Waafrika ni muda sasa wa kurudia kuabudu Mizimu yetu

Waafrika ni muda sasa wa kurudia kuabudu Mizimu yetu

 
Waafrika wamekuwa masikini kwa sababu ya kuendekeza mizimu
 
Waafrika wamekuwa masikini kwa sababu ya kuendekeza mizimu
Duniani watu wanakwenda kwenye UJAHILIA .Wanaotaka kwenda kuabudi MIZUMU lkn itabidi hata nguo musivae tena nguo zimeletwa na waarabu pamoja na dini .
 
Toa iyo avata ndo tubishane
Hahaha avatar isikutishe maana mie ni mtu wa mixa,,,, na tena sipo kwenye huu ukristo wa wamagharibi ambao umejaa upotoshaji,,,, huyo ni kirill wa urusi wa kanisa la mashariki nachanganya mizimu na ukristo wenu maana nimeona nao ni ibada ya mizimu tu sema kwakua wamepewa majjna ya kizungu wanaitwa saints/watakatifu basi mkaridhika mie mababu zangu na mizimu ya kwetu nao ni watakatifu na nawaomba kama mnavyoomba hao watakatifu wa kizungu sababu najua mtu mweusi alimjua mungu kabla hata kuletewa hizo dini za wageni na sikikuu zenu za kidini nazitumia kama sikukuu/matambiko kwa wazee
 
Wewe na myahudi ni nani mwenye Dini yake.... myahudi mwenyewe kwenye torati anaambuwa hasiuwe, yeye kule Gaza anauwa.

Alafu unataka kujifanya mfia dini kuliko Myahudi... Hata waluokuwa wanaabudu Mizimu bado nao maombi yao yalifanya kazi... Wewe hupo leo kwa sababu miungu iliwalinda babu zako huko miaka mingi kabla ya hizi Dini.... Kwa hiyo babu yako aliyefariki karne ya 7 bila kujua ukristo yeye aliwezaje kuishi
Sasa mkuu Exodus 22:2
Inazungumzia kuhusu kuua mwizi.

Ni hivi kuna Murder na Killing hivyo ni vitu viwili tofauti, mahakamani unaweza kwenda na umeua na ukaachiwa huru...
 
Hahaha avatar isikutishe maana mie ni mtu wa mixa,,,, na tena sipo kwenye huu ukristo wa wamagharibi ambao umejaa upotoshaji,,,, huyo ni kirill wa urusi wa kanisa la mashariki nachanganya mizimu na ukristo wenu maana nimeona nao ni ibada ya mizimu tu sema kwakua wamepewa majjna ya kizungu wanaitwa saints/watakatifu basi mkaridhika mie mababu zangu na mizimu ya kwetu nao ni watakatifu na nawaomba kama mnavyoomba hao watakatifu wa kizungu sababu najua mtu mweusi alimjua mungu kabla hata kuletewa hizo dini za wageni na sikikuu zenu za kidini nazitumia kama sikukuu/matambiko kwa wazee
Kumbe ni mtu wa misa 🤣🤣sasa kumbe hadi kanisani unaendaga kumbe
 
Rejea kichwa cha habari tajwa hapo juu.

Dini ndio chanzo cha matatizo mengi Duniani. Katika Dunia ya leo raia wanakosa ushirkiano tu kwa sababu wanatofautiana Kidini, Mkristo anambagua Muislamu na Muislamu anambagua Mkristo. Na ubaguzi wa kidini hauzungumzwi sana ila kiukweli ndio unaotendeka kwenye ofisi nyingi na taasisi nyingi, siku hizi ubaguzi wa kikabila unaenda ukipungua, huku ubaguzi wa kidini ukizidi kukuwa.

Je Dini zilianza kuingia Afrika karne zipi;

Dini za Kiislamu na Ukristo zilianza kuingia Afrika muda mrefu uliopita. Ukristo uliingia Afrika kwa mara ya kwanza karne ya 1 BK (Baada ya Kristo) kupitia wamishonari na biashara na Waafrika wa Kaskazini. Ukristo uliendelea kuenea katika maeneo tofauti ya Afrika.

Uislamu ulianza kuingia Afrika katika karne ya 7 BK (Baada ya Kristo) kupitia kazi ya Muhammad na Waislamu wa kwanza. Kupitia biashara na uvumbuzi wa safari za jangwani, Uislamu ulienea kwa kasi katika maeneo mengi ya Afrika, haswa katika Afrika Kaskazini.

Je Kabla ya Dini hizi waafrika tulikuwa tunaabudu nini?

Kabla ya kuingia kwa dini za Kiislamu na Ukristo, tamaduni za Kiafrika zilikuwa na dini na imani za kiasili zilizojumuisha ibada ya miungu ya asili, roho za wafu, na nguvu za asili. Dini za Kiafrika zilitofautiana sana kutoka eneo moja hadi lingine na kati ya jamii tofauti za Kiafrika.

Mara nyingi, dini za Kiafrika zilijumuisha ibada ya miungu au roho za wakubwa wa kale, kama vile mababu au wazee wa kabila. Kwa mfano, jamii nyingi za Kiafrika ziliabudu miungu ya jua, mvua, na ardhi, kwa sababu vitu hivyo vilikuwa muhimu kwa maisha yao ya kila siku.

Dini za Kiafrika pia zilijumuisha ibada ya wazee na mababu waliokufa, kwa kuwa waliona kumbukumbu na heshima kwa wafu kama sehemu muhimu ya utamaduni wao. Imani hizi za kiasili zilikuwa sehemu ya utamaduni wa Kiafrika na zilisimulia hadithi za uumbaji, maisha, na mazishi.

Kwa hiyo, kabla ya kuingia kwa dini za nje, Waafrika walikuwa wanaabudu miungu yao ya asili na walikuwa na imani za kiasili zilizohusiana na maisha yao ya kila siku na utamaduni wao, na maombi yalikuwa yanafanya kazi.

MY TAKE: Ukitizama Dini hizi za Ukristo na Uislamu ni dini zilizoletwa tu Afrika. Walikuja na kutuambia Imani zao ni bora kuliko zetu, hivyo tuache Imani zetu tufate Imani zao. Dini hizi mbili zinaimiza katika Kusameheana, kutokuua, kutokudhuru, na zinaamini katika Kupendana. Inasikitisha sana hawa wenye dini zao wamekuja Afrika na kutuhubiria Amani lakini wao hawafuati hiyo Amani wala hayo mafundisho. Mbona wenye dini zao wenyewe Waisraeli na wapalestina wameshindwa kufuata maandiko na wanauana kama kuku, inakuaje mimi muhaya wa Bukoba ambaye hapo mwanzo nilikuwa naabudu mizimu nifuate maandiko hayo ambayo wahusika wenyewe wameshindwa kuyafuta.

Mimi kwa mtazamo wangu naona walitumia dini zao kama chambo hili kutuweka katika ukoloni miaka hiyo maana waarabu ndio walikuwa walanguzi wa watumwa kisha wanaenda kuwauzia wazungu. Hivyo walitumia mafundisho ya dini zao kutufanya kutufumba akili na uwezo ili iwe rahisi kututawala.

Mbona hatuoni ishara yoyote kutoka juu kwa muumba mwenyewe baada ya mapigano hayo, maana tunaambiwa maeneo yale ni matakatifu, hivyo kwa akili tu lazima kungetokea ishara ya kukataza mapigano, ila naona tu Aliakibar ndio nyingi huko Gaza, huku Shalom zikiwa nyingi huko Israel.
Kila mtu akiomba mwenyezi hamsaidie.

Sasa tumeona ni namna gani Dini hizi za kuletwa vile hazifanyi kazi, ni bora kurudi kwenye kuabudu Mizimu yetu ambayo hapo mwanzo tulikuwa tukiiomba, mwandishi mashuhuri wa vitabu Yericko Nyerere aliwahi kugusia hili, kwamba turudi kwenye Imani zetu za hawali, na mimi sasa naona umuhimu wake
Ujui ulicho kiandika sababu mpaka sasa robo tatu ya watu bado waabudu mizimu na binadamu wenye hela robo tu ya watu ndio wanao muabudu muumba wa kweli

Tofaoti iliopo kwa zama hizi na zakale babu zetu walijiweka wazi bila kuficha zama izi watu wanajificha kwenye dini lakini wacho kiabudu wanakuja wao

Enzi za mkwawa na mwana marundi ubaguzi ulikuwepo tena mbaya zaidi ya huu
 
Hata hivyo kiuhalisia bora hali ilivyo sasa, lakini tukisema turudi kwenye dini zetu hali ingekuwa mbaya, makabila karibu 120 Kila mmoja na dini yake imagine, Leo hii watu wa makabila mbalimbali wanaweza kupatana kwasababu ni wakristo au waislamu, Bora kuwe na pande mbili zinazozozana ambapo kutuliza migongano inaweza kuwa rahisi kuliko kuwa na dini 120 ambazo kukitokea migongano hasa ikiwa kwenye Karne hii ya sayansi na teknolojia na uwazi plus kujitambua kutazuka balaa kubwa ambalo ili liishe lazima dini karibu 100 zihusike in which is impossible.

Hata kiutawala itakuwa ni ngumu mno. Kumbuka dini zetu zile zinakwenda sambamba na makabila au ukabila hivyo jambo baya kutokea miongoni mwa makabila ni dakika sifuri tu tena hapo hujasema influence ya mataifa makubwa kwenye kutuchanganya vizuri kiutamaduni.

Kwa kuwa wengi wetu TZ hatujitambui hizi dini mbili kubwa zinatosha kabisa, dini zaidi ya 100 Kwa jamii isiyojitambua ni mzigo mzito mno. Fikiria mtu anasema kuwa wenye dini Yao aidha wayahudi au waarabu wanauana so what?, kwani sisi Babu zetu na dini zao walikuwa hawauani aidha kutoa makafara ya watu au hata zile vita za makundi ya kikabila, kule kaskazini mbona walikuwa wanapigana hadi machifu wa kabila moja na kuuana kabila moja licha ya hizo dini za mizimu kuwepo.

Hivyo, mapigano kama Yale ya mashariki ya kati dini zinakuwa ni kama kisingizio tu. Watu wana mahangaiko Yao hapa duniani wanaamua kuuana tu, waache wauane maana Kila mmoja ana EGO.
 
Back
Top Bottom