Nitarudi kujibu comments zenu nna jazba sana hapa nikijibu lazima nitapaniki nitawajibu kwa hasira na sitoendelea na hiki kibwanga
PART TWO
usiku kama wa saa saba wazee wa kazi wakaanza kazi yao wakaanza kijisehemu chenye wamalawi wengi full kuwachapa yaani wamewachakaza sanaa usiku ulee na kuwapeleka N2- yaani barabara kubwa kwa maana wapande magari waondoke kwao wengine wamekimbilia kituo cha police unaambiwa police kama hawawaoni raia vilee nomaa ilikuwa, baada ya mda watu tukashituana kwenye group kwamba wazushi wameanza mda huu saa 7 kuganya vurugu Kwa usiku ulee wenye magari ndio waliamka na kupitia baadhi ya watu /raia wageni wenye hasira zao na kuongozana mpaka kituo cha police
Walee wazushi wakawa wanawakimbiza wageni Kwa kuwapiga na magongo usiku huo na walikuwa wanakimbilia kituo cha police basi banah baada ya watu kujaa palee kituo cha police likaanza nomaa, Kwa kuwa police walijifanya kama hawahusiki raia wakigeni waliokuwepo ikabidi wakinukishe na kuungana na walee waliokimbizwa, wamama wakigeni wakaambiwa watulie wanaume wakaanza kazi binafsi usiku huo sijakuwepo mimi nilianza kazi hasubuhi ya kuwabalasa wazushi
Mziki ulikuwa mnene zilipigwa hapo mpaka polisi wakaingilia Kwa kupiga mabomu na mabunduki juu kiufupi wajinga tuliwaweza Kwa usiku ulee wakakimbia kazi ikaanza tena hasubuhi yake
Saa kumi na moja raia tumeshaamshana na kuanza kupanga tunaanzia wapi tulikuwa wengi sanaa, wazimbabwe ni nomaa aisee hawana mzaha, tulikuwepo wazimbabwe, wabongo, wagana, wanaigeria, wamalawi, waethiopia, wasomali na wamozambiki- kilinuka hiyo hasubuhi sisi tuliamka mapema kumbe na wao walishaamka kwa kutufukuza tuondoke
Tuliwaambia kuwa atayeshindwa vitaa yeye ndiye atakayeondoka, wakuu isikieni tu vitaa ni balaa lingine kabsa yaani sio ya kuiomba hata kidogo M/Mungu nijaalie niondokane na balaa hili nikiwa mzima amini
Tunapanga maandalizi mpaka saa moja, saa moja na nusutukatoka na kuwafata walipo, kuna kajisehemu kuna uwanja ndio wanaposimamaga Kwa mikutano yao na kupanga waanzie nyumba ya nani? Tukawakuta hapo sasa bwanah hawakuamini kama tupo tayari Kwa vita Na tulikuwa wengi kinomaa yaani tukiongozwa na wenye bunduki ila walizificha mpaka waone vitaa inakomaa vipi? Tulikuwa na mapanga na magofu stiki na malungu
Haina kuuliza hiyo wao walikuwa takribani kama 100 hivi wengine waliogopa fujo mziki wa jana usiku walijua hawa wapo seriously, sisi tulikuwa wengi sanaa aisee
Tukawavamia na kuanza kuwapa kichapo na fimbo na Malungu tuliongea kuwa tusiwapige mapanga maana bado tuna muendelezo katika hiki kitongoji
Walijitahidi kupambana lakini na wingi wetu tuliwaweza tuliwachakaza sanaaa baadhi yao tuliwavunja miguu na mikono, tuliwapasua pasua yaani kama lisaa Na nusu tunawapiga tu- ndipo yakaja magari ya asikari wa kawaida yaani police tukawagomea na baada ya kupiga mabomu na kuongeza vikosi vingine ndio tukawaacha walikuwa wanalia tu yaani Kwa hicho kichapo
Mda si mda waandishi ww habari wakaja sehemu ya tukio na kuanza kutuhoji
Wapo walioelezea, kuwa serikali haioni kinachoendelea mpaka mnawaachia wanatunyanyasa kama hivi kama hatutakiwi kweli watangaze na watupe utaratibu tuondoke kiharali na mali zetu kwani na sisi tuna kwetu kinachotufanya tugande hapa ni mali zetu tu na familia zetu, kama hamtuhitaji ni mseme tu na mtuandalie mazingira tuondoke kwa amani sio kutesana kama hivi- ilikuwa hivyo
Mchezo haukuishia hapo
Hapo baadhi ya wageni wengine wapo machakani wamejificha maporini huko wapo waliohama mji Kwa kukimbia vurugu na vurugu ikiisha watarudi kuendelea na maisha yao kama kawaida
Siku hiyo ikaisha tukajipongeza sanaa , huwa tuna shushuhsu kwenye group lao la whatsapp kuwa kinachoendelea atujulishe kama kawa akatuambia nini? Kinaendelea kuwa wamepanga kesho yake wakinukishe kweli na wameapa kuwa hiyo ndio vita ya bunduki kuwa lazima wafe watu
Tukapata habari , wasomali na waethiopia na wagana na wanaigeria katatutoa hofu- wakatuambia kuwa tuna bunduki tutakuja nazo wakasema Bora watu wafe ili heshima iwepo, Na baadhi ya wabongo waliokuwa Na bastora zisizo Na vibali wakasema watakuja nazo na itakuwa poa tu
Na tukasisitizana kuwa hatutakufa sisi tu kuwa sisi tutakufa na wao pia watakufa
To be continue