Vyakula vipi umekula pindi umepigika vilivyo?

Vyakula vipi umekula pindi umepigika vilivyo?

Jkt nilikutana na ugali mchungu sana ule unga ulikua umeharibika baada ya kukaa muda mrefu store wakaamua kutulisha sisi kuruta wa Mungu.

Siku za kwanza ulikua unatushinda sasa kambini ilikua kuna eneo limetengwa la kufugia nguruwe yale mabaki ya ugali yaliyotushinda wakawa wanapelekewa nguruwe lakini hata nguruwe nao walikataa kula

Mazoezi yalivyozidi kuwa makali ilibidi tule ule ugali mchungu bila kulazimishwa maana usipopiga msosi hutoboi, licha ya kuwa nguruwe walikataa ule ugali ila sisi tuliula na tulimaliza stock
Ndiyo tatizo la viumbe ambavyo havijapitia Jeshi. Vinadeka sana. Hao nguruwe walipaswa kupitishwa JKT. Siku nyingine wasingerudia kuonesha dharau kubwa kiasi hicho!

Wanaanzaje kukataa ugali uliopikwa kabisa?
 
Ndiyo tatizo la viumbe ambavyo havijapitia Jeshi. Vinadeka sana. Hao nguruwe walipaswa kupitishwa JKT. Siku nyingine wasingerudia kuonesha dharau kubwa kiasi hicho!

Wanaanzaje kukataa ugali uliopikwa kabisa?
DAah 😂😂😂😂🙌🙌🙌🙌
 
Unaweza ukavumilia siku ya kwanza na ya pili. Kuanzia siku ya tatu na kuendelea, chochote kisicho na sumu kinaweza kikageuka kuwa chakula kwako japo hapo awali hakikuwa chakula.
Dah Mungu abariki mikono yetu iende kinywani
 
Back
Top Bottom