Mkuu, kwanza Chuo hakikulazimishi wewe usome kitu flani ndani ya siku flani, ningependa uufute kabisa huo mtazamo wako kwanza,
Fahamu kwanza utaratibu WA Chuo umewekwa kabla hata ya mwanafunzi kwenda hapo chuoni, Na hata kwenye sekta nyingine Ni vivyo hivyo, Na hauwezi kubadilishwa Na kitu kimoja kikaathiri wengi kwa sababu ya interest zako, kwa ifupi Chuo kinapopanga ratiba fulani huwa hawaangalii Ni nani muislam au mkristu kwa sababu like siyo suala la dini, kinachoangaliwa pale Ni itifaki ya Chuo husika ambayo mwanafunzi lazima aitambue kabla ya kufanya maamuzi ya kujiunga Na Chuo hicho (hapa nazungumzia kile kipindi TCU haijakuwa Na mandate ya kudahili wanafunzi)
...sasa Kama wewe Ni muislam alaf unaenda Chuo cha kinachomilikiwa Na mfumo kristu, ujue Kuna mambo lazma yatabase kwenye ukristu Na Ni lazma uyafuate Kama ukitaka, Na huwezi sema umenyimwa haki.
PIA ifahamike kuwa hata mitihani ya taasisi za elimu zinazomilikiwa Na serikali, huwa Kuna note inawekwa kuwa ratiba haitabadilishwa endapo tarehe ya mtihani itaangukia kwenye sikukuu za kitaifa n.k. (Christmas Na Eid nazo Ni sikukuu za kitaifa) Na hili nimeshalishuhudia Mkwawa University kipindi nipo chini ya UDSM, watu walifanya mtihani siku ya Christmas Na mwaka mpya. So usiwalaumu SAUT maana najua Wao ndo waliwafukuza wanafunzi wa kisabato walipogoma kufanya mtihani siku ya jumamosi.
Na sijui Ni haki gani SAUT waliyoikiuka, je, unaweza itaja? Na ukiitaja ueleze na mipaka ya haki za binaadamu, maana najua haki za binaadamu zina mipaka (check limitations of human rights)
Mfano mzuri Ni shule za kiislam, Kama Thaqaafa pale mwanza Na nyingine uzijuazo, (mdogo wangu Ni mkistu 100% Na kasoma pale, Na Mimi ndo nlikuwa ninampeleka so najua protocal zao hata kabla) hiyo shule wasichana Ni lazima wavae hijab, ambalo nna uhakika Ni vazi la kiislam Na lugha inayotumika Ni English au Arabic, so Na mdogo wangu alivaa na hakuna aliyelalamika. Kwasababu yeye ndiye aliyechagua wakati alikuwa Na options za kwenda shule nyingine tena za kikristu.
Sasa unataka kundi flani la watu wanaoabudu j5 Na Wao jumatano iwe siku ya mapumziko?, Kama Ni hivyo mbona waislam wanafanya mitihani ijumaa Na hawalalamiki?, hilo la wasabato limetoka wapi?, au Wao ndo wana haki zaidi, ukitaka kujibu anza kunijibu kuhusu ijumaa Na waislam kuhusu kufanya kazi Na kwenda mashuleni, then uendelee.
Tafakari.