Uchaguzi 2020 Vyama vya upinzani vijifunze ujazaji fomu kwa wagombea wao kutoka CCM

Uchaguzi 2020 Vyama vya upinzani vijifunze ujazaji fomu kwa wagombea wao kutoka CCM

Mzalendo Uchwara

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2020
Posts
4,437
Reaction score
13,836
Najua ni ujinga na upuuzi kwa NEC kuwaengua wagombea wa vyama vya upinzani kwa makosa madogo madogo katika ujazaji wa form.

Lakini pamoja na hilo, vyama vyote vya upinzani vinalo la kujifunza hapa. Unaweza kujiuliza, mbona wagombea wengi wa CCM form zao hazina matatizo? Iko hivi;

- Baada tu ya kanuni za uchaguzi kutangazwa, CCM walitoa semina kwa viongozi wao wote (makatibu wakuu hadi ngazi za chini) juu ya kanuni hizo. Sote tuliliona hili likifanyika.

- Uteuzi wa wagombea ulipo kamilika, wagombea wote waliitwa wilayani na form zao. Wakaelekezwa waende kuzijaza sehemu ya wadhamini pekee, kisha wakapewa tarehe ya kurudi tena hapo wilayani ili kukamilisha ujazaji.

- Tarehe ya kurudi ilipofika, form, wote walirejea na viambatanishi vyote muhimu kama vile picha ya paspoti n.k

- Viongozi wa chama walizikagua fomu zote, kisha zoezi la ujazaji likaanza. Ilikua wanajaza kipengele kimoja baada ya kingine wote kwa pamoja chini ya maelekezo na usimamizi wa viongozi.

- Baada ya zoezi kukamilika, form zikakaguliwa tena, kisha zote zikarudishwa ofisi ya msimamizi wa uchaguzi ndani ya siku moja.

Jinsi CCM walivyofanya zoezi hili muhimu inakuonesha tofauti kubwa kati yao na vyama vingine. Wamelifanya kama taasisi imara yenye uongozi imara mpaka ngazi za chini. Hakukua na nafasi ya mgombea kufanya makosa ya kijinga (either kwa makusudi au bahati mbaya), au kujichelewesha kupeleka form.

Anyway, hivyo ndivyo zoezi lilivyo endeshwa hapa wilayani kwetu, natumaini utaratibu ulikua huohuo nchi nzima.

Ni lazima vyama vya upinzani vijifunze kwenye hili, la sivyo wataendelea kulia kila uchaguzi.
 
Umeamua kufanya makusudi tu, kwa taarifa yako mgombea wa ccm hata asiporudisha fomu bado nec itamtangaza kuwa mgombea, pili lazima ujue kuna vitu ni halali kwa ccm kuvifanya na ni makosa kwa wapinzani, mgombea wa ccm kiti cha ubunge njombe mjini mfatilie vizuri uone kama ana vigezo vya nec kugombea
 
Umeamua kufanya makusudi tu, kwa taarifa yako mgombea wa ccm hata asiporudisha fomu bado nec itamtangaza kuwa mgombea, pili lazima ujue kuna vitu ni halali kwa ccm kuvifanya na ni makosa kwa wapinzani, mgombea wa ccm kiti cha ubunge njombe mjini mfatilie vizuri uone kama ana vigezo vya nec kugombea
Huyo wa njombe kosa lake ni very technical, hata katibu mkuu wa wilaya asingeweza kuliona kirahisi.

Lakini nenda katizame form za wagombea udiwani wa CCM hata wale darasa la saba, hautokuta makosa ya kizembe kama kusahau kubandika picha n.k

Hii ni kwasababu chama hakikuwaacha wajaze peke yao, kiliwasimamia kufanya zoezi hilo. Na hili ni jambo zuri kwa wengine kujifunza
 
Umeamua kufanya makusudi tu, kwa taarifa yako mgombea wa ccm hata asiporudisha fomu bado nec itamtangaza kuwa mgombea, pili lazima ujue kuna vitu ni halali kwa ccm kuvifanya na ni makosa kwa wapinzani, mgombea wa ccm kiti cha ubunge njombe mjini mfatilie vizuri uone kama ana vigezo vya nec kugombea
Tadayo wa jimbo la mwanga hajasaini fomu yake lakini NEC imetupilia mbali pingamizi la mgombea wa upinzani,. Huu ni mfano mmoja ila hawa jamaa wa kijani wanajitoa ufahamu.
 
Huyo wa njombe kosa lake ni very technical, hata katibu mkuu wa wilaya asingeweza kuliona kirahisi.

Lakini nenda katizame form za wagombea udiwani wa CCM hata wale darasa la saba, hautokuta makosa ya kizembe kama kusahau kubandika picha n.k

Hii ni kwasababu chama hakikuwaacha wajaze peke yao, kiliwasimamia kufanya zoezi hilo. Na hili ni jambo zuri kwa wengine kujifunza
Tume ni ccm utake usitake, kosa umesema ni tecnical la mgombea wa njombe na kawekewa pingamizi sasa nec inasubiri nini kumtoa?
 
Kwahiyo wagombea wa CCM wanachoweza ni kujaza fomu tu!!! Kama kichwani zingekuwa zinachaji mbona midahalo wanaogopa toka ngazi ya kitongoji mpaka magogoni!
Pointi yangu kuu hapa ni chama kuwasaidia wagombea wake kwenye mambo haya.

Hili linaweza kuepusha hata wale wanao nunuliwa na kukosea kujaza form kwa makusudi.
 
Ni nani anayeweza kumuengua mgombea wa CCM kisa kakosea kujaza fomu?Anakuwa anaitaka ajira yake?Nikuambie tu,hata CCM wanakosea kujaza fomu ila kinachofanyika kwao ni kufunika kombe mwanaharamu apite!
Lakini wapinzani wanaenguliwa kwa kukosea kujaza form, hivyo dawa ni kutokukosea! Chama kiwajibike kuwasaidia wagombea wake badala ya kila kuachiwa akajaze anavyojua yeye.
 
Labda ww form ya kugombea iliotengenezwa na tume hujaiona

Form hiyo imetengenezwa kwa mitego ya hali ya juu inataka utulivu na uelewa wa hali ya juu hata ccm wakiachiwa wajaze wenyewe hawataiweza

Makosa ya kumuengua mgombea yanatakiwa yawe ya muhimu na si kukosea herufi au kujaza kwa herufi ndogo au kukosea mwaka wa kuzaliwa makosa muhimu ni yale yalioainishwa ndani ya katiba

Km uraia, umri, kuwa na akili timam,na kujua kusoma na kuandika
 
Labda ww form ya kugombea iliotengenezwa na tume hujaiona
Form hiyo imetengenezwa kwa mitego ya hali ya juu inataka utulivu na uelewa wa hali ya juu hata ccm wakiachiwa wajaze wenyewe hawataiweza
Makosa ya kumuengua mgombea yanatakiwa yawe ya muhimu na si kukosea herufi au kujaza kwa herufi ndogo au kukosea mwaka wa kuzaliwa makosa muhimu ni yale yalioainishwa ndani ya katiba
Km uraia, umri, kuwa na akili timam,na kujua kusoma na kuandika
Ni kweli kabisa, ilitengenezwa hivyo makusudi ili iwe mtego, sasa vyama vya upinzani wanapaswa kuiona hiyo mitego mapema na kuitegua.

CCM wao walihakikisha wagombea hawajazi form wenyewe bila usimamizi, waliijua hiyo mitego kwakua wao ndio waliitega.

Mbinu chafu zinafanya hadi na Trump kule Marekani ili ashinde Novemba. Ukibakia kulialia utalia milele. Ni lazima wajifunze mbinu chafu na umafia mwingine
 
Usiwajaze watu uongo ili kujenga hoja ya kuhalalisha njama na maovu yanayofanywa na CCM! Maelekezo yaliyopo kwenye zile form yanajitosheleza na yanaeleweka kabisa wala haitaji Semina wala uzoefu! Nani hajuwi kama vimeshafanywa visvyoeleweka??

Acheni kujichanganya mseme CCM ilisambaza wanasheria Nchi nzima!, Mara mseme walitoa semina! Mara walipelekwa wilayani! Wananchi sio wajinga wanelewa wazi kuwa kuna mitego inawekwa kwenye hizo form ili mgombea akijaza tu, hachomoki kwenye pingamizi au anaenguliwa kwa madai ya kukosea kujaza form!

Kuna mapingamizi mengine yametengenezwa na watu wasio wagombea lakini kwa maelekezo na ushirikiano na wanaoshughulikia hizo form alafu mtu unatoka hadharani kutamka eti hawakupewa semina na kusimamiwa! Hivi kuna vyama vinavyofanya shughuli zao kwa umakini kama wapinzani hususani CHADEMA??

Kama ujazaji wa hizo form ni lazima kusomea sheria , basi hata hao waliopita bila kupingwa hawana vigezo!
 
Ebu acha kujitekenya na kucheka mwenyewe. Vipi kuhusu mapingamizi ya akina Mwanyika (wezi) na Bona Kaluha(Mnyarwanda) kutupiliwa mbali na hayo unataka kutueleza nini? au wapinzani hawajui kujaza fumu za mapingamizi pia?
 
Usiwajaze watu uongo ili kujenga hoja ya kuhalalisha njama na maovu yanayofanywa na CCM! Maelekezo yaliyopo kwenye zile form yanajitosheleza na yanaeleweka kabisa wala haitaji Semina wala uzoefu! Nani hajuwi kama vimeshafanywa visvyoeleweka?? Acheni kujichanganya mseme CCM ilisambaza wanasheria Nchi nzima!, Mara mseme walitoa semina! Mara walipelekwa wilayani! Wananchi sio wajinga wanelewa wazi kuwa kuna mitego inawekwa kwenye hizo form ili mgombea akijaza tu, hachomoki kwenye pingamizi au anaenguliwa kwa madai ya kukosea kujaza form! Kuna mapingamizi mengine yametengenezwa na watu wasio wagombea lakini kwa maelekezo na ushirikiano na wanaoshughulikia hizo form alafu mtu unatoka hadharani kutamka eti hawakupewa semina na kusimamiwa! Hivi kuna vyama kuna vyama vinavyofanya shughuli zao kwa umakini na wapinzani hususani CHADEMA?? Kama ujazaji wa hizo form ni lazima kusomea sheria , basi hata hao waliopita bila kupingwa hawana vigezo!
Unazijua vizuri elimu za wagombea wenu? Hususani wale wa udiwani? Kuna mtu akiambiwa jaza namba yako ya kadi ya mpiga kura anajaza tarakimu peke yake anaacha ile herufi 'T', unaweza kuona ni kosa dogo lakini unaengiliwa vizuri tu kwa kosa hilo.
 
Ebu acha kujitekenya na kucheka mwenyewe. Vipi kuhusu mapingamizi ya akina Mwanyika (wezi) na Bona Kaluha(Mnyarwanda) kutupiliwa mbali na hayo unataka kutueleza nini? au wapinzani hawajui kujaza fumu za mapingamizi pia?
Chama kifuate taratibu za kisheria, kama ni kukata rufaa wakate.

Lakini pia 'what aboutism' haisaidii, kunyooshea kidole kasoro chache za upande ule haiondoi kasoro nyingi za upande wako.
 
Back
Top Bottom