Wabobezi wa sheria tunaomba tafsiri ya kisheria tofauti ya mtuhumiwa kufutiwa mashitaka na mtuhumiwa kusamehewa mashitaka..

Wabobezi wa sheria tunaomba tafsiri ya kisheria tofauti ya mtuhumiwa kufutiwa mashitaka na mtuhumiwa kusamehewa mashitaka..

baba anjela

JF-Expert Member
Joined
Mar 17, 2013
Posts
431
Reaction score
310
1.Wabobezi Wa sheria naomba mtupe tafsiri kati ya kusamehewa mashtaka na kufutiwa mashtaka....

2.Kati ya kusahewa mashtaka na kufutiwa mashtaka ni njia ipi inamsafisha mtuhumiwa mbele ya macho ya jamii....

3.Ni njia gani ya kuondolewa mashitaka inamtofautisha mtuhumiwa alietenda kosa na mtuhumiwa aliesingiziwa kutenda kosa.
 
Mkuu baba anjela, naomba nichangie mada yako. Naweza kuwa si mbobezi wa sheria unayemtarajia lakini kwakuwa nami ni Mwanasheria na Wakili Msomi, nawiwa kuchangia jambo hili.

Mosi, kuna tofauti ya kuondoa/kufuta mashtaka na kusamehe mfungwa. Kuondoa/kufuta mashtaka hufanywa na Ofisi ya Mashtaka ya Taifa inayoongozwa na Mkurugenzi wa Mashtaka kupitia kwa Mawakili Wasomi wa Serikali wanaoendesha kesi husika. Hili hufanyika kabla ya kesi husika kuhitimishwa kwa kutolewa hukumu. Mara zote, kifungu cha 91 (1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, Sura nambari 20 ya sheria za Tanzania hutumika.

Msamaha hutolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa wale ambao wameshapatikana na hatia na kuhukumiwa adhabu mbalimbali katika kufaidi mamlaka yake yaliyopo kwenye Ibara ya 145 (1) aya ya (a) hadi (d) ya Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Yaani, msamaha hutolewa kwa wafungwa. Hadi hapo, iko wazi kuwa Rais hana mamlaka ya kufuta/kuondoa mashtaka ya washtakiwa ila ni Mkurugenzi wa Mashtaka. Rais ana mamlaka ya kutoa msamaha kwa wafungwa.

Kimsingi, kwa ilivyo na ilipo kesi ya Mbowe na wenzake, Mkurugenzi wa Mashtaka aweza kuondoa/kufuta mashtaka dhidi yao. Hapo (kwakuwa hakuna hukumu bado) hakuna suala la kusamehewa kwa akina Mbowe.
 
nakumbuka Adden Rage alifungwa gerezani, alipopata msamaha wa rais akaappeal mahakama ikamfutia makosa kwamba alitiwa hatiani kimakosa, hakuwa na hatia.

Kwa mwelekeo wa roho mbaya aliyoidhihirisha, anaweza akalazimisha atiwe hatiani kisha ajifanye amempa msamaha. Ili wazime harakati zake za kisiasa. Maana Freeman ni mwiba kwao.
 
1.Wabobezi Wa sheria naomba mtupe tafsiri kati ya kusamehewa mashtaka na kufutiwa mashtaka....

2.Kati ya kusahewa mashtaka na kufutiwa mashtaka ni njia ipi inamsafisha mtuhumiwa mbele ya macho ya jamii....

3.Ni njia gani ya kuondolewa mashitaka inamtofautisha mtuhumiwa alietenda kosa na mtuhumiwa aliesingiziwa kutenda kosa.
Usiwe kama Kiroboto tumesema unamsamehe vipi mtu ambaye hajakuwa na hatia., mtu hajakukosea vipi unamsamehe? Mtie hatiani kwanza halafu ndio ulete izo longolongo
 
Back
Top Bottom