Wabongo watakulinda mitandaoni lakini sio wakati unatekwa

Wabongo watakulinda mitandaoni lakini sio wakati unatekwa

Kwani humu mtandaoni watu wanapiga kelele au wanabadilishana mawazo? Sheria za nchi zinasema kuna uhuru wa kutoa maoni ila hautakiwi kuvunja sheria na ndiyo tunautumia.

Ningekuwa navunja sheria ningekuwa nishakamatwa ,hapa tunaeleweshana tu ,issue ya kufanya lolote ,hivi unaweza ukaleta purukushani kwa watu zaidi ya watatu mbavu waliokuja na mitutu? Kama wao wanajiamini waje man to man mtu mmoja kwa mmoja na si Mobb huku wakiwa na silaha.
Nimependa ustaarabu wako. Sorry kwa kauli niliyotumia. Ni baada tu ya kuona umekwazika lakini huwezi kuwakabili jamaa watekaji,maana hujui wana nini,ja hata likiwa basi zima kulifyeka hawaoni taabu.
Haya mambo yapo toka enzi,na karibia nchi zote ulimwengu mzima. Kihisia,kiubinadamu,utagundua watu wana roho mbaya,si kila kosa linastahili adhabu ya kifo.
Lakini pia,kumbuka hiyo roho ya kupigania haki za wenzako,unayo wewe. Na kuna wengine,wanaona kuna kikwazo. Hivyo huandaa mazingira ya kuondoa kikwazo. Bahati mbaya hawaji wao,wanatumwa watu. Kwa gharama yoyote. Mtu kawekeza milioni zake kufanikisha uovu wake, mwingine awekeze mdomo! Duniani hakuna haki.
 
Umeongea pointi. Ila,ni kwa maoni yako.
1. Kwanza ungejiuliza,kwa nini atekwe yeye na si wewe au mwenzako?

2. Vijana wengi,hata wazee bado wanaojiona wana nguvu,hawaamini katika kubadilishiwa mazingira. Kinachotokea ndo hicho,unaanzisha vurugu,huku unasahau kwamba huyo unaetaka kupambana nae,huenda amevurugwa zaidi yako.

3. Hata kama ushahidi upo,wakisema walikufata kwa tuhuma za uharifu,ukawagombeza kutumia siraha,au wale wenzetu waliopitia mafunzo ya kujihami,wakakuondoa uhai. Na visingizio vingine vingi na wataeleweka.

4. Kwa nini,utekwe au ufatwe? Je,wewe umejipangaje katika kufanya unachokifanya. Kuna wakati unajua unamwaga mchuzi wa watu,unatakiwa ujipange na wewe. Sasa unapingana na mtu anaekuzidi,unamtukana au unamtafuta ubaya,unategemea nini? Ununue Mark II uanze kushindana na mwenye V8.

5. Mwisho kabisa,kama unajua kuna lolote umefanya(maana hufatwi hivi hivi bila sababu),kuwa mpole angalau urahisishe mambo. Ukiambiwa upo chini ya ulinzi,na mbinu za kuchomoka huna,tulia.


Kuna mmoja kasema eti kulikuwa na trafiki amekaa siti ya mbele.
Bado huo ni utoto. Anajuaje hakua mtu anayemfatilia mwanzo mwisho? Wangapi wanavaa sale za jeshi au polisi na wana mambo yao?
Wewe ndio umeonyesha rangi halisi ya mbongo tunayemsema hapa. Huyo mbongo ndio wewe
 
Mwanaume unaogopa kupigwa risasi moja ufe

lakini upo tayari kukamatwa na kupelekwa usipo pajua nawatu usio wajua na kwa kosa usilo lijua na kuenda kufanyiwa

kitu usichokijua ambacho maumivu yake ni mala lakimoja ya risasi moja ya kichwa huo nao ni ubata
 
View attachment 3090098
Moja kwa moja kwenye hoja

Nimeshangazwa sana na mazingira aliyotekwa kiongozi wa Chadema. Sishangazwi kwa sababu ni kiongozi wa upinzani bali ni mazingira aliyotekwa.

Mimi sikuwepo, lakini najaribu kufikiria tu, iliwezekanaje? Otherwise aliyekuwepo anisahihishe.

Najaribu kuwaza hivi....kuna taharuki ya utekaji imeenea. Polisi wakilaumiwa. Viongozi wa dini wamesema. Kule Busega waliandamana mpaka mtu akauliwa na polisi. Katika hali kama hiyo maana yake wananchi tulitakiwa kulindana sisi kwa sisi. Kwamba hatutakuwa tayari kuruhusu mtu akitwaliwa katika mazingira yasiyoeleweka. Lazimu tuzuie hilo tukio kwa hali na mali hata kama damu itamwagika.

Lakini watu wameingia kwenye bus wakamshusha yule jamaa wakaondoka naye. Sifikirii kama alitulia tu, obvious alikomaa kwanza na kujisanua. Mwisho watekaji wakafanikiwa kumteka mbele ya abiria.

Maana yake kwenye jamii kama hii ambayo serikali haina habari na ulinzi na usalama wa raia wake, unapaswa wewe mwenyewe binafsi kujilinda. Usijekusubiri maraia watapika kelele wakati unatekwa. Wao watasubiri kupiga kelele mitandaoni na Jamiiforums tu. Muda huo umeshachezea kichapo kikali na hata kifo.

Na hiki chama kinachoteka watu kuweni na huruma basi. Kweli unamteka mtu kwa sababu tu kakukosoa?

Watanzania ni waoga. Huoni juzi dereva kauawa abiria wamejificha kwenye gari.
 
Back
Top Bottom