Wabongo wengi wanaoishi Marekani wana maisha magumu tofauti na wale wanaoishi nchi za Scandinavian

Wabongo wengi wanaoishi Marekani wana maisha magumu tofauti na wale wanaoishi nchi za Scandinavian

Wajanja ni wale wasiochagua kazi, nasikia kazi za ndani zinalipa, kuzibua vyoo, na kupalilia bustani. Wakija bongo hawasemi kazi zao.
ndo maana West Africa wanatuzidi kwa mengi. Wengi wao wana taaluma zinazoeleweka. Sisi Watanzaia wengi tia maji tia maji
 
Kama yule mkaka wa mbey...analazimisha usabusraibu YouTube yake akusanye one click. Amechakaa sana mjamaa.
 
Kuna ukweli kiasi fulani. Wengi wa Wanaoishi Marekani hata kama wana hela kuna style fulani ya maisha inakuwa sio sawa. Uvaaji na mwonekano unakuwa kama wa kihuni huni. Lakini kama walivyotangulia kusema wanaJF wengine ni kuwa hakuna sehemu rahisi duniani kwenye kutafuta hela. Kuna watu wako Kolwezi, Kasumbalesa, Sumbawanga na sehemu zingine za chaka wana hela kuliko hata hao wa Germany.
Pia wabongo wakifika USA wanaaacha ga utamaduni wa kibongo na kufuata wa wenyeji. Yani hakuna kushikana mkono Wala nini, Kila mtu afe kivyake.

Pia usitegemee eti umefika USA unajitafuta ukashukia Kwa ndugu udhani atakuvumilia kama ilivyo Tz. Ni big no. Hapo utapaswa nunua msosi wako na baada ya siku kadhaa bills zitakuhusu pia na huku huna kitu.

Hapo anakutafutia sababu ya kukutimua ukawe homeless. Wapo wabongo kibao homeless USA.
 
Iwapo tutafanya utafiti asilimia kubwa sana ya watu Duniani,
si Tanzania pekee Duniani kote, ndio ni Dunia yote kabisa wangependa kuishi/kwenda America na kwa sababu za msingi kabisa na zinazoweza kukubalika kwa yyote anaejielewa.

Lakini shida ni kuwa; America si ya kila mtu (Te hee 😀 )

Kuna ambae yupo nyumbani Bongo ama kwingineko,
Hana chochote, hana taarifa sahihi na za kweli, na hana uwezo wa kuweza kwenda America,
Mbung'o huyu ni Bendera fuata upepo lakini ataponda nae kwa kusikiatu pasi na kutafiti.

Lakini kuna ambae yupo nje ya Bongo kanasa sehemu (Ng'ambo ya mauchochoroni) anatamani sana sana angeweza kwenda America lakini nae hawezi yaani kafika na kurudi Bongo hawezi(mazingira yanambana) inaweza kuwa Kisheria au tena Kiuchumi. Afanyeje? Ataponda.

Vilevile kuna mwenzangu na mie ambae 'kaharibu' aidha 'kadunda' mara kadhaa alipoomba Visa ya America,
au tena alikuwepo huko America lakini akafurushwa kwa kukosa uhalali wa kuwepo huko yaani America haimtaki.
Huyu nae atajaribu kusema kaiona America na haipendi America kwa Riwaya na Makala juu,
Ilimradi tu aponde.

Narudia tena Dunia yote inaiota America, America, America.
Lakini America SIO ya kila mtu.

Hata hivyo, kama inavyoweza kuwa sehemu yoyote ile nyingine Duniani,
Hakuna mahali panapokosekana changamoto za hapa na pale lakini kwa ushahidi na taarifa za uhakika hivi tunavyoongea hakuna wa kuifikia America kwa uhakika ya kupiga hatua za kustaajabisha kimaendeleo kwa Wahamiaji.

Swala la msingi zaidi;
Una nini mkononi (unapeleka nini America) na umejiandaaje kuelekea huko kwa maana ya u-me-ji-pa-nga-je?
Sio kukurupuka.
Kingine huko kazikazi, watoto wa mama wakishindwa watatafuta visingizio.

Unataka ndio hivyo, hutaki ndio hivyo.

Chukua hiyo na tafakari.
 
Pia wabongo wakifika USA wanaaacha ga utamaduni wa kibongo na kufuata wa wenyeji. Yani hakuna kushikana mkono Wala nini, Kila mtu afe kivyake.

Pia usitegemee eti umefika USA unajitafuta ukashukia Kwa ndugu udhani atakuvumilia kama ilivyo Tz. Ni big no. Hapo utapaswa nunua msosi wako na baada ya siku kadhaa bills zitakuhusu pia na huku huna kitu.

Hapo anakutafutia sababu ya kukutimua ukawe homeless. Wapo wabongo kibao homeless USA.
Hapo nilipokoleza;
Naomba nirekebishwe iwapo nakengeuka ila, ni nadra sana mtu/Mhamiaji kuwa Homeless.
Wahamiaji wengi wanakuwa wanafafanya Kazi ambazo zinawafanya waweza kuwalipia 'Paa kichwani'.
Hata hao Homeless (Waamerica) mara nyingi ni Waraibu wa madawa au Wahalifu waliopitiliza ambao hawaajiriki na ambao wanachagua Kaziza kufanya.
Kingine tuache uzwazwa unapozungumzia wasio na makazi kwani Tanzania hakuna wasio na makazi?
Rubbish.

Msimezeshwe ujinga hizi taarifa mbona hazihitaji kuhadithiwa zipo mitandaoni tele.

Mtanzania a
 
Back
Top Bottom