Vyoo vya Uwanja wa Ndege JNIA ni vichafu na havijafanyiwa ukarabati kwa muda mrefu

Koryo2

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2016
Posts
2,056
Reaction score
2,519
Nimesafiri kwa ndege kwa kutumia uwanja wa ndege wa Julius Nyerere kwa kupitia terminal two.

Wakati nikisubiri kuingia kwa ajili ya safari nilibanwa na nikabidi niende msalani. Nilichokikuta pale kwenye vyoo vya nje terminal two sikuamini macho yangu.

Kwa kweli vyoo ni vichafu na havijafanyiwa ukarabati kwa muda mrefu. Ni vema uongozi wakati wote wakawa wanapitia mapungufu yaliyomo kwenye uwanja huu wa Kimataifa.

Uwanja wa JNIA ni lango la Kimataifa na tuepuke aibu hii.

Nawashauri fanyeni ukarabati haraka iwezekanavyo.

Nawasilisha.
 
Vile vya nje unaweza fikiria vyoo vya bar za tandale
 
Hili la vyoo vichafu ni donda ndugu kwenye vyoo vingi vya public.

Ni aibu Sana kwa inchi yetu kushindwa kuhudumia vyoo vya public,

Kwa kweli ni uchafu mtupu.

Sent from my M2101K7BG using JamiiForums mobile app
 
Bila shaka kutakuwa na watu wa TAA humu. Nadhani watakuwa wamesoma na kupeleka taarifa ofisini kwao. Ila siku nyingine ukibanwa, jisogeze kidogo Kama unakwenda Terminal 3 , au Nenda Kabisa Terminal 3 - kule bado kupya. Nenda kale matunda ya nchi kule. Hata Kama unasafiri na local lightsโ€ฆ.
 
si ungeenda katia gogo kwa toilet ya ndegeee ๐Ÿ˜‚

wamekusikia watarekebisha
 
Bila picha unawasingizia
 
Inawezekana hicho sio kipaumbele; kwa sababu kwa taasisi kama ile itakuwa na kifungu cha ukarabati katika bajeti zao.
 
Uwe unaenda terminal 3,vipo poa
 
Asante kwa kuliona hilo.
Ni kweli kabisa nami nilipita hapo mwezi uliopita wa February nilichokiona sikuamini ila kwa kweli uongozi wa ATC ulione hili ni aibu tupu mqhali pa wasafiri wa aina mbalimbali vyoo kuwa katika hali ile.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ