Waandaji wa ASFC: Uchaguzi wa Uwanja wa kucheza uwe kwa kuzingatia Ubora na Ukubwa

Waandaji wa ASFC: Uchaguzi wa Uwanja wa kucheza uwe kwa kuzingatia Ubora na Ukubwa

Mpira wa jana kutokana na ukubwa wa Simba umeangaliwa na Mataifa mbalimbali lakini ubovu wa uwanja mpira uligeuka butuabutua, undava na kukamiana hata kadha ya mpira haikuwepo, next time TFF mechi km hizi zipigwe Taifa tu
 
Mimi naunga mkono juhudi za TFF kupeleka mechi hizi kwenye Mikoa ambayo haina timu za ligi kuu. Lengo ni zuri sana na kiuhalisia limesaidia sana kuleta hamasa ya michezo na mapato kwa wafanyabiashara wa mikoa husika.

Kuhusu pitch ya kuchezea tumeona jinsi uwanja ulivyoenda kupandwa nyasi hivi karibuni na kufanikiwa kuwa vile. Kwakuwa Serekali tayari imehaidi kuleta nyasi bandia na kuboresha viwanja hii hoja inaweza kuwa solved iwapo watakarabati na kuongeza majukwaa ili kuweza kuruhusu kuingia watu wengi.

Kwa ile mechi ya Kigoma ingekuwa wanacheza fainali Biashara na Azam wala tusingeona haya mapungufu ya uwepo wa majukwaa kwa kuwa idadi ya watu uwanjani ingekuwa ndogo. Hivyo point ya mtoa mada inamashiko iwapo timu za Simba na Yanga ndio zitafika fainali.
 
TFF wanaingiza siasa kwenye hii michuano, wajifunze nchi kama UK fainali inachezwa wembley lakini sisi tunapeleka fainali kwenye viwanja vibovu ambavyo haviwezi kubeba watazamaji wa kutosha.
 
Kwa mujibu wa msemaji wa Azam FC, ZakaZakazi, ukubwa wa dimba (pitch) la Azam Complex ni sawa kabisa na ule wa Benjamin Mkapa.

Aliyaongea hayo alipokua anatoa ufafanuzi na kushangazwa na uamuzi wa CAF kuwazuia NAMUNGO kutumia uwanja wa Azam katika mechi za makundi za kombe la shirikisho barani Afrika.
Hata kwa kuangalia kwa macho tu unaona ni sawa au huwa huangalii mpira?
 
Hivi viwanja vya CCM kama wamevisahau chama hakikosi ela ya kuviboresha hata kimoja kimoja ili kuendana na nyakati zilizopo kuna vingine kama mbeya pale ule sio uwanja
 
Kwanza nawapongeza kamati mahususi kwa ajili ya Uandaaji wa Kombe la Shirikisho maarufu kama Azam Federation Cup. Hakika kila mwaka kuna maendeleo kadri ambavyo linazidi kusonga mbele. Hakika mnazidi kufanya soka la Tanzania lizidi kupiga hatua mkishirikiana na TFF.

Lakini pamoja na jitihada nyingi, kuna kasoro ambazo lazima mzitatue ili kufanya mashindano yenyewe yalete hisia na msisimko wa aina yake.

Moja, ni uchaguzi wa uwanja maalum kwa ajili ya kupigia mchezo wa fainali. Logic yenu ya kuchagua viwanja katika mikoa ambayo hazina timu Ligi Kuu ili kuleta chachu ya maendeleo ya soka katika mikoa husika ni nzuri sana.

Lakini, lazima tukubaliane na ukweli kuwa mechi ya fainali inakutanisha timu bora katika mashindano hayo. Na kwa kuwa ni mechi ya kuhitimisha mashindano husika, lazima tuzingatie ubora wa pitch, ukubwa wa pitch na uwezo wa kubeba mashabiki.

Kwa siku ya leo, mechi ilikuwa ya hovyo na isiyovutia kabisa. Kwa mtu ambaye huenda labda haijui Simba na Yanga, kufungulia chaneli angelijua ni mechi ya timu za mtaani tu.

Hakuna mipira ya kueleweka. Ni butua butua tu. Uwanja umebana sana. Mipango ya mwalimu inafeli na matumizi ya nguvu yanazidi katika kupigania mpira. Mchezo unakosa ladha

Mpaka inawapa wachezaji shida kupimia kiwango cha force cha kupiga mipira. Mara nyingi mchezaji anapiga mpira akidhani itafika mahali fulani, lakini inazidi kiwango. Kama ulimuangalia Chama, kona mbili zote zinafika karibu na kona ya upande mwingine.

Mechi ya fainali ichezwe katika viwanja vikubwa na vyenye uwezo wa kubeba idadi ya mashabiki wengi. Watazamaji 20k kwa mechi ya watani wa jadi ni ndogo sana.

Boresheni mashindano na hakika yataizidi kuvutia.

Mwisho, naipongeza sana timu ya Mabingwa Simba SC kwa kutwaa tena kombe hili. Hakika tunastahili tena na tena.
Hilo ulilosema lipo wazi uwanja uliotumika haufai hata kwa mechi za nusu fainali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa kuongezea, wangetenga viwanja kwa kanda na kisha wao wakaiboresha pitch kwa kushirikiana na TFF.

Mfano wachague Dar, Dodoma,Mbeya, Tabora, Arusha na Mwanza.

Zinatisha sana hizo sehemu ku host fainali msimo mmoja hadi mwingine.
Kwahio chie watu wa lindi na ntwara chio watanzania
 
Hata kwa kuangalia kwa macho tu unaona ni sawa au huwa huangalii mpira?

20210726_202742.jpg


Kaa humo mkuu
 
Back
Top Bottom