Kumbe?!!! Basi limeisha hilo πππAnanipenda huyo wala usihofu.
Si unaona nilikua nimetulia zangu kanifata mwenyewe?
Na unajua nini?
Ukiona ID yeyote inanitukana kaa nayo mbali,ni ya tapeli.Hapo atanivizia na Id nyingine sehemu nyingine anitukane
Huyu ndo kachekesha zaidiUmeambiwa mafanikio yake ni
1. TV inchi 65
2. Mke mwenye ''mkia'' wa maana na watoto
3. Kununua vitu super market
4. Kausafiri.
Maskini wanazidi kuongeza huko Marekani πππUkihitaji salamu nenda pwani kwa waswahili,kwangu utaambulia chuya ukalishie kuku!
Bado sijafahamu ni kwanini watanzania wengi wanaoishi nchi za Marekani,Canada na Uk huwa wanamaisha magumu kupita kiasi tofauti kabisa na wale wanaoishi nchi za Scandinavian na Germany!.
Ninawafahamu jamaa kadhaa wanaoishi huko tangu zamani na hakuna walichofanya cha maana kwenye familia zao(Wazazi) hapa Tanzania,wengi huwa wanarudishwa kipindi cha matatizo tu lakini huwezi kuwaona wakiwa wanarudi kipindi cha furaha kuwasalimia ndugu zao.
Watanzania wengi wanaoishi nchi za Scandinavian huwa wamerekebisha makazi ya wazazi wao na pia huwa wamejenga nyumba za kifahari ili wanapokuwa wanakuja likizo basi hufikia huko,siyo nyumba tu bali huwa na usafiri mzuri!.
Hii ni tofauti kabisa na wabongo wanaoishi Marekani,Canada na UK,hawa huwa wanarudi makwao endapo Baba au Mama ni mgonjwa au amefariki kabisa,na huwa wakija hata vaa yao inatia mashaka!.
Huwa wanapenda kuvaa miwani mikubwa kama wachomelea welding na kujifanya kuishangaa Tanzania kana kwamba ni chooni!,Unakuta hata hela ya kuwatoa marafiki zake tu Out hawana zaidi ya kujiongelesha blah blah na masifa kibao!.Wengi wamechoka kimuonekano,Sura hazina nuru na mionekano yao imefubaa!.
Ukiwauliza wanabaki kusingizia Marekani Kodi ni kubwa na Ishu za Bills zinabana kila kona,Unabaki kumshangaa kana kwamba huko Marekani ni yeye tu ndiye Bills hupewa kubwa!.
Wabongo wengi wanaoishi Marekani na Canada waliofanikiwa huwa ni kuanzia Umri wa Miaka 50 - na Kuendelea,hawa ndiyo angalau huwa wamejenga makwao na hata hujitahidi kuprovide kwenye familia zao.
Ila hawa wenzangu na mie kuanzia miaka 25 - 45 huwa hawana cha maana zaidi ya blah blah na ngonjera kibao huku kila muda wakipiga simu na kusimanga serikali na kuwakashifu ndugu kana kwamba wanaishi kwenye vyoo!.
Wengine tunawafahamu wamekwenda huko miaka ya 90 lakini hadi leo ni kuzurura tu hawana paper!.
Any way:
Ukitaka kuona walivyo na hasira,wewe soma comments!
Issue ni kupata kazi za kitaaluma ni rahisi zaidi Europe. Na ukiwa na taaluma na ukijua lugha, kufeli huku ni uzembe wako.Nchi za Scandianvia unabebwa sana na serikali ukiwa hujiwezi kiuchumi tofauti na USA. Lakn hakuna maendeleo yoyote ya maana utayapata zaidi ya kula kulala. Hizi nchi gharama za maisha zipo juu mno kuanzia kodi ya nyumba, kodi ya makato kwenye mshahara, nguo, vyakula, usafiri, starehe. Kila kitu ni super expensive. Kama unalipwa mshahara wote utaishia kwenye kulipia bills
Kwa hali ilivyo sasa kutoboa Marekani ni vigumu sana. Haki za mfanyakazi ni ndogo na pia mfumo wa bima ya afya ni mbovu. Ujerumani ni nchi nzuri sana lakini mpaka uje ujiseti inabidi upate cheti cha huku huku na ujue lugha. Huku malipo yako poa na mfanyakazi unalindwa sana.
Kwa kumalizia mimi naona ukishafanya kazi kwa miaka mitano ukawa na experience ya kutosha kwenye field yako Bora urudi Bongo. Maana kama una mtaji unaweza hata ukaanzisha biashara yako.
Hio ilikuwa zamani ni sawa sawa useme kuwa ni rahisi kutoboa Afrika ya kusini kuliko Botswana kwa mwaka huu wa 2023. Kama haujatembea hauwezi kujua.Bora ukae kimya tu. jiulize swali moja tu, kwanini marekani kuna wageni wengi, kwanini Marekani ni ndoto ya wengi, kwanini balozi zinajaa watu kuomba visa. hilo tu linatosha
Hio ilikuwa zamani ni sawa sawa useme kuwa ni rahisi kutoboa Afrika ya kusini kuliko Botswana kwa mwaka huu wa 2023. Kama haujatembea hauwezi kujua.
Mimi nipo ujerumani kama hauna taaluma Marekani pako poa lakini kama una taaluma Ujerumani papo poa sana. Changamoto kubwa ni lUGha lakini ukishaijua mambo yapo poa. Kwa mtu aliyepo marekani anajua kuwa marekani haifikii europe kwa maslahi ya kazi za kitaaluma. I doubt that you are currently in US, labda kama ulikuwa unaishi huko zamani.Mimi naishi Marekani ni marafiki canada Australia na baadhi ya nchi za Euro, kwaiyo tuna share taarifa.
Marekani ni sehemu sahihi kwa mtafutaji
Mimi nipo ujerumani kama hauna taaluma Marekani pako poa lakini kama una taaluma Ujerumani papo poa sana. Changamoto kubwa ni lUGha lakini ukishaijua mambo yapo poa. Kwa mtu aliyepo marekani anajua kuwa marekani haifikii europe kwa maslahi ya kazi za kitaaluma. I doubt that you are currently in US, labda kama ulikuwa unaishi huko zamani.
kama unabeba box Marekani utapata hela kuliko Ujerumani lakini kama una taaluma ujerumani pako poa sana. Inaonekana haupo Marekani na unafuatilia sana data za internet. USA is over rated na mtu mwenye first hand experience knows that. Wewe leta ushahidi upo Marekani na mimi nitaleta wangu kuwa nipo Ujerumani.Kuongea kwa maneno hatuwezi kukuelewa
Sema hivi, kupitia chanzo fulani, Ujerumani ndio nchi nzuri kwa wafanyakazi wenye taalum. alafu fanya na kutupia na kapicha basi.
Inaeleweka kwamba Marekani ndio nchi ya kwanza kimalipo kwa wafanyakazi, ujerumani hata kwenye top 5 countries huwa haipo.
kama unabeba box Marekani utapata hela kuliko Ujerumani lakini kama una taaluma ujerumani pako poa sana. Inaonekana haupo Marekani na unafuatilia sana data za internet. USA is over rated na mtu mwenye first hand experience knows that. Wewe leta ushahidi upo Marekani na mimi nitaleta wangu kuwa nipo Ujerumani.