Vyombo vya Dola viendelea kuwachukulia hatua wanaovaa mavazi ya kijeshi

Kama majeshi hayataki rangi zao ziigwe bora raia wakaige mabaka na mistari ya wanyama kama chui, twiga, pundamlia, fisi, chatu, kanga na tausi. Huko nako mamlaka ya uhifadhi wanyamapori nao wakichachama watu kuiga rangi za wanyama itakuaje? Anyway kama wana hakimiliki ya madoa, mabaka na mistari ya wanyama kisheria itabidi waachiwe tu. Tayari kuna nguo zenye kufanana na rangi za wanyama na raia wanazivaa na hawajui kama kuna sheria ya kukataza kufanana na wanyama. Bora wahusika wajitokeze wawaweke wazi raia wasije wakawatia hasara kwenye biashara zao
 
Mbona huna hoja, kwahiyo wakizuia raia kuvaa hayo mavazi na majambazi wakitaka kuvaa watashindwa?
Kwamba hao majambazi walivaa nguo za jeshi kwasababu raia wanavaa?
 
Kwahiyo JWTZ wapo sahihi, mabasi yalitekwa na watu waliovaa sare za jeshi.
Haya matukio yalifanya sana mipakani (hasa Kigoma) na wahalifu kutoka nchi jirani zilizokumbukwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…