CMG wakiandaa kitu ni lazima kitatoboa achana na kelele hizi za mitandaoni za wanaowabeza hapa ila kesho ndio wa kwanza kukata tiketi.
Kwenye burudani wanaanza wao alafu wanaofuatia hawafiki hata robo ya ubora wa CMG bado wanajaribu tu,redio nyingi zinaishi kutegemea ubunifu wa Clouds Fm kuanzia mpangilio wa vipindi,maudhui hadi uwasilishaji wa watangazaji narudia tena wakiamua kuandaa kitu basi jua wanachanga karata dume yaani wakiamua hata Mkuu wa nchi na baraza lake waibuke kwenye tamasha utashangaa tu mzee baba yupo pale viwanja vya Leaders.