DOKEZO Vyombo vya ulinzi na Usalama taarifa hii naomba muichukulie kwa uzito mkubwa

DOKEZO Vyombo vya ulinzi na Usalama taarifa hii naomba muichukulie kwa uzito mkubwa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Tukiacha jokes za JF, ila Paul Kagame kajipenyeza sehemu zote nyeti, ule mpango wa bahima empire kuitawala Kanda yote ipo siku itatimia

Bila wazee kumaliza mission fulani huenda Leo mpango ungeshakamilika
Kabla haujatimia atakuwa amekufa kwa uzee
 
Naona mnavyojifariji,kati ya watu wako smart na sio wa kuchukulia poa basi ni kagame, hapa ametuma ujumbe amemute anasubiri reaction.
Ukubwa wa nchi usiwape kiburi,na vile sasa hivi usalama watu wanaingia kwa vimemo basi tusijiamini sana.
Mara nyingi nimekuwa nikiwambia kwa namna JWTZ walivyobweteka mtu unaweza kuingia zako kambini bila hata kustukiwa,nawapa pole maana sasa hivi majeshi yote wanaingia kwa kutafuta ajira tena uwe na connection na siyo uzalendo t kwa hiyo ufanisi unapungua kila siku.
ONYO.Jeshi letu ni la sita kwa ubora kwa hiyo mtu yeyote asijichanganye atajuta

Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app
 
Upo sahii mkuu

Si mlaumu kagame, amefanya kazi nzuri, lkn sasa afanye ya kuwaona wanyaRwanda wote ni kitu kimoja. Ahubiri maridhiano na kusameheana na upendo. Akumbuke kwamba hata akifikisha miaka mingapi, bado ataondoka. Sasa afikirie akiondoka, atawaacheje wananchi wakee. Isije ikawa kama Sudan, baada ya kuondoka Bashir nchi imegeuka machinjio na uwanja wa vita.
 
Naona mnavyojifariji,kati ya watu wako smart na sio wa kuchukulia poa basi ni kagame, hapa ametuma ujumbe amemute anasubiri reaction.
Ukubwa wa nchi usiwape kiburi,na vile sasa hivi usalama watu wanaingia kwa vimemo basi tusijiamini sana.
Mara nyingi nimekuwa nikiwambia kwa namna JWTZ walivyobweteka mtu unaweza kuingia zako kambini bila hata kustukiwa,nawapa pole maana sasa hivi majeshi yote wanaingia kwa kutafuta ajira tena uwe na connection na siyo uzalendo t kwa hiyo ufanisi unapungua kila siku.
ONYO.Jeshi letu ni la sita kwa ubora kwa hiyo mtu yeyote asijichanganye atajuta

Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app

Kwa kiasi fulani yuko hivyo. Lkn asijisahau kwamba yeye ataishi kama mlima. Kuna siku ataondoka. Swali la kujiuliza; akiondoka ataiachaje rwanda na watu wake?
 
Huko mbeya yupo dogo mmoja alitengeneza www.com ya ikulu na ya mkuu wa mkoa.

Acha mvua zinyeshe tujue panapovuja
 
Wabongo tunapenda Sana kujifariji laiti tungejua,hao miamb wanawatu wao Hadi wa kufoji vyeti na kuingizwa jeshini rasmi

Siibez nchi yangu,ila hakuna muda wa kua makini hivi sasa na baadae
Mkuu kama unawafahamu watu wa namna hiyo kwanini, tusiwataje kwa Mamlaka ziwachukulie hatua?
 
Wahuni tu wale na hawana ethic zozote za kiutawala au kisiasa bali wanatetea maslahi yao.
Mtu yoyote anaeua raia wasio na hatia ni muhuni haijalishi yupo wapi.

Ntaganda asingelazimishwa na RPF kukimbilia Kigali.

Bas na yeye ningefanya nae mahojiano kuhusu genge lake la M23 ambao ni wauza almasi na dhahabu za Congo DRC.

Eastern Kivu kuna makundi ya kihuni zaidi ya 16 ya wacongomani na wahutu na watusi na yote yanaua raia wasio na hatia
Na akitaka apewe details za biashara zipi wanafanya nchi za jirani ili kujiimarisha atawapewa?
 
Hayo ni Mambo madogo Sana ndugu,usituaminishe kuwa WAHA sio raia WA TZ.
Na wamasai,wajaluo,wamakonde,wanyasa,wailaki.
Hayo Mambo yalishapitwa na wakati.
Mjifunze kupitia Malekani,Canada mda mwingine.
Hivi Kuna Nchi Dunia ya Leo ambayo Ina watu mchanganyiko Kama Malekani.
Mbona majukumu yako palepale na unapewa ulaia kiroho safi.
Unaweza kuwa raia WA kuzaliwa usiwe na impact yoyote kwa Nchi yako.
So,Kigoma KAGERA iachieni iwe sehemu ya Rwanda basi.
Msome historia ya Nchi,kuanzia kwa machifu.
Mabalozi wetu WA CCM wao kazi yao ni kumsifia viongozi na kuhusudu teuzi.
Endeleeni hivyo hivyo na CCM yenu.

Wenzetu 90% ya mabalozi wao ni vitengo,au askari kabisa.
Sisi huku ni makada WA chama,shwaini.
 
Ninaandika haya kwa sababu nakupenda nchi yangu Tanzania kwa sababu na wewe unanipenda pia. Ninaandika haya kwa sababu sitamani hata siku moja kuona machafuko ndani ya nchi yetu nzuri ya kupendeza inayotamaniwa na kila nchi/kila mtu.

Japo nimeingilia kazi ya vyombo vya ulinzi na usalama vya nchi yetu naimani wenye kazi yenu mpo humu na kama yatakua na tija mnaweza kuyachukua na kama hayana tija mnaweza kuachana nayo japo naimani yatakua na tija kama sio kesho hata vizazi vijavyo.

Kazi ya ulinzi ya usalama wa nchi yetu ni jukumu la kila raia mwema mwenye mapenzi mema na nchi hii bahati nzuri sana mimi ni kati ya raia wema ninayeipenda nchi yangu Tanzania, binafsi kuna taarifa humu JF wakati mwingine ninazisoma kama story na zingine ninazichukulia kwa uzito mkubwa kati ya taarifa ambayo leo hii nimeichukulia kwa uzito mkubwa ni Ndugu "Vicent Karega Mnyarwanda kudai kuwa Waha ni wenyeji wa Rwanda".

Naanzia hapa hii taarifa ingekua imesemwa na mtu kama mimi pale Rwanda wala nisingejisumbua kuja na hili bandiko ila kwa sababu imesemwa na Vicent Karega basi imebidi nije na kuwapa vyombo vya ulinzi na usalama la kufikiri kidogo.

Who is Vicent Karega?

Baada ya kupitia vyanzo anuwai nimegundua huyu mtu ni mtu muhimu sana kwenye Serikali ya Rwanda chini ya Rais Kagame.

Vicent Karega alishawahi kuwa balozi wa Rwanda Nchini South Afrika, wote tunaelewa nini kilichowapata waliokua wanajeshi wa vyeo vya juu waliokua kinyume na Sera za Kagame na kuishia kwenda kuishi South Afrika wengi wao walikula vyuma waliuliwa kipindi wanakula vyuma huyu jamaa ndio alikua balozi kule.

isitoshe Vicent Karega alishawahi kuwa Balozi wa Rwanda nchi Democratic Republic of Congo wote tunaelewa kinachoendelea pale Drc chini ya M23 rais wa Congo amekua akitoa shutuma kila kukicha Rwanda ipo nyuma ya M23 sio ajabu hata Tp mazembe waliwekewa ngumu kuvaa yale maandishi.

Pia Vicent Karega Ubelgiji walimkataa kama Balozi wa Rwanda nchini mwao, tunafahamu kati ya nchi za Ulaya Ubelgiji ndio nchi yenye Intelijensia kali sasa kama wao walimkataa hatuwezi kujua sababu ila ajabu anaweza kuteuliwa kuwa Balozi Tanzania akapokelewa vizuri tu.

Baada ya kusoma ile taarifa humu Jf kuna maswali mawili matatu nimejiuliza

Vicent Karega anasema waha wapo karibia milioni 2 hebu tujiulize hizi takwimu kazitoa wapi na watu milioni 2 ni wengi sana jeshi zima la Urusi hata milioni 2 hawafiki je mpaka ametaka kufahamu idadi ana malengo gani ?

Akazidi kusema ni Kabila la tatu kwa ukubwa nchi Tanzania mimi binafsi sifahamu hizo takwimu ila Vicent Karega anazifahamu. Plse vyombo vya ulinzi na usalama najua mpo makini sana ndio maana tunalala usingizi mtamu ila naomba muongeze umakini zaidi hasa ujajusi.

Kwanini nimetoa angalizo nlishawahi kuja na uzi humu kuonyesha jinsi Urusi anavyopandikiza raia wake nchi za jirani na mwisho wake kudai raia wake wanaonewa na kuishia kuanzisha vita kafanya hayo Georgia, Ukraine, Finland, Chechnyia...nk sio ajabu leo nchi kama Finland inataka kujenga uzio kwenye mpaka wake na Urusi ili kuzuia warusi wasiingie Finland.

Je mpaka Vicent Karega ameamua kusema haya anataka kupima Tanzania itareact vipi binafsi ningependa sana nchi kama nchi itulie isijibu kitu, Je wameshamaliza kuipeleleza nchi yetu na kufahamu ubora wetu na udhaifu wetu sitaki kuamini katika hilo.

Ni kweli Watanzania tunapenda sana wageni ila kwa dunia ya sasa ni vyema tukaanza kuangalia maslahi ya nchi kwanza turudi kwenye lile Somo letu la Uraia Ulinzi na Usalama ni Jukumu la Kila Mtanzania.
 
Wanyarwanda RPF wanaamini watanzania ni wapumbavu na hawana uwezo wa kijeshi kupambana nao .Na wana mpango wa kuchukua maeneo ya Karagwe na Ngara kwa nguvu,,sema tu uwepo wa JWTZ hasa wale makomandoo wa mipakani unawatatiza na wanajua 1994 bila usaidizi wa JWTZ special forces wasingeweza kuwashinda RDF.Na RPF wanaamini kua Waha na Wahangaza na Wanyambo ni sehemu ya wanyarandwa.

Vicent Karega namjua na ndio anataka kumrithi Kagame afu siku awapime watanzania kijeshi na yamkute yale yaliyomkuta Iddi Amini.

EVERYBODY KNOWS KAREGA ALICHOKIFANYA KWA WAKIMBIZI WA KIHUTU NCHINI RWANDA NA ZAIRE 1994 UP TO 1999
nina hamu wa2vamie,,,ili tuingie rwanda nijikamatie pisi kali ya ki2si,,,,,,,nimpige mikasi mpaka anipatie mtoto!!!!
 
Rwanda hana cha kuifanya Tz, labda kwenye ujasusi wa kiuchumi maana Kagame ni smart sana ila tz tuna wachumi wa kukariri na kufundisha vyuoni na kutamba bungeni ila hawajatusaidia lolote la maana zaidi ya kuishi kwa neema ya Mungu na utitiri wa rasilimali zetu sie wakopaji mashuhuri, ila ujasusi wa kidola rwanda hana la kuitisha tz... waendelee kuwaburuza wa congo maana congo nako viongozi ni wapigaji hawajawa serious na m23.
kwahyo kwa tz rwanda ni bwana mdogo sana.
 
Niliwahi kusimuliwa kwamba miaka hiyo kitambo Waburundi waliwahi kuja na 5Bs wakiwa na mpango wa kuivamia Tz na kuliteka eneo la kaskazini mwa wilaya ya Ngara(Bugufi). Sijui nini kilitokea wakaingia mitini na mission yao so naona na Wanyarwanda wana mission na Kigoma.

Butebe
Butebuke
Bugufi
Buzaba
 Burundi
 
Back
Top Bottom