Mkuu wa chuo
JF-Expert Member
- Feb 3, 2011
- 7,620
- 5,335
Hahahahahah, mkuu haukuona kule alivyotupangia decree ya Artashasta, lakini sheria za Wamedi na Waajemi isiyobadilika yupo fit...Mkuu unataka uletewe katekism?
Mwishowe utaambiwa we Jesuits!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hahahahahah, mkuu haukuona kule alivyotupangia decree ya Artashasta, lakini sheria za Wamedi na Waajemi isiyobadilika yupo fit...Mkuu unataka uletewe katekism?
Mwishowe utaambiwa we Jesuits!
Unajua mimi sikujua kuna vita baridi humu, watu wanaleta udini na huwa sipendi kabisa kukashifu, kuongea na kudharau kile anachoamini mwenzangu..!
Sijui Eiyer alikusudia nini lakini ikiwa ni kwa ajili ya kukashifu, atakuwa amepungukiwa sana..
heela, m'bwange ukundie masa wee, una makombere sana avae, haya sema wewe basi.Ndio maana mnaambiwa, kama hujui uliza, kama hutaki kuuliza basi kaa kimya. Ukiongea hivyo unaonekana wa ajabu.
Wakuu,
Jana nilijuwa na jamaa zangu na niliwauliza kuhusu chuo kizuri cha sheria kwakuwa kuna jamaa yangu anahitaji
Katika mazungumzo hayo kuna jamaa alitaja chuo kumoja cha kisabato ndipo jamaa yetu akasema kuwa vyuo vya kisabato havitoi degree hiyo kwasababu ya kidini,nilishangaa
Bahati mbaya pale hakukuwa na mtu mwenye majibu sahihi ya maswali yangu,naombeni mnijuze kama hili lina ukweli na kama ni kweli ni kwanini
Karibuni Ntuzu Ishmael Mkuu wa chuo charminglady Basluma Original Otorong'ong'o Nkwesa Makambo Lisa Valentine na wengine ...
Naombeni Wasabato mchimbe ni kwann mlikuwa hamsomi(Ila sijui kama hata leo vyuo vyenu mnasoma Law)kama kuna watu Wasabato wameamua kusoma Law ni kwa mapenzi yao ila Kikanisa ni kosa na nikama Umeamua kufanya kazi siku ya Jumamosi...
kumbuka huwa hamvai pete kwa wanandoa kisa eti ni utamaduni wa Kikatoliki na Rumi...Lol....Trend ni hiyo hiyo hata katika LL.B
Endelea kuchunguza maandiko ili upate maarifa na sio kupotosha umma.
shule za sekondari zenyewe hazifiki hata 10, najua shule ya Parane na Suji tu, ila kama nimesikia wana chuo kingine huko Tabata kinahusiana na issue za aviation?
Good.....Yap yap hapa sasa ndo patamu...Licha ya hayo yote ishu nzima ni hapo kwenye CANON LAW....
Ntuzu alikuwa haamini...Haya sasa..
heela, m'bwange ukundie masa wee, una makombere sana avae, haya sema wewe basi.
wasabato hawawezi kuwa na idea ya kuwa na chuo kiuu,wao wanajua tu biblia na kubishana kuhusu hiyo biblia
Nichunguze kwa mujibu na muongozo wa nani...??? Usije ukaniambie nichunguze kwa mujibu wa LESSOn na manuscript za Hellena White, please...
hakuna kitu kinanikwaza niwapo church kuona ada za UoA kuwa ni za juu kupita maelezo.... yaani hiki chuo hata sielewi mtoto wa maskini wanamsaidiaje?????? huwa naumia sana. samahani sana kutoka nje ya maada
Sio Jumamosi tuu hata Jumapili mitihani hufanyika..Kwa kifupi siku yoyote chuo kikiamua wanafunzi watafanya mtihani hakuna ubishi mtafanya tuu..
Ok mkuu...
Lkn hebu tuangalie haya malengo km yanafaa mbele ya Bwana....! Yesu alipokua hapa duniani ktk huduma zake alikua akifundisha kuokoa roho na kuponya mwili...
Sasa km malengo ya vyuo vya kisabato ni kumpatia mtu maarifa ambao ndio mwili na kuponya roho ambapo atajifunza neno la Mungu, kuna ubaya gani mkuu? Na tujiulize sheria km sheria ina nafasi gani ktk ulimwengu wa kiroho wakati katiba au sheria kuu neno la Mungu tunalo tayari?
Haya ni maoni yangu na Mimi nafatilia kujua kwanini hawatoi sheria ktk vyuo.
Ok mkuu...
Lkn hebu tuangalie haya malengo km yanafaa mbele ya Bwana....! Yesu alipokua hapa duniani ktk huduma zake alikua akifundisha kuokoa roho na kuponya mwili... .
Mbona vyuo vya kukatoliki vinalazimisha watu kufanya mitihani jmosi na wakikataa hufukuzwa? Hili mbona hawalihoji mbali na kwamba linakiuka haki za binadamu? Si bure ipo namna
Duuuuh.... Ina maana kuwa mwanasheria kwa msabato ni dhambi? Napata tabu kujua wanaendeshaje taasisi zao bila wanasheria.
Mkuu, kwanza Chuo hakikulazimishi wewe usome kitu flani ndani ya siku flani, ningependa uufute kabisa huo mtazamo wako kwanza,
Fahamu kwanza utaratibu WA Chuo umewekwa kabla hata ya mwanafunzi kwenda hapo chuoni, Na hats kwenye sekta nyingine Ni vivyo hivyo, Na hauwezi kubadilishwa Na kitu kimoja kikaathiri wengi, kwa ifupi Chuo kinapopanga ratiba fulani huwa hawaangalii Ni nani muislam au mkristu kwa sababu like siyo suala la dini, kinachoangaliwa pale Ni itifaki ya Chuo husika ambayo mwanafunzi lazima aitambue kabla ya kufanya maamuzi ya kujiunga Na Chuo hicho (hapa nazungumzia kile kipindi TCU haijakuwa Na mandate ya kudahili wanafunzi)
...sasa Kama wewe Ni muislam alaf unaenda Chuo cha kinachomilikiwa Na mfumo kristu, ujue Kuna mambo lazma yatabase kwenye ukristu Na Ni lazma uyafuate Kama ukitaka, Na huwezi sema umenyimwa haki.
Mfano mzuri Ni shule za kiislam, Kama Thaqaafa pale mwanza Na nyingine uzijuazo, (mdogo wangu Ni mkistu 100% Na kasoma pale, Na Mimi ndo nlikuwa ninampeleka so najua protocal zao hata kabla) hiyo shule wasichana Ni lazima wavae hijab, Na lugha inayotumika Ni English au Arabic, so Na mdogo wangu alivaa na hakuna aliyelalamika. Kwasababu yeye ndiye aliyechagua wakati alikuwa Na options za kwenda shule nyingine tena za kikristu.
Sasa unataka kundi flani la watu wanaoabudu j5 Na Wao jumatano iwe siku ya mapumziko?, Kama Ni hivyo mbona waislam wanafanya mitihani ijumaa Na hawalalamiki?, hilo la wasabato limetoka wapi?, au Wao ndo wana haki zaidi, ukitaka kujibu anza kunijibu kuhusu ijumaa Na waislam kuhusu kufanya kazi Na kwenda mashuleni, then uendelee.
Tafakari.