Waarabu wa Morocco Wawashangaza Waafrika

Waarabu wa Morocco Wawashangaza Waafrika

FaizaFoxy

Platinum Member
Joined
Apr 13, 2011
Posts
100,246
Reaction score
123,145
Baada ya nchi za Kiafrika Mali, Burkina Faso na Niger kutengwa na Waafrika wenzao ndani ya umoja wa ECOWAS na kutiwa adabu ya kufungiwa biashara zote, kufungiwa umeme na huduma zote za kibinadamu hadi chakula.

Wametengwa baada ya nchi hizo kupinduwa serikali zilizokuwa zinajineemesha kwa kundi la watu fulani tu na wakoloni waliokuwa wakiwadanganya kuwa wanaweza kuwalinda daima.

Cha ajabu, nchi za Kiafrika kama Nigeria na zote wanaowazunguka zilikutana na kuamuwa kuwatenga wenzao kwa kuwasikiliza wakoloni.

Katika sherehe za miaka 48 ya Morocco Mfalme Mohamed wa Morocco akatangaza kuzibeba nchi hizo zilizotengwa nankuwekewa vikwazo kwa hali na mali, na potelea mbali nchi zingine zote zilizowatenga zifanye zinavyotaka.

Amewaruhusu watumie bandari zake, Barabara na Raiway na amejitolea kujenga reli, barabra za kuwafikisha bandarini. Pia amewaambia na kuwaahidi kuwa chochote wanachohitaji wasihangaike, hao ni ndugu zake. Bila kuongea, ameonesha kuwa uzalendo wa Afrika haupo kwenye rangi zetu bali kwenye nia na mioyo yetu.

Viongozi wa nchi hizo walitokwa na machozi baada ya Mfalme wa Morocco kutangaza hayo bila kuombwa wala kutowa dalili za awali. Wanasema hawajategemea.

mengine zaidi jionee mwenyewe:


View: https://youtu.be/Eva9vB5Cexo?si=MC3nny7LL4Z6fnKM
 
Moroco ni waarabu wapo Africa kwa bahati mbaya
Uarabu siyo rangi kijana. Wapo waarabu wengi sana weusi jirani zako tu, hapo Sudan.

Uarabu ni lugha na tamaduni.

Wewe siyo mstaarabu?

Hao unaowaona wewe Waafrika wa kweli ni nani kasimama kuwatetea hao vijana waliopinduwa huko, zaidi ya Mfalme Mohamed wa Morocco?

Tena si kuwatetea tu, na kuwashika mkono kuwanyanyuwa mpaka waweze kusimama wenyewe.

Hii kwa vyovyote ni historia ambayo haijawahi kutokea Afrika na hata duniani.
 
Tafsiri ya kinachoongewa post namba moja, kwa msaada wa google (bado naendelea kui edit kidogo kidogo).

Alichokifanya Mfalme wa Morocco siyo tu kimeistuwa imeshtua sio tu Afrika lakini pia Dunia nzima. Mmorocco ni Mwafrika ki nchi hata ki watu. Niwanaona ni vigumu kuamini kwa sababu ya weupe wa ngozi ya Wamorocco na lugha ya Kiarabu wanayozungumza, lakini "genetics" zao Kisayansi zinasema Wamorocco wana kila vinasaba vinaonesha kuwa wana undugu wa karibu sana na Waafrika weusi.

Baada ya mapinduzi nchini Niger, Mali na Burkina Faso nchi za Afrika (ya weusi) Kama Nigeria, ilianza kujiondowa upande wao. Walienda mbali hata kutishia kutumia nguvu na wakaweka Vikwazo kuwa vibaraka wa Magharibi. Hiyo ndiyo iliyofanya mambo kuwa mabaya zaidi kwa Mali, Niger na Burkina Faso kwa sababu ni nchi kavu (zisizo na bandari) na vikwazo vya kuwakataa Kote duniani hasa kwa Biashara. Hapo ndiyo wakati Morocco ilipoingia kati na kumshangaza kila mtu.

Lakini ni nini kiliwafanya hivyo pamoja na Ecowas ikiongozwa na Nigeria kuwa kibaraka? Auu vitu Vinginevyo vilivyojificha?

Kijografia imekuwa ni adhabu kubwa kwa Niger, Mali na Burkina Faso. Niger Mali na Burkina Faso ziko Afrika Magharibi ni mataifa yasiyo na bandari, ambayo yameshindwa patikanaji wa huduma za Bahari kwa sababu ya vikwazo walivyowekewa na ndugu zao. Kijiografia nchi hizizinategemea sana nchi jirani Ndani ya Jumuiya ya Kiuchumi ya Magharibi kwa ajili ya biashara na upatikanaji wa mahitaji ya binadam ya kila siku. Kutengwa kwao na kuwekewa vikwazo na ndugu zao imekuwa chanzo cha matatizo Katika kukabiliana na mapinduzi ya kijeshi ya hivi karibuni katika Mataifa haya matatu ya Ecowas.

*mengine tutaedeleza kwa maswali yatakayojitokeza.
 
Hakuna kitu chabure kwenye hii capitalist world
Naam, kweli kabisa lakini wako wapi ndugu zao weusi? Mbona wamewatenga wasiitumie firsa hiyo ya "hakuna cha bure"?

Nafahamu, wengi mtaumizwa kwa hili na sababu nnazijuwa. Lakini ndiyo ukweli huo.
Hakuna nchi ya Africa isiyoongozwa na super power, kuna kitu kinaitwa mfumo, na mfumo ni muunganiko wa vitu vingi vinavyounda kitu kimoja, na kitu kimoja hakiwezi kutoa au kusimama chenyewe bila kuongozwa na vijimfumo vidogovidogo vinavyounda mfumo kamili
 
Hakuna kitu chabure kwenye hii capitalist world

Hakuna nchi ya Africa isiyoongozwa na super power, kuna kitu kinaitwa mfumo, na mfumo ni muunganiko wa vitu vingi vinavyounda kitu kimoja, na kitu kimoja hakiwezi kutoa au kusimama chenyewe bila kuongozwa na vijimfumo vidogovidogo vinavyounda mfumo kamili
Kwa hiyo "mfumo" wako huo ndiyo ulikuzuwia kuwapa mahitaji muhimu ndugu zako?
 
Wametengwa baada ya nchi hizo ku[induwa serikali zilizokuwa zinajineemesha kwa kundi la watu fulani tu na wakoloni waliokuwa wakiwadanganya kuwa wanaweza kuwalinda daima.

Cha ajabu, nchi za Kiafrika kama Nigeria na zote wanaowazunguka zilikutana na kuamuwa kuwatenga wenzao kwa kuwasikiliza wakoloni.
Ule usemi unaosema Mwislam ni ndugu wa Mwislam hao waislam wa Africa wameamua kuukana?
 
Bibi zee jeusi linashadadia miarabu. Angalia hapo chini kwenye video hao miarabu wenzako walivyowafanyia waliberia. Wamewalaza sakafuni na wakawapeleka wazungu hotelini na walisafiri pamoja kwenye ndege moja. Huyo ni waziri kutoka Liberia.

Mxiuuuu black granny.


View: https://www.youtube.com/watch?v=vhe3P9k28Ho&pp=ygUoTW9yb2NhbiByZWZ1c2luZyBsaWJlcmlhbiB0byBib2FyZCBwa2FuZQ%3D%3D

Hayo matukio yapo sana tu.

Mimi naongelea kuziokowa nchi tatu kwa mpigo, au hujaiona mada? Siongelei matukio kwenye huu uzi, naongelea maendeleo.
 
Baada ya nchi za Kiafrika Mali, Burkina Faso na Niger kutengwa na Waafrika wenzao ndani ya umoja wa ECOWAS na kutiwa adabu ya kufungiwa biashara zote, kufungiwa umeme na huduma zote za kibinadamu hadi chakula.

Wametengwa baada ya nchi hizo kupinduwa serikali zilizokuwa zinajineemesha kwa kundi la watu fulani tu na wakoloni waliokuwa wakiwadanganya kuwa wanaweza kuwalinda daima.

Cha ajabu, nchi za Kiafrika kama Nigeria na zote wanaowazunguka zilikutana na kuamuwa kuwatenga wenzao kwa kuwasikiliza wakoloni.

Katika sherehe za miaka 48 ya Morocco Mfalme Mohamed wa Morocco akatangaza kuzibeba nchi hizo zilizotengwa nankuwekewa vikwazo kwa hali na mali, na potelea mbali nchi zingine zote zilizowatenga zifanye zinavyotaka.

Amewaruhusu watumie bandari zake, Barabara na Raiway na amejitolea kujenga reli, barabra za kuwafikisha bandarini. Pia amewaambia na kuwaahidi kuwa chochote wanachohitaji wasihangaike, hao ni ndugu zake. Bila kuongea, ameonesha kuwa uzalendo wa Afrika haupo kwenye rangi zetu bali kwenye nia na mioyo yetu.

Viongozi wa nchi hizo walitokwa na machozi baada ya Mfalme wa Morocco kutangaza hayo bila kuombwa wala kutowa dalili za awali. Wanasema hawajategemea.

mengine zaidi jionee mwenyewe:


View: https://youtu.be/Eva9vB5Cexo?si=MC3nny7LL4Z6fnKM

Hivi mauaji yanayofanywa na Magaidi wa kiislam kule Somalia na Sudan huyaoni?

Jifunze kukemea wenzako pia
 
Jiulize wewe Waafrica wote wako wapi?
African Union ilitegemewa kutoa tamko la kuunga mkono na kulaani uvamizi uliotaka kufanywa na France na ndugu zao! Lakini kwa kuwa viongozi wa Africa wengi wao kuwa vibaraka wakaufyata!! Kasoro Kagame.
 
Bila kuiweka Algeria kwenye equation, basi mtakua mnaliangalia hili suala very superficially.
Hizo nchi zina population kubwa ya Barbers na Touaregs. na kabla ya hapo miji kama Timbuktu na Djene ni miji muhimu kwa sahel na maghreb regions kiuchumi na kijamii.
Kiufupi Sahel region ni muhimu kwa Maghreb kuliko ilivyo Maghreb kwa Sahel . Hakuna mambo ya mapenzi hapo.
 
Back
Top Bottom