Wabunge 19 Viti Maalum CHADEMA wafungua kesi. Bunge lasema linasubiri uamuzi wa Mahakama Kuu

Wabunge 19 Viti Maalum CHADEMA wafungua kesi. Bunge lasema linasubiri uamuzi wa Mahakama Kuu

Leo spika wa Bunge ameelezea sakata la wabunge 19 wa viti maalum CHADEMA waliofukuzwa na chama chao. Kwa ufupi, wabunge husika wamefungua kesi mahakamani kupinga maamuzi ya baraza kuu la CHADEMA na Bunge limesema halitaweza kutangaza viti hivyo kuwa wazi kuuheshimu muhimili mwenzake wa mahakama.

=====

Spika amesema taarifa walianza kuiona kwenye mitandao ya kijamii usiku wa tarehe 11 Mei kwamba baraza kuu la CHADEMA limeazimia kukubaliana na uamuzi wa kamati kuu ya CHADEMA kuwafukuza uanachama wabunge 19 kupitia chama hicho.

Tarehe 12 Mei kwa njia ya barua pepe, wabunge hao 19 walimfahamisha spika maamuzi yaliyofikiwa na baraza kuu kwamba si halali, yako kinyume na katiba ya Tanzania na hayakuzingatia haki ya msingi ya kuwasikiliza au kuwaruhusu kujitetea.

Wabunge hao 19 wa CHADEMA wamepeleka kesi mahakama kuu ya Tanzania kupinga uamuzi huo na mwenendo mzima wa maamuzi yaliyofanyika kupitia shauri namba 16 la mwaka 2022 dhidi ya baraza la wadhamini CHADEMA, tume ya Taifa ya uchaguzi na mwanasheia mkuu wa Serikali.

Pia Spika Tulia amesema Mei 12 saa 9:30 alasiri afisa wa CHADEMA alifika bungeni aliyejitambulisha kwa jina la Meshack alifika ofisi ya spika Dar kukabidhi barua kwa spika na aliambiwa asubiri kwani wakati wa Bunge maafisa wote wanakuwa Dodoma, akaondoka baada ya kufanya mawasiliano na viongozi wake.

Tarehe hiyo hiyo Bunge lilipokea barua pepe iliyosainiwa na katibu mkuu wa CHADEMA juu ya maamuzi ya kikao cha baraza kuu juu ya kukataliwa rufaa ya wanachama 19 wa Chadema.

Spika amesema tarehe 13 Mei, barua hiyo iliwasilishwa ofisini kwa Spika kwa mkono na naibu katibu mkuu wa CHADEMA, Singo Kigaila na baadae ikapokea barua hiyohiyo kwa DHL.

Spika amesema Mamlaka ya mwisho ya utoaji haki ni Mahakama katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hivyo katika nchi yenye kuongozwa na sheria na kuheshimiana kati ya mhimili mmoja na mwingine, Bunge haliwezi kuingilia mchakato wa Mahakama hivyo inalazimika kusubiri mpaka mahakama itapotoa uamuzi wake kuhusu jambo hilo.

Spika amesema wabunge husika walimtaarifu mapema kabla hajapokea taarifa yoyote rasmi kutoka CHADEMA, hivyo analazimika kutotangaza nafasi za viti maalum 19 za CHADEMA ziko wazi hadi hapo mahakama itakapokamilisha kazi yake ya kutoa uamuzi.

Spika amesema endapo kutakuwa na maswali, msemaji wa jambo husika ni Spika.

Wabunge wamegonga meza kwa wingi kupongeza maamuzi yaliyosomwa na Spika.

Pia, Soma;

=> Kamati Kuu ya CHADEMA yawavua nyadhifa na uanachama Halima Mdee na wenzake 18 walioapishwa kuwa Wabunge wa Viti Maalum

=> Baraza Kuu la CHADEMA laridhia kufukuzwa kwa Halima Mdee na wenzake 18. Asilimia 97.6 waafikiana na maamuzi

=> Wabunge 19 kufungua kesi, vigogo CCM na ofisi ya Spika wahusishwa katika uratibu!
View attachment 2226708
Toka alipooletwa ki mchongo kuwa naibu Spika nilijua mavi matupu
 
Kwa nini usiwe mvumilivu kuvua mbivu na mbichi? Unadhani CC na Baraza kuu ni kikao cha watakatifu wasiokosea? Sasa ni muda wa Dalali DJ kuaibika
 
Leo spika wa Bunge ameelezea sakata la wabunge 19 wa viti maalum CHADEMA waliofukuzwa na chama chao. Kwa ufupi, wabunge husika wamefungua kesi mahakamani kupinga maamuzi ya baraza kuu la CHADEMA na Bunge limesema halitaweza kutangaza viti hivyo kuwa wazi kuuheshimu muhimili mwenzake wa mahakama.

=====

Spika amesema taarifa walianza kuiona kwenye mitandao ya kijamii usiku wa tarehe 11 Mei kwamba baraza kuu la CHADEMA limeazimia kukubaliana na uamuzi wa kamati kuu ya CHADEMA kuwafukuza uanachama wabunge 19 kupitia chama hicho.

Tarehe 12 Mei kwa njia ya barua pepe, wabunge hao 19 walimfahamisha spika maamuzi yaliyofikiwa na baraza kuu kwamba si halali, yako kinyume na katiba ya Tanzania na hayakuzingatia haki ya msingi ya kuwasikiliza au kuwaruhusu kujitetea.

Wabunge hao 19 wa CHADEMA wamepeleka kesi mahakama kuu ya Tanzania kupinga uamuzi huo na mwenendo mzima wa maamuzi yaliyofanyika kupitia shauri namba 16 la mwaka 2022 dhidi ya baraza la wadhamini CHADEMA, tume ya Taifa ya uchaguzi na mwanasheia mkuu wa Serikali.

Pia Spika Tulia amesema Mei 12 saa 9:30 alasiri afisa wa CHADEMA alifika bungeni aliyejitambulisha kwa jina la Meshack alifika ofisi ya spika Dar kukabidhi barua kwa spika na aliambiwa asubiri kwani wakati wa Bunge maafisa wote wanakuwa Dodoma, akaondoka baada ya kufanya mawasiliano na viongozi wake.

Tarehe hiyo hiyo Bunge lilipokea barua pepe iliyosainiwa na katibu mkuu wa CHADEMA juu ya maamuzi ya kikao cha baraza kuu juu ya kukataliwa rufaa ya wanachama 19 wa Chadema.

Spika amesema tarehe 13 Mei, barua hiyo iliwasilishwa ofisini kwa Spika kwa mkono na naibu katibu mkuu wa CHADEMA, Singo Kigaila na baadae ikapokea barua hiyohiyo kwa DHL.

Spika amesema Mamlaka ya mwisho ya utoaji haki ni Mahakama katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hivyo katika nchi yenye kuongozwa na sheria na kuheshimiana kati ya mhimili mmoja na mwingine, Bunge haliwezi kuingilia mchakato wa Mahakama hivyo inalazimika kusubiri mpaka mahakama itapotoa uamuzi wake kuhusu jambo hilo.

Spika amesema wabunge husika walimtaarifu mapema kabla hajapokea taarifa yoyote rasmi kutoka CHADEMA, hivyo analazimika kutotangaza nafasi za viti maalum 19 za CHADEMA ziko wazi hadi hapo mahakama itakapokamilisha kazi yake ya kutoa uamuzi.

Spika amesema endapo kutakuwa na maswali, msemaji wa jambo husika ni Spika.

Wabunge wamegonga meza kwa wingi kupongeza maamuzi yaliyosomwa na Spika.

Pia, Soma;

=> Kamati Kuu ya CHADEMA yawavua nyadhifa na uanachama Halima Mdee na wenzake 18 walioapishwa kuwa Wabunge wa Viti Maalum

=> Baraza Kuu la CHADEMA laridhia kufukuzwa kwa Halima Mdee na wenzake 18. Asilimia 97.6 waafikiana na maamuzi

=> Wabunge 19 kufungua kesi, vigogo CCM na ofisi ya Spika wahusishwa katika uratibu!
View attachment 2226708
Mahakama chini ya maelekezo ya CCM.
 
Spika ametoa taarifa Bungeni kwamba, Bunge halina mamlaka ya kusitisha uwakilishi wa wabunge 19 waliofukuzwa Chadema akieleza kwamba chombo pekee chenye mamlaka ya kufanya maamuzi ya mwisho kisheria ni Mahakama.

Hivyo watasalia Bungenimpaka hapo Mahakama itakapotoa hukumu.
Sarakasi za Uviko 19. Spika yupo sahihi, Bunge haliwezi kuingilia mhimili mwingine wa Mahakama. Ni jambo la kusubiria maamuzi ya Mahakama.

Mapovu Yaendelee...!
Thanks GOD- Precedent sent... kwa sasa na kwa siku zijazo....
 
Tanzania ina wasomi wa hovyo sana, kuna Mtu anajiita P atakuja na kukwambia mambo ya voices from within, tokea lini nchi ikaendeshwa na voices from within? au utasikia kila kitu kihahusisha KARMA- KARMA ni katiba ya nchi au chama? Alafu anajinasibu ni mawili nguli wa sheria- ni aibu kwa wasomi wa Tanzania.
 
Leo spika wa Bunge ameelezea sakata la wabunge 19 wa viti maalum CHADEMA waliofukuzwa na chama chao. Kwa ufupi, wabunge husika wamefungua kesi mahakamani kupinga maamuzi ya baraza kuu la CHADEMA na Bunge limesema halitaweza kutangaza viti hivyo kuwa wazi kuuheshimu muhimili mwenzake wa mahakama...
Mahakama zetu zinajidhalilisha sana ndo maana haziaminiki rushwa mbele.
 
Leo spika wa Bunge ameelezea sakata la wabunge 19 wa viti maalum CHADEMA waliofukuzwa na chama chao. Kwa ufupi, wabunge husika wamefungua kesi mahakamani kupinga maamuzi ya baraza kuu la CHADEMA na Bunge limesema halitaweza kutangaza viti hivyo kuwa wazi kuuheshimu muhimili mwenzake wa mahakama...
OK. Conjurers at work. Let's wait to see.
 
Maigizo hayataisha Tanzania CHADEMA wakomae wao Kama wao ova.
watakomaa nao vipi hapo mpaka kesi ya msingi itolewe maamuzi hivyo wataendelea kuwemo sana mpaka bunge la bajeti litakapohitimishwa.
 
Hili ndio swali ambalo mimi najiuliza kwani nilitarajia Mdee na wenzake waende Mahakamani kuomba zuio la utekelezaji wa maamuzi ya Baraza Kuu la CHADEMA.

Pia, nilitarajia Spika atumie zuio la Mahakama lilowasilishwa kwake na Wabunge hao kama kigezo cha kuwaruhusu waendelee kubaki Bungeni.

Je, wanasheria mnasemaje?
Na mimi najua hivyohivyo..

Kwamba covid19 wamechelewa kwenda mahakamani.. walipaswa waende wakazuie baraza kuu lisijadili uanachama wao na sio sasa hivi wameshatimuliwa..

Lakini nimesikia mahala (za chini ya kapeti) kwamba hata hii kesi mpaka tunaingia siku ya leo ilikuwa haijafunguliwa labda iwe imefunguliwa sasa hivi.
 
Chadema wawaache tu 2025 wanamwagwa
Nadhani issue hii sio suala la 2025 au kesho ni muhimu nchi kuwa na sheria na sheria zisichague wakumuadhibu na yupi wakuachiwa, haki ni muhimu sana tu. Hawa wabunge wana haki kwenda mahakamani kama sheria zinaruhusu lakini swali kukiwa na swala mahakamani hata wakiwa mtumishi wa umma kashitakiwa na akaenda mahakamani je anaruhisiwa kuendelea kufanya kazi au inabidi aachie mpaka hukumu ikitoka? hapa ndio tunatakiwa kuwekwa sawa.

Kwa bunge au CCM wanamaslahi gani na hawa watu 19 kuna fadhila gani zinalipwa. Jambo baya ka kusikitisha ni kuona watunga sheria ndio wanapiga makofi mengi wakijuwa wazi sheria zinapindishwa.

Hii ni sad day katika sheria za nchi hii na zinapoteza credibility ya bunge na nchi. Je kesho mahakama ikisema wamevuliwa uanachama watarudisha malipo yote waliyolipwa wakiwa wabunge?

Kawaida inakuwa wanasimamishwa wakishinda kesi wanalipwa stahiki zao zote. Mimi sina imani na Chadema lakini nakuwa nasikitika nikiona tunakuwa na double standard ikija suala la haki.
 
Safi sana hatimaye tunarudi tena Mahakamani...hahahhahahaha Mahera na Ndugai kama nawaona wanavyokuja kutoa ushahidi namuoana pia askari magereza aliyemtoa yule mmoja ambaye alienda kuapa akitoke huko. Hapa ndio aibu uenda ikaipata CHADEMA ama serikali na Bunge kwa ujumla.
🤔🤔🤔
 
Kuna mambo ukiwa na akili timamu unaona kabisa yanaweza kufanyika kwenye zile nchi za kijinga tu.kamwe huwezi kuyaona kwenye nchi zenye watu smart wanaojielewa.

Nasikitika kusema nchi nyingi za kundi la kwanza zinapatikana Afrika na hii ikiwa mojawapo.Nchi ambayo mwenye elimu na asiye na elimu wote wanakiwango sawa cha kufikiria.nchi ambayo mwenye madaraka na asiye na madaraka wana kiwango sawa cha maamuzi.Inasikitisha sana.
 
Naendelea kusimamia msimamo wangu wa kutoshangilia kiongozi yeyote anayeingia madarakani haraka haraka wakati sijui muelekeo wake.

Haya wale wa anaupiga mwingi mnasemaje hapa?.

Spika mliyekuwa mnashangilia baada ya Ndugai kupalazwa nje ya box mpo?.

Yaani hii nchi ni kutulia kama umewekwa kwenye jokofu each day!.
 
Mbona siku nyingi tu walishatoka chadema hao.
Nilishauri tangu mwanzo chadema waachane na hao akina mdee wasihangaike nao waendelee na maisha yao.
Lakini hapa shida ni UBUNGE.
CHADEMA inaweza kufungua kesi dhidi ya wabunge 19 waliowafukuza kwenye chama chao kwamba hawawatambui, wasijitambulishe, wasitambuliwe na wasiitwe wanachama au wabunge wa CHADEMA.

Hiyo ndio kesi pekee CHADEMA wanayoweza kufungua mahakamani uamuzi ukatolewa ndani ya muda mfupi na kuna uwezekano mkubwa wa kushinda. Kesi nyingine yoyote inayohusu kutaka wabunge hao waondolewe bungeni itamalizika 2025.
 
Back
Top Bottom