Wabongo watakulinda mitandaoni lakini sio wakati unatekwa

Wabongo watakulinda mitandaoni lakini sio wakati unatekwa

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001

Moja kwa moja kwenye hoja

Nimeshangazwa sana na mazingira aliyotekwa kiongozi wa Chadema. Sishangazwi kwa sababu ni kiongozi wa upinzani bali ni mazingira aliyotekwa.

Mimi sikuwepo, lakini najaribu kufikiria tu, iliwezekanaje? Otherwise aliyekuwepo anisahihishe.

Najaribu kuwaza hivi....kuna taharuki ya utekaji imeenea. Polisi wakilaumiwa. Viongozi wa dini wamesema. Kule Busega waliandamana mpaka mtu akauliwa na polisi. Katika hali kama hiyo maana yake wananchi tulitakiwa kulindana sisi kwa sisi. Kwamba hatutakuwa tayari kuruhusu mtu akitwaliwa katika mazingira yasiyoeleweka. Lazimu tuzuie hilo tukio kwa hali na mali hata kama damu itamwagika.

Lakini watu wameingia kwenye bus wakamshusha yule jamaa wakaondoka naye. Sifikirii kama alitulia tu, obvious alikomaa kwanza na kujisanua. Mwisho watekaji wakafanikiwa kumteka mbele ya abiria.

Maana yake kwenye jamii kama hii ambayo serikali haina habari na ulinzi na usalama wa raia wake, unapaswa wewe mwenyewe binafsi kujilinda. Usijekusubiri maraia watapika kelele wakati unatekwa. Wao watasubiri kupiga kelele mitandaoni na Jamiiforums tu. Muda huo umeshachezea kichapo kikali na hata kifo.

Na hiki chama kinachoteka watu kuweni na huruma basi. Kweli unamteka mtu kwa sababu tu kakukosoa?
 
View attachment 3090098
Moja kwa moja kwenye hoja

Nimeshangazwa sana na mazingira aliyotekwa kiongozi wa Chadema. Sishangazwi kwa sababu ni kiongozi wa upinzani bali ni mazingira aliyotekwa.

Mimi sikuwepo, lakini najaribu kufikiria tu, iliwezekanaje? Otherwise aliyekuwepo anisahihishe.

Najaribu kuwaza hivi....kuna taharuki ya utekaji imeenea. Polisi wakilaumiwa. Viongozi wa dini wamesema. Kule Busega waliandamana mpaka mtu akauliwa na polisi. Katika hali kama hiyo maana yake wananchi tulitakiwa kulindana sisi kwa sisi. Kwamba hatutakuwa tayari kuruhusu mtu akitwaliwa katika mazingira yasiyoeleweka. Lazimu tuzuie hilo tukio kwa hali na mali hata kama damu itamwagika.

Lakini watu wameingia kwenye bus wakamshusha yule jamaa wakaondoka naye. Sifikirii kama alitulia tu, obvious alikomaa kwanza na kujisanua. Mwisho watekaji wakafanikiwa kumteka mbele ya abiria.

Maana yake kwenye jamii kama hii ambayo serikali haina habari na ulinzi na usalama wa raia wake, unapaswa wewe mwenyewe binafsi kujilinda. Usijekusubiri maraia watapika kelele wakati unatekwa. Wao watasubiri kupiga kelele mitandaoni na Jamiiforums tu. Muda huo umeshachezea kichapo kikali na hata kifo.

Na hiki chama kinachoteka watu kuweni na huruma basi. Kweli unamteka mtu kwa sababu tu kakukosoa?

Watanzania ni waoga wakiona "MJEGEJO" ,fikiria "WAJOMBA" wameingia ndani wameshika "MAGITAA" na "Bangiri" unaweza ukaleta fyoko fyoko? Kwanza tujengewe ujasiri.
 
Watanzania waoga sana wakiona tu land cruiser zimepaki hawasogei hata kuzisogelea .maana wanasema landcuiser zililiovertake Hilo basi na kuli block kama move vile na abiria wote kimyaa.Natamani ningekuwepo hata Mimi kwenye Hilo basi pangechimbika.
 
Rais ameapa kuwalinda Raia ,Kwa katiba hii lakini anapokaa kimya inamaana yeye anahusika kwenye mambo haya
Ukimya wa rais unaleta wasiwasi sana ,kama pale Tegeta Complex mchana kweupe camera kibao lakini mtu anatekwa ,hivi mabus hayana camera? Mbona mwendokasi kuna camera? Nawashauri mabaus yawe na camera kama kuweka vingamuzi inawezekani ,why kusiwe na hidden camera ili kuweza ku-capture hayo matukio?
 
Umeongea pointi. Ila,ni kwa maoni yako.
1. Kwanza ungejiuliza,kwa nini atekwe yeye na si wewe au mwenzako?

2. Vijana wengi,hata wazee bado wanaojiona wana nguvu,hawaamini katika kubadilishiwa mazingira. Kinachotokea ndo hicho,unaanzisha vurugu,huku unasahau kwamba huyo unaetaka kupambana nae,huenda amevurugwa zaidi yako.

3. Hata kama ushahidi upo,wakisema walikufata kwa tuhuma za uharifu,ukawagombeza kutumia siraha,au wale wenzetu waliopitia mafunzo ya kujihami,wakakuondoa uhai. Na visingizio vingine vingi na wataeleweka.

4. Kwa nini,utekwe au ufatwe? Je,wewe umejipangaje katika kufanya unachokifanya. Kuna wakati unajua unamwaga mchuzi wa watu,unatakiwa ujipange na wewe. Sasa unapingana na mtu anaekuzidi,unamtukana au unamtafuta ubaya,unategemea nini? Ununue Mark II uanze kushindana na mwenye V8.

5. Mwisho kabisa,kama unajua kuna lolote umefanya(maana hufatwi hivi hivi bila sababu),kuwa mpole angalau urahisishe mambo. Ukiambiwa upo chini ya ulinzi,na mbinu za kuchomoka huna,tulia.


Kuna mmoja kasema eti kulikuwa na trafiki amekaa siti ya mbele.
Bado huo ni utoto. Anajuaje hakua mtu anayemfatilia mwanzo mwisho? Wangapi wanavaa sale za jeshi au polisi na wana mambo yao?
 
Umeongea pointi. Ila,ni kwa maoni yako.
1. Kwanza ungejiuliza,kwa nini atekwe yeye na si wewe au mwenzako?

2. Vijana wengi,hata wazee bado wanaojiona wana nguvu,hawaamini katika kubadilishiwa mazingira. Kinachotokea ndo hicho,unaanzisha vurugu,huku unasahau kwamba huyo unaetaka kupambana nae,huenda amevurugwa zaidi yako.

3. Hata kama ushahidi upo,wakisema walikufata kwa tuhuma za uharifu,ukawagombeza kutumia siraha,au wale wenzetu waliopitia mafunzo ya kujihami,wakakuondoa uhai. Na visingizio vingine vingi na wataeleweka.

4. Kwa nini,utekwe au ufatwe? Je,wewe umejipangaje katika kufanya unachokifanya. Kuna wakati unajua unamwaga mchuzi wa watu,unatakiwa ujipange na wewe. Sasa unapingana na mtu anaekuzidi,unamtukana au unamtafuta ubaya,unategemea nini? Ununue Mark II uanze kushindana na mwenye V8.

5. Mwisho kabisa,kama unajua kuna lolote umefanya(maana hufatwi hivi hivi bila sababu),kuwa mpole angalau urahisishe mambo. Ukiambiwa upo chini ya ulinzi,na mbinu za kuchomoka huna,tulia.
Kipi bora? Wakuulie hapo hapo nyumbani/kwenye bus au Kutii amri na kwenda kuuliwa porini?
 
Mimi nakumbuka kauli ya kibaki tu,
Mleta mada wewe si mbongo muoga?
 
Kipi bora? Wakuulie hapo hapo nyumbani/kwenye bus au Kutii amri na kwenda kuuliwa porini?
Mkuu,we pambana na hali yako,uzuri utaishia kupiga kelele hapa mtandaoni,ila ungekuwepo usingefanya lolote.

Mi nimekoment kwanza bila kujua kinaongelewa nini,nilijua ni kwa ujumla.

Siku zote ukiambiwa siasa ni mchezo mchafu,elewa.
Majambazi au wezi tu wa kawaida,wakikuvamia na kugundua umewatambua,hukufanyia nini?

Japo ni haki yake,lakini kustaafu jeshi,hakumaanishi upo nje ya uongozi wa jeshi. Hivyo,jeshi lenu kama bado limefunikwa na mwamvuli wa chama,af unahama,jiulize wanakuchukuliaje!
Huko siingii sana,ila hata yeye,si mtoto mdogo kwamba angeshuka hivi hivi,bila kujua kinachoendelea.
Kosa ni la aliejiita Polisi na akamteka au kosa ni la uongozi wa ngazi za juu!
Haya mambo,ni nchi ipi labda unayoijua hainaga mambo hayo?
Unadai ungemtetea na kuzuia kumshusha,kama nani?

Je,unahisi mpaka anasafiri na basi,hana usafiri binafsi? Ungeleta hoja ya lini haya yataisha,chanzo nini,wahusika kina nani(japo unawajua). Kwani yeye wa kwanza? Na wengine subiri watakuja. Ushujaa unatafutwa kihalali,kama kweli una nia njema,toka mitandaoni,simama na simamia ukweli wako,lakini, kuwa tayari kwa lolote.


Majuzi ulisikia skendo ya dereva wa basi alieuwawa mbele ya basi zima,na hakuna aliyejali. Si kila mmoja alikuwa anaokoa mambo yake huko nyuma?
Nani aende kufungwa au kulamba shaba kwa kuingilia mambo yasiyomhusu?
 
Nimeshangaa sana kuashiria kwako kuwa nchi ina Rais wakati ile position ni void
Kuna kitu watu hujiwekea akilini,na uhalisia ni tofauti. Ukifatilia kiundani zaidi,ni nadra sana kukuta rais ana maamuzi kuhusu mambo flani. Labda awe dikteta. Vinginevyo,anaendeshwa.
 
Umeongea pointi. Ila,ni kwa maoni yako.
1. Kwanza ungejiuliza,kwa nini atekwe yeye na si wewe au mwenzako?

2. Vijana wengi,hata wazee bado wanaojiona wana nguvu,hawaamini katika kubadilishiwa mazingira. Kinachotokea ndo hicho,unaanzisha vurugu,huku unasahau kwamba huyo unaetaka kupambana nae,huenda amevurugwa zaidi yako.

3. Hata kama ushahidi upo,wakisema walikufata kwa tuhuma za uharifu,ukawagombeza kutumia siraha,au wale wenzetu waliopitia mafunzo ya kujihami,wakakuondoa uhai. Na visingizio vingine vingi na wataeleweka.

4. Kwa nini,utekwe au ufatwe? Je,wewe umejipangaje katika kufanya unachokifanya. Kuna wakati unajua unamwaga mchuzi wa watu,unatakiwa ujipange na wewe. Sasa unapingana na mtu anaekuzidi,unamtukana au unamtafuta ubaya,unategemea nini? Ununue Mark II uanze kushindana na mwenye V8.

5. Mwisho kabisa,kama unajua kuna lolote umefanya(maana hufatwi hivi hivi bila sababu),kuwa mpole angalau urahisishe mambo. Ukiambiwa upo chini ya ulinzi,na mbinu za kuchomoka huna,tulia.


Kuna mmoja kasema eti kulikuwa na trafiki amekaa siti ya mbele.
Bado huo ni utoto. Anajuaje hakua mtu anayemfatilia mwanzo mwisho? Wangapi wanavaa sale za jeshi au polisi na wana mambo yao?
Hii ni akili kubwa..umegundua kitu
 
Umeongea pointi. Ila,ni kwa maoni yako.
1. Kwanza ungejiuliza,kwa nini atekwe yeye na si wewe au mwenzako?

2. Vijana wengi,hata wazee bado wanaojiona wana nguvu,hawaamini katika kubadilishiwa mazingira. Kinachotokea ndo hicho,unaanzisha vurugu,huku unasahau kwamba huyo unaetaka kupambana nae,huenda amevurugwa zaidi yako.

3. Hata kama ushahidi upo,wakisema walikufata kwa tuhuma za uharifu,ukawagombeza kutumia siraha,au wale wenzetu waliopitia mafunzo ya kujihami,wakakuondoa uhai. Na visingizio vingine vingi na wataeleweka.

4. Kwa nini,utekwe au ufatwe? Je,wewe umejipangaje katika kufanya unachokifanya. Kuna wakati unajua unamwaga mchuzi wa watu,unatakiwa ujipange na wewe. Sasa unapingana na mtu anaekuzidi,unamtukana au unamtafuta ubaya,unategemea nini? Ununue Mark II uanze kushindana na mwenye V8.

5. Mwisho kabisa,kama unajua kuna lolote umefanya(maana hufatwi hivi hivi bila sababu),kuwa mpole angalau urahisishe mambo. Ukiambiwa upo chini ya ulinzi,na mbinu za kuchomoka huna,tulia.


Kuna mmoja kasema eti kulikuwa na trafiki amekaa siti ya mbele.
Bado huo ni utoto. Anajuaje hakua mtu anayemfatilia mwanzo mwisho? Wangapi wanavaa sale za jeshi au polisi na wana mambo yao?
Sijaona ushauri wa maana kwa comment yako!
Hiyo namba 5 ndiyo imenishangaza zaidi. Kwa hiyo, ukijiregeza kama kuku wakati wa kutekwa, ndiyo utasalimika?
 
Mkuu,we pambana na hali yako,uzuri utaishia kupiga kelele hapa mtandaoni,ila ungekuwepo usingefanya lolote.

Mi nimekoment kwanza bila kujua kinaongelewa nini,nilijua ni kwa ujumla.

Siku zote ukiambiwa siasa ni mchezo mchafu,elewa.
Majambazi au wezi tu wa kawaida,wakikuvamia na kugundua umewatambua,hukufanyia nini?

Japo ni haki yake,lakini kustaafu jeshi,hakumaanishi upo nje ya uongozi wa jeshi. Hivyo,jeshi lenu kama bado limefunikwa na mwamvuli wa chama,af unahama,jiulize wanakuchukuliaje!
Huko siingii sana,ila hata yeye,si mtoto mdogo kwamba angeshuka hivi hivi,bila kujua kinachoendelea.
Kosa ni la aliejiita Polisi na akamteka au kosa ni la uongozi wa ngazi za juu!
Haya mambo,ni nchi ipi labda unayoijua hainaga mambo hayo?
Unadai ungemtetea na kuzuia kumshusha,kama nani?

Je,unahisi mpaka anasafiri na basi,hana usafiri binafsi? Ungeleta hoja ya lini haya yataisha,chanzo nini,wahusika kina nani(japo unawajua). Kwani yeye wa kwanza? Na wengine subiri watakuja. Ushujaa unatafutwa kihalali,kama kweli una nia njema,toka mitandaoni,simama na simamia ukweli wako,lakini, kuwa tayari kwa lolote.


Majuzi ulisikia skendo ya dereva wa basi alieuwawa mbele ya basi zima,na hakuna aliyejali. Si kila mmoja alikuwa anaokoa mambo yake huko nyuma?
Nani aende kufungwa au kulamba shaba kwa kuingilia mambo yasiyomhusu?
Kwani humu mtandaoni watu wanapiga kelele au wanabadilishana mawazo? Sheria za nchi zinasema kuna uhuru wa kutoa maoni ila hautakiwi kuvunja sheria na ndiyo tunautumia.

Ningekuwa navunja sheria ningekuwa nishakamatwa ,hapa tunaeleweshana tu ,issue ya kufanya lolote ,hivi unaweza ukaleta purukushani kwa watu zaidi ya watatu mbavu waliokuja na mitutu? Kama wao wanajiamini waje man to man mtu mmoja kwa mmoja na si Mobb huku wakiwa na silaha.
 
Sijaona ushauri wa maana kwa comment yako!
Hiyo namba 5 ndiyo imenishangaza zaidi. Kwa hiyo, ukijiregeza kama kuku wakati wa kutekwa, ndiyo utasalimika?
Sawa,haina noma. Ukijitunisha msuri ndo utasalimika? We tu elewa kwamba juu ya mafia,yupo mafia anaemzidi umafia. Hilo ukilielewa,utajua ufanyeje
 
Ukimya wa rais unaleta wasiwasi sana ,kama pale Tegeta Complex mchana kweupe camera kibao lakini mtu anatekwa ,hivi mabus hayana camera? Mbona mwendokasi kuna camera? Nawashauri mabaus yawe na camera kama kuweka vingamuzi inawezekani ,why kusiwe na hidden camera ili kuweza ku-capture hayo matukio?
Camera zipo Tajiri kutizama kama Bus lilijaza Abiria kweli ama Boss kaibiwa....!
 
Camera zipo Tajiri kutizama kama Bus lilijaza Abiria kweli ama Boss kaibiwa....!

Nawashauri Chadema wakiongozwa na Boni Yai na MMM waendee haraka wakachukue CCTV Footage wazianike online tuwajue waliomuua Ally Kibao.
 
Back
Top Bottom