Vyombo vya Habari vya Kimataifa vinapata faida gani kuzusha uongo kuihusu Tanzania na Rais Magufuli ?!. Angalia uongo/uzushi wa The Guardian la UK!

Hata Kama hali ya kisiasa sio nzuri hailazimishi kuandika uongo kusifia kinafiki bwana unaweza andikia mambo mengine nje ya siasa
 
Hebu weka ushahidi kwanza wa hzo nchi duniani zinazotusifu tulivyopambana na Covid 19
 
My Take
Hawa jamaa wanapata nini kwa kutuzushia uongo?. What do they stand to gain?. Na nyinyi Watanzania wenzetu mmafaidika na nini kwa kuwa vibaraka wa mabeberu na kutunga uongo kuhusu nchi yenu?!.
Uzalendo wenu uko wapi?.
Issue hapa (kwa Kovid19) ina anzia na watawala kuwapa huo upenyo wa kujaza pengo lililopo na "data" zao. Usipotoa takwimu muhimu zenye kuaminika basi ujue wajanja watajazia. Wewe huna takwimu na wao hawana sasa inategemea nani ana aminiwa na nani.
Tuwe waangalifu hapa, mimi ninacho ona ni watanzania wa aina fulani kujenga picha kuwa Raisi wetu ni mwamba wa korona, nchi nyingine zinamsifu, nchi nyingine zina muiga. Mwisho tuna amini hivyo na mwingine akisema vinginevyo basi balaa lina anza. Jana tulishuhudia ITV wakibinya taarifa za COVID 19 huku Tanzania kisa zilikuwa hasi, tunataka kusikia taarifa chanya lakini vitendo vyetu vingine hutia shaka.
 
Kuna watu wana masikio na wanasikia lakini hawasikilizi- serikali imesema Corona ipo na narudia Corona ipo isipokuwa wagonjwa ndio wamepungua (ama kwa kufariki au kupona) na imesema tuendelee kuchukua tahadhali.
 

Neno uzalendo halitumiki ipasavyo kwa sasa nadhani tutumie Utanzania!

Kukubali kuburuzwa, kukubali uongo, kuonewa na matakataka yote yasiyostahili kibinadamu yakikudondokea huo ndiyo 'uzalendo' wa sasa

Uzalendo huo ni ule wa mwenye shibe kumwambia mwenye njaa kuwa njaa inavumilika yakupasa uwe mpole na ukatii!

Tukirudi kwenye uzalendo wa Mwalimu, tungeuishi japo nusu tu nakuapia tungeshabadilisha kila kitu katika hii nchi!
 
Seriously? kuwa hujui faida yao? Sasa ngoja nikupe faida zao;

1.Umesema vyema; ''vyombo vya habari'', wanauza, na ni wafanya biashara, habari za Ma-Rais vichwa wa Africa, wanaovutia ushawishi wa kimataifa, ambako wazungu wana maslahi mapana kiuwekezaji nchini mwao, nchi zenye Man power kubwa km Bongo, RSA,Kenya nk lazima chombo chochote cha habari kitapata mauzo mazuri sana. ukilinganisha na Marais vilaza wale wa Yes! yes! sir! wa nchi maskini km Rwanda, Manzini, Mayote, Reunion nk!

2,Kuaminisha wananchi wa nchi zao kuwa viongozi wao ni Bora zaidi kuliko nchi yeyeote Duniani hata ambazo hazitaki kufuata ushauri na misimamo yao! wana waaaminisha kwingineko kote Duniani siyo salama! wasisafiri huko na kuiga misimamo yao!

3.Amini tu kuwa mkisemwa saana bila sababu, kuliko wengine, jua kuwa mko njia sahihi, au wanataka kuwasukumia kitu kibaya kitakacho waharibia msimamo wenu km kulileta hilo li-COVID19 maksudi tu ili watunange. kumbuka wahenga walisema, ''Hasidi hana sababu''.

3.Sababu wananchi wa USA wana hela, wanashawishi hizo hela zao wasizipeleke Tanzania kutalii, Kibiashara, kiuwekezaji nk. hasa ukizingatia kuwa mafungamano yetu na China ni makubwa, hivo wa USA na nchi za NATO kiujumla, wakija kutalii huku hela hiyo lazima iende china pia, kutufanyia manunuzi, huyu China kwa sasa ni hasimu wao mkubwa.

4.Ku-shake confidence ya Watanzania km wewe hapo umekuwa shocked na hili, na wa-Africa wengine ambao wanaweza kufuata mkumbo na msimamo wa Rais Magu. uliangalie hili suala km vita ya Maneno! siyo kamsemo tu.

5.Wamarekani baadhi yao hawaamini kwamba ni gonjwa lilioletwa na Mungu, Bali wanaamini ni Mark of Beast Plan. yaani 666, NWO, na mifumo ya kidunia, Kwa muktadha huu ni rahisi kuwageuka viongozi wao wanao sisitiza Matumizi ya PPE, na kuleta migomo na vurugu zisizo mithirika, endapo tu wataona Tanzania inafanya vyema kwa kuondoa na kuikataa Lock down. na watu wasife

6.Daima wao wanajiona wako juu kimaarifa, na kila kitu, akitokea mwenye Maarifa kuwazidi lazima auawe haraka sana, au wamzimishe kwa maneno ikibidi kwa fedha, km tulivyonyimwa hela za COVID-19 lakini wenzetu wote wa EAC Wamepewa. hapo ili tuone kijicho! tuumie! kifupi hawataki kupingwa kwa jambo lao, na wandishi wanao riport habari wanalipwa Mahela mingi, kumbuka vyombo hivyo vinamilikiwa na Matajiri wa Dunia hata wewe wakikupatia , sidhani km unge kuja humu ki hivi au, niseme una wawinda kijanja ili uitwe.

7.Hao watanzania wenzetu wanaounga mkono ni maskini, si wamepewa hela? sasa unataka wao wafe njaa ajili ya kuwatetea Mafisadi? wanao jineemesha kwa feddha ya WB, IMF wakati vitoto vyao vinakufa njaa? hata hii ulioandika hapa sidhani km hujaenda kuvuta mpunga Chato! elewa kuwa gonjwa la COVID19 ni vita hasa kiuchumi, Kisiasa, mtu yeyote anaweza kupoteza Ulaji au heshima, bila kujali, Umri, nafasi yake ktk jamii, yuko wapi kisiasa kiuchumi, kitamaduni. WEWE Mayalla umenielewa Bro.

8. Na ONYO' Kwanza hii kasumba fake, ya kuandika jina lako kizungu siipendagi, wakati wewe ni Msukuma kwisha kazi wa Nyashimba, sijui Nyakabindi huko! jirekebishe bro! na ukiri kuwa umejirekebisha ili tukusamehe! wewe ni ''MAYALA tu'' km ulivo jitanabaisha kwa kipindi pendwa cha ''Kiti Moto! ITV, na TBC'', hizi fake Double '' L'' Zimetoka wapi? kibantu hiyo inasomeka Mayalila, umebadili ID lini?. kuwa na msimamo mmoja original, mayalila au mayala utafungwa siku moja!
 
Hii umeisahau
Mkuu p Pole sana kwa kuandiak mada Ndeeefu.ila pamoja na urefu wa Bango lako,
Taarifa hii Umeisahau Mkuu
Sasa uwongo uko wapi hapa?
Ikiwa Mataifa yote makubwa na madogo wanatowa Tarifa za maendeleo ya ugonjwa Tajwa,sisi tunazuia kwa maslahi gani?
Mhe.Raisi Aliwahi kusema na kukataza watu wasizikwe usiku,lakini taarifa hii kabla ya kusemwa na BBC ilisemwa eti ni uongo,
sasa kwa nini Mh.Raisi kazuia mazishi ya Usiku na ya Kinyemela? kama ni uongo?
Tunastaajabisha sana , Maana tunasema Corona imekwisha ,kisha tunaendelea kuzuia mikusanyiko,hata ya sikukuu na ile ya Mikutano ya Kisiasa nchini.
na huku tukiambiwe tuenelee kuchukua tahadhari za kiidaktari, wakati Corona tumeshaishinda.
Si jui Muongo nani?
 
Kuna watu wana masikio na wanasikia lakini hawasikilizi- serikali imesema Corona ipo na narudia Corona ipo isipokuwa wagonjwa ndio wamepungua (ama kwa kufariki au kupona) na imesema tuendelee kuchukua tahadhali.
Tahadhari kama ile tuliyo iona coco beach ?
 
Mimi navyomuelewaga Pascal nitofauti sana na watu wanavyo muongelea au ndo niseme mimi sielewi au?


Pascal ujumbe umefika kwa waelewa.
 
Paskali hapo ndipo unapofeli na ndiyo maana unapishana na magari ya uteuzi na hata mahela ya kishindo cha awamu ya 5! wewe mara nyingi unaleta habari mbaya toka vyombo vya habari vya nje badala ya kuja na habar taaaaaamuuuu zinazosifia awam ya 5 au kama vipi nawe uwe unajibu hizo habari mbaya kupitia magazeti yetu pendwa uhuru, mzalendo, tanzanite, dailynews uone faster tu Dr. Abbass atapangiwa kazi nyingine nawe utakuwa enzin mawinguuuni
 
Zana za Kilimo na Ufipa Mangi Disco Joker (DJ) ndio vibaraka wa mabeberu, hawa ni kuwapa tu kesi za uchochezi na uhujumu uchumi kwa kila tamko lao kwenye public, kesi zikiwa kuanzia ishirini watashinda mahakamani huku sisi tukiendeleza ujenzi wa bwawa la umeme!!

Mh Ziwa Tanganyika kaharibu mno Aljazeera jana nimeona akiongea kwa English iliyonyooka kaijengea dunia taswira kuwa bongo watu milioni wanaugua korona na maiti za korona za kumwaga kila kona na zinazikwa usiku!! kasema eti serikali haisemi kweli Zana za Kilimo anataka kweli ipi? mkongoman mbishi sana yule!! Morisson kapiga faulo kiufundi kaitungua Simba ZZK anasema sio goli Manula hakuwa amejiandaa vizuri!!! mpira upigwe tena!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…