Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kam wizauti
...
Weekend hii kwanini tupoteze muda kusasambuana... Kitu shwaaap kwenye mfereji wa Suez... then ndo tunaangalia vilivyomo kwenye vyupa na juu ya mkaa wa moto
Kabla ya salamu tuanzie hapo kwenye list!.. list ipi..??
Nenda mwenyewe mi sina hela nipo zangu skani nakunywa juisi kola na komamanga.Aahahahahahahhaaaa kuna joto kali humu tangu jana jioni.
Eeehhh banaa mambo ya kuongea kwa codes mi sijazoea.
Achana na hiyo habari tuendelee na yetu.
Twende zetu tukale samaki wa kuoka beach na ice cream za tangawizi
Nenda mwenyewe mi sina hela nipo zangu skani nakunywa juisi kola na komamanga.
He he! Hata nikikubali kwani sikujui!.. hukawii kunichenjia na kuniangalie Lile jicho chokozi!.. hapo hata siulizi Nani atalipa wallet yenyewe itatikisika..😂Kwani nimekwambia unalipa wewe???!
Haya kama umesusia ofa yangu. Usiku mwema 😆
Kibeeree banaa, usihofu navaa miwani yenye lenzi ya darubini hivyo hutohadaikwa na mboni 🤣🤣🤣😋😋He he! Hata nikikubali kwani sikujui!.. hukawii kunichenjia na kuniangalie Lile jicho chokozi!.. hapo hata siulizi Nani atalipa wallet yenyewe itatikisika..😂
Nenda tu na asprin mi kwa Leo nitaendelea na juisi kola yangu.. miwani kitu gani bhana si utaivua tu haichukui hata sekunde.. naona unaushika u Eva ili uniangamize adam..😂Kibeeree banaa, usihofu navaa miwani yenye lenzi ya darubini hivyo hutohadaikwa na mboni 🤣🤣🤣😋😋
PISI NI NENO AMBALO LIMEKUJA KUPUNGUZA UKALI WA NENO MDANGAJI,NA MDANGAJI NI NENO LILOKUJA KUPUNGUZA UKALI WA NENO KAHABA,Habari zenu watu..?
Tukiachana na yule niliekuta kanisevu "KIBERENGE" nikapiga chini,nimeamua kusonga mbele japo bado nawasiliana nae kiaina ila hakomi kuacha kuniita hivyo akinitext tu utaona text "we kibe haujambo" inaniuma sana.. tuachane na hilo
Kuna pisi moja kali niliiandikia barua.. nilijipinda mtoto wakiume na mwandiko wangu wakulala nikijitahidi kuusimamisha lkn yote hayo hakuona binti yule!.. kwenye barua nikaweka na msimbazi mmoja ili kumshawishi kusoma muandiko wa komamanga mimi..! Lkn pamoja na yote hayo alinijibu kwa kuandika nyuma ya barua "SI DATE NA POSTA MIMI!" kilichoniuma zaidi pesa alichukua hakurudisha!.
Nikaachana nae japo sikulala siku tatu mpk mbu walinizira kuniuma nafikiri hata wao pia walikuwa wakinione huruma!..
Wapili huyu alikuwa mpole nikaona hapa nimepata toto moja zuri.. nikabadili mbinu nikaona nitumie face to face approaching nisijeitwa tena posta!,so nikaanza mazoezi ya kumtongoza nikaandika na essay kabisa nikaimeza kichwani.. nikaenda mcheki sasa asalaleee lile jicho lake tu lilitosha kunisahaulisha essay zote nilizokuwa nimemeza!.. nilikuwa nakumbuka kabisa baada ya kumwambia "Mambo mrembo..? Then ningemwambia umependeza!" Baada ya hapo ndo ningeanza tiririka lkn dah! Niliishia kumuuliza tu kwenye kampeni za CHAUMA utaenda kula ubwabwa!! Mpk alinishangaa.. sijui kichwa kilipata shida gani.. hilo likapita nikajipanga tena upya kumtokea mara hii nilimfata nimeandika kabisa essay nikaanza kumsomea mbele yake lkn asalaleee komamanga la watu nilianza kutetemeka mpk sauti nayo ilikuwa ikitetemeka!. Ndugu nilichekwa mimi.. ikabidi nihairishe zoezi sahivi nikikutana nae anacheka tu na ameshanipa jina Kaka wa mikaratasi na anajua ilikuwa ni joke kumbe nilikuwa namaanisha..!
Huyo nae nikaachana nae..
Watatu sasa huyu nae ndo wale wanaitaga black beauty.. Toto fulani hivi kama twiga aliesimama kwenye mlima Kilimanjaro!
Hizi ndo zile pisi wanaita mboga saba! Unaweza hata ombea zamana na ukapata!.. komamanga la watu nikaona hapa ndo pakujitosa nikaakti kama gentleman kumbe lamba mwiko fulani tu!.. huyu kwanza nilianza pata tabu kwenye kiingereza chake tu!.. Mi naskia katamka "LILO BIL" hapo nitahangaika kujua anamaanisha nini kumbe kasema little bit!!.. hapo tu nikaanza kujiuliza hivi nimekuja kutongoza ama kutafuta changamoto!!.. ikabidi nijipe moyo tu nitatongoza hivyohivyo.
Nikajipanga siku ya siku nikamtoa out,kula sana mazagazaga kunywa sana ma wine,wisky n.k sasa kabla sijamuambia dhamira yangu akanitaka tukaogelee kulikuwa na swimming pool!. Na kuogelea sijui lkn nikaona hapa nitaonekana boya! Wacha nichukue point za umahiri asalaleee.. laiti ningejua maji ni nini walahi nisingeenda kuogelea mule!,nikajitupa kwa kujifanya mbobezi na ile step ya kwanza yakutumbukia nilienda kama mshale na hapo ndipo nilipokosea!! Naomba nisiendelee tumshukuru tu aliejuu kuwa nilitoka mzima!.. so hapo sikumuambia dhamira yangu msala wa kutumbukia kama mshale na kunywa vikombe uliharibu!..
Nilimtongoza kwa sms tu na niliandika li essay likubwa lkn alivyojibu sasa hapo ndo nilikata tamaa! Hata hakujisumbua aliandika hivi tu "UNIKOME KAMA ULIVYOKOMA KWENYE SWIMMING POOL!!".
Ndugu zanguni mi staki kuwa padri wala mtumishi.. hebu niambieni ati Nakosea wapi mbona nakataliwa hivi..??
Nenda tu na asprin mi kwa Leo nitaendelea na juisi kola yangu.. miwani kitu gani bhana si utaivua tu haichukui hata sekunde.. naona unaushika u Eva ili uniangamize adam..😂
Walimu wa kiswahili utawajua tu..😂PISI NI NENO AMBALO LIMEKUJA KUPUNGUZA UKALI WA NENO MDANGAJI,NA MDANGAJI NI NENO LILOKUJA KUPUNGUZA UKALI WA NENO KAHABA,
Sent from my itel S11 using JamiiForums mobile app
Sasa kasie hao huko juu wanikatae na wewe kweli..! Ntaishi vipi mimi..😅
Mkuu mi pisi nataka pisi Kali sitaki kuja kujilaumu! Ntakomaa nao mpk nipate mmoja wao tu na nikimpata nitamganda mpk ahisi kapata zimwi limjualo halimkuli likamwisha!..Kwa maono yangu naona kama unalazmisha kutembea wkt hata hujakaa,anza na pisi za kawaida huku ukpandisha vyeo mdogo mdogo kama jeshin,all in all huu ndo uzi ulionifurahisha tangia kujiunga jf,cjajua uliuandaa kwa cku ngap na ulifanya editing mara ngap
Haha!pisi kali zinachangamoto yake,bora ukaaanzia uswahilin kupatq experience taratiibu natumai baada ya hapo hizo pisi kali utaziona kama vipisi tu,Mkuu mi pisi nataka pisi Kali sitaki kuja kujilaumu! Ntakomaa nao mpk nipate mmoja wao tu na nikimpata nitamganda mpk ahisi kapata zimwi limjualo halimkuli likamwisha!..
Mkuu huu Uzi niliandika naweza sema nilichukua nusu saa tu.. mbona mi nauona wakawaida!.. Kuna nyuzi yangu ya "safari kwenda mirihi (a journey to mars)" hiyo ndo ilinisumbua we i search tu ipo jamii intelligence kule.