishe mishe tuu hizi za zile, haijulikani alikuwa akisoma saa ngapi, ila pepa zikija, anafumua ile mbaya!. Moja ya maeneo ambayo jamaa alikuwa ni ni mtundu au tusema ni mbishi, ni kwenye school debate!. Jamaa akishakuwa na uhakika yuko on the right track, ni mbishi hakuna mfano!. Hata nami nilikuwa na matatizo yangu tangu shule, yale matatizo ya kawaida ya Chapa Ng'ombe, unapokutana na vibinti vya Vyeupe vya Kiarusha pale Mlimani Ilboru, ukijumlisha na lilke baridi la kule, tena wakati huo, "bwawa halijaingia luba!'...

Tundu lissu aliondoka na wani kali, akaenda Galanos hatimaye UDSM. Sisi vilaza wengine tukaishia vile vyuo vya mashenzini!. Tulipoteana kwa kipindi cha miaka 10!, tulikuja kukutana tena mjini Atlanta, yeye akiwa na yeke nami na yangu, ndipo akanieleza yuko LEAT, na huko aliichachafya serikali vivyo hivyo kama anavyo mchachafya Madame Spika, kwa kumsubu bila huruma!.

Pamoja na utundu wote huu wa Mhe. Tundu Lissu, wakati tukisubiria kusikia ni adhabu gani itamfika hapo kesho, kuna maswali matatu tujiulize!.
  1. Jee ni kweli Mhe. Tundu Lissu ni mtundu kihivyo na ndio anayeongoza kwa utovu wa nidhamu hadi kustahili adhabu kali?.
  2. Au ni Spika ndiye dhaifu hadi kushindwa kumdhibiti Tundu Lissu na utundu wake?.
  3. Baada ya kuthibitisha, Mhe. Tundu Lissu alikuwa ni mtundu toka shuleni, jee nani wa kubadilika kati ya Mhe Tundu Lissu na wabunge wa upinzani, wakae kimya wakati sheria, taratibu na kanuni, zikikiukwa, na kupindishwa?, hivyo kumpatia fursa Mhe. Spika kujiendeshea bunge anavyotaka, ili kudumisha utii, na nidhamu, bunge liwe la amani?.
  4. Hivyo Mhe Spika kuwathibitishia Watanzania kuwa hata yeye ambaye ni Spika wa majaribio ya "jinsia" "ameweza" kuliendesha bunge vizuri tuu, ambalo ni mhimili mmoja wa dola, hivyo jee, 2015, tukamilishe majaribio ya "jinsia" kwa mihimili miwili iliyobakia?, ili nchi yetu iwe ni nchi ya usawa halisi wa kijinsia?.

Wasalaam

Pasco.
(Skulu Meti wa Toto T).


Asante sana kaka Pasco,
maelezo na story nzuri sana
naona Mzee Mohamed Said keshakufundisha aina ya uandishi wake,
 
Ngoja niandike kwa kifupi tu, sote tunafahamu kuwa Bunge la JMT na vikao vyake, linaongozwa kwa kanunu na sheria kama ilivyo kwa mabunge mengine.
Kwa kuwa umeamua kuuweka huu mjadala kuwa baina ya Tundu Lissu na Anne Makinda, basi ni vyema tukajikita zaidi kwenye ufahamu wao binafsi juu ya utambuzi na uchanganuzi wa sheria.
Ikumbukwe kuwa kila mara Tundu Lissu anaposimama na kupinga hoja au kutokua na imani na jambo fulani bungeni, huwa ananukuu vifungu fulani vya kanuni na taratibu. Sasa hapa tujiulize, uwezo wa Anne Makinda kutafsiri sheria ni mkubwa kiasi gani? Taaluma yake ya Ualimu inamsaidia kupambana na wanazuoni wa sheria kama Lissu?
Sidhani kama ni kweli maana ni mara kadhaa tumekuwa tukimsikia Anne Makinda, akikiri kuwq bado kanuni na sheria za Bunge zinamtatiza haswa katika kuzitafsiri.

"Nashukuru kutambua kuwa kaka yangu Pasco nawe ni Mmenye mwenzangu"
Makinda si mwalimu nadhani alisomea ukarani wa mahesabu kule Mzumbe. Walimu wana uelewa mpana eti, si kama hilo kinda
 
Asante sana kaka Pasco,
maelezo na story nzuri sana
naona Mzee Mohamed Said keshakufundisha aina ya uandishi wake,
Asante , katika fasihi simulizi Mzee Mohamed Said
ni Maalim wa ukweli , tatizo lake ni moja tuu -sumu ya udini aliyofanikiwa Sana kuipandikiza, soon tutashuhudia ikimea na wakati wa mavuno ukifika patakuwa hapatoshi!.
P.
 
Ngoja niandike kwa kifupi tu, sote tunafahamu kuwa Bunge la JMT na vikao vyake, linaongozwa kwa kanunu na sheria kama ilivyo kwa mabunge mengine.
Kwa kuwa umeamua kuuweka huu mjadala kuwa baina ya Tundu Lissu na Anne Makinda, basi ni vyema tukajikita zaidi kwenye ufahamu wao binafsi juu ya utambuzi na uchanganuzi wa sheria.
Ikumbukwe kuwa kila mara Tundu Lissu anaposimama na kupinga hoja au kutokua na imani na jambo fulani bungeni, huwa ananukuu vifungu fulani vya kanuni na taratibu. Sasa hapa tujiulize, uwezo wa Anne Makinda kutafsiri sheria ni mkubwa kiasi gani? Taaluma yake ya Ualimu inamsaidia kupambana na wanazuoni wa sheria kama Lissu?
Sidhani kama ni kweli maana ni mara kadhaa tumekuwa tukimsikia Anne Makinda, akikiri kuwq bado kanuni na sheria za Bunge zinamtatiza haswa katika kuzitafsiri.
"Nashukuru kutambua kuwa kaka yangu Pasco nawe ni Mmenye mwenzangu"
Mkuu watu8 kwa bahati mbaya sana (refer Speaker's cv) huyu mama hata sio mwalim kitaaluma ila tu uwezo wake wa kutafsiri sheria ni mdogo sana sana, hana tofauti kwa uwezo wa kufikiri na Livingistone Lusinde (Mbunge wa Mtera) a.k.a Mzee wa matusi au kibajaji.
 
Asante , katika fasihi simulizi Mzee Mohamed Said
ni Maalim wa ukweli , tatizo lake ni moja tuu -sumu ya udini aliyofanikiwa Sana kuipandikiza, soon tutashuhudia ikimea na wakati wa mavuno ukifika patakuwa hapatoshi!.
P.

Hilo liko wazi Mkuu, na ubovu ndio hakuna mtu wa kulikemea hilo kwani kila mtu ana interest na hilo
 
Hii thread imewavua nguo bibi Makinda na ******! Ni juu yao kuchutama au kuning'iniza machenza na machungwa!
 
tunahitaji akina tundulisu kama 20 pale bungeni japo kwa mustakabali wa taifa
 
Nimebahatika kusoma na Mhe. Lissu shule moja kule Ilboru, (sio darasa moja) miaka hiyo enzi za Mkuu mmoja aitwae Bino!. Huyu Bino alikuwa ni mwalimu mkuu bingwa wa nidhamu, ila kwa Tundu, alinyanyua mikono juu na kwisha kuishusha juu baada ya kuthibitika kuwa japo Tundu alikuwa "toto tundu", ila pia ndie aliyekuwa kipanga wa darasa lake!, kwani pepa alikuwa akizifumua, utadhani mtihani katunga yeye!.

Tundu Lissu alijiunga shule ya vipanga ya Ilboru akitokea Singida, wakati huo akiitwa Antipasi Tundu, na alikuwa ni mtoto mtundu kweli!. Wakati huo, Ilboru ilichukua wanafunzi wenyeji wa Arusha, Singida na Shinyanga!. Sisi Wasukuma tukiitwa "Wasukusu", wenyeji wakiitwa "wamenye" huku jamaa wa Singida wakijiita watu wa "Singapore", uji ukiitwa "sumu", na nje kulikuwa na duka la kwa "Akwii".....

Umenikumbusha mbali, enzi za Bino (Bichwa, Binaisa) na Second master Mzava na "eh bwan mzee" mwalimu Juma....
 
Wanabodi,

Juzi katika kikao cha bunge, Spika wa Bunge, Mhe. Anne Maklnda, alimtaja Mbunge wa Singida, Mhe. Tundu kama ndie Mbunge anayeongoza kwa kuwa chanzo cha vurugu za bungeni, kwa kuongoza kwa utovu wa nidhamu, kuleta fujo na vurugu bungeni, hali ambayo sio tuu inahatarisha hali ya utulivu, amani na usalama wa bungeni, bali pia kumepelekea Spika kufuta baadhi ya ratiba za bunge ambazo zilikwisha ridhiwa na kuingizwa kwenye order paper ikiwemo kupokea hoja binafsi za wabunge, kwa kilichoelezwa kuepuka vurugu zaidi.

Jana kika cha kamati ya Uongozi kimekaa kujadili hali hiyo na matokeo yake, tutayapata kesho asubuhi baada ya kipindi cha maswali ya papo kwa papo na maswali na majibu! ni hakika rungu la kiti, lazima litamshukia Mhe. Tundu Lissu!.

Swali la kwanza la kwanza ambalo wengi mtapenda kujiuliza ni, ni jee ni kweli, Mhe. Tundu ni mtundu na ndie chanza cha utovu wote wa nidhamu wa bunge hili la kumi?, kama anavyoelezwa na Madam Speaker?, au huo utundu wa Mhe. Tundu, sio utundu bali uzingatiaji wa kanuni za Bunge, kufuatia Mhe. Spika, kuonyesha udhaifu mkubwa katika kuliendesha bunge kwa kutokuzingatia, sheria, taratibu na Kanuni?.

Kwa vile mimi ni mmoja wa watu tunaomfahamu Mhe. Tundu, Tangu akiwa Shuleni, Ilboru (sio darasa moja, Nikiwa A-level, yeye alikuwa O-Level) naomba kuchukua fursa hii kumfariji Mhe. Spika, kwa kumuomba asiumize sana kichwa chake kuendelea kubishana na Mheshimiwa Tundu Lissu kuhusu kanuni za bunge, wala wasipoteze muda kumuadhibu kwa jambo ambalo liko wazi kabisa na udhaifu unajulikana tangu chanzo chake, ulipo na labda utaendelea kuwepo, hata akiadhibiwa vipi, kwa sababu Mhe. huyu ni mbishi hakuna mfano!, haswa pale anapokuwa na uhakika kuwa yuko right!.

Nashauri Mhe. Spika, lazima ufike mahali, umkubali huyu jamaa kuwa lile jina lake la Tundu, sio jina tuu, huyu bwana analiishi jina lake kwa kuwa ni mtundu kweli pale kanuni zinapopindishwa ili kutoa mteremko kwa upande fulani!.

Nimebahatika kusoma na Mhe. Lissu shule moja kule Ilboru, (sio darasa moja) miaka hiyo enzi za Mkuu mmoja aitwae Bino!. Huyu Bino alikuwa ni mwalimu mkuu bingwa wa nidhamu, ila kwa Tundu, alinyanyua mikono juu na kwisha kuishusha juu baada ya kuthibitika kuwa japo Tundu alikuwa "toto tundu", ila pia ndie aliyekuwa kipanga wa darasa lake!, kwani pepa alikuwa akizifumua, utadhani mtihani katunga yeye!.

Tundu Lissu alijiunga shule ya vipanga ya Ilboru akitokea Singida, wakati huo akiitwa Antipasi Tundu, na alikuwa ni mtoto mtundu kweli!. Wakati huo, Ilboru ilichukua wanafunzi wenyeji wa Arusha, Singida na Shinyanga!. Sisi Wasukuma tukiitwa "Wasukusu", wenyeji wakiitwa "wamenye" huku jamaa wa Singida wakijiita watu wa "Singapore", uji ukiitwa "sumu", na nje kulikuwa na duka la kwa "Akwii".

Utundu wa Tundu Lissu ulkikuwa ni kwenye mishe mishe tuu hizi za zile, haijulikani alikuwa akisoma saa ngapi, ila pepa zikija, anafumua ile mbaya!. Moja ya maeneo ambayo jamaa alikuwa ni ni mtundu au tusema ni mbishi, ni kwenye school debate!. Jamaa akishakuwa na uhakika yuko on the right track, ni mbishi hakuna mfano!. Hata nami nilikuwa na matatizo yangu tangu shule, yale matatizo ya kawaida ya Chapa Ng'ombe, unapokutana na vibinti vya Vyeupe vya Kiarusha pale Mlimani Ilboru, ukijumlisha na lilke baridi la kule, tena wakati huo, "bwawa halijaingia luba!'...

Tundu lissu aliondoka na wani kali, akaenda Galanos hatimaye UDSM. Sisi vilaza wengine tukaishia vile vyuo vya mashenzini!. Tulipoteana kwa kipindi cha miaka 10!, tulikuja kukutana tena mjini Atlanta, yeye akiwa na yeke nami na yangu, ndipo akanieleza yuko LEAT, na huko aliichachafya serikali vivyo hivyo kama anavyo mchachafya Madame Spika, kwa kumsubu bila huruma!.

Pamoja na utundu wote huu wa Mhe. Tundu Lissu, wakati tukisubiria kusikia ni adhabu gani itamfika hapo kesho, kuna maswali matatu tujiulize!.
  1. Jee ni kweli Mhe. Tundu Lissu ni mtundu kihivyo na ndio anayeongoza kwa utovu wa nidhamu hadi kustahili adhabu kali?.
  2. Au ni Spika ndiye dhaifu hadi kushindwa kumdhibiti Tundu Lissu na utundu wake?.
  3. Baada ya kuthibitisha, Mhe. Tundu Lissu alikuwa ni mtundu toka shuleni, jee nani wa kubadilika kati ya Mhe Tundu Lissu na wabunge wa upinzani, wakae kimya wakati sheria, taratibu na kanuni, zikikiukwa, na kupindishwa?, hivyo kumpatia fursa Mhe. Spika kujiendeshea bunge anavyotaka, ili kudumisha utii, na nidhamu, bunge liwe la amani?.
  4. Hivyo Mhe Spika kuwathibitishia Watanzania kuwa hata yeye ambaye ni Spika wa majaribio ya "jinsia" "ameweza" kuliendesha bunge vizuri tuu, ambalo ni mhimili mmoja wa dola, hivyo jee, 2015, tukamilishe majaribio ya "jinsia" kwa mihimili miwili iliyobakia?, ili nchi yetu iwe ni nchi ya usawa halisi wa kijinsia?.

Wasalaam

Pasco.
(Skulu Meti wa Toto T).

Wanabodi, hii post naitumia tuu kufanya reference ya kilichotokea jana, na the role of Tundu Lissu ili kuestablishi kama ni kweli kuna tatizo kwa wapinzani, au ni muendelezo wa ukandamizaji na uminywaji demokrasia unaofanywa na kiti, ukiongozwa na dikiteta JN?!.
Pasco.
 
Mkuu Pasco hapo namba 4, matamko na mapendekezo yamepamba moto kuleta "usawa wa jinsia" hapo 2015.
 
Wanabodi, hii post naitumia tuu kufanya reference ya kilichotokea jana, na the role of Tundu Lissu ili kuestablishi kama ni kweli kuna tatizo kwa wapinzani, au ni muendelezo wa ukandamizaji na uminywaji demokrasia unaofanywa na kiti, ukiongozwa na dikiteta JN?!.
Pasco.
Hapa nafanya tuu rejea, Jumatatu nitamfutilia Tundu Lisu kwa karibu, ili kujua kama atamsumbua na Sitta kama alivyomsumbua Spika Makinda?.
Pasco
 
Hapa nafanya tuu rejea, Jumatatu nitamfutilia Tundu Lisu kwa karibu, ili kujua kama atamsumbua na Sitta kama alivyomsumbua Spika Makinda?.
Pasco

Sawa kabisa. Tunafuatilia kwa karibu
 
hapa nafanya tuu rejea, jumatatu nitamfutilia tundu lisu kwa karibu, ili kujua kama atamsumbua na sitta kama alivyomsumbua spika makinda?.
Pasco

uje na data za msingi kwani na mimi nitamfuatilia kwa makini sana huyu mbabe wa sheria.
Ukituzunguka kwa masilahi ya watu fulani nitakupnga tu!
 
Back
Top Bottom