Tetesi: Wabunge 19 wa CHADEMA washauriwa kujiuzulu kupisha mchakato halali ndani ya chama wa kupata wabunge halali, walioomba msamaha Watafikiriwa

Tetesi: Wabunge 19 wa CHADEMA washauriwa kujiuzulu kupisha mchakato halali ndani ya chama wa kupata wabunge halali, walioomba msamaha Watafikiriwa

Huwezi kuijua nguvu ya chadema au unaijua lakini unaikana. Halafu hatugombani na wanawake, Bali tunataka mchakato wa chama ufuatwe na sio mtu anjiamulia kwenda bungeni wakati chama hakijamteua.

Halafu shehe mkuu alitumika kwa busara ili wewe uje useme ulichosema. Lakini Mbowe kutoka kulianzia pale Mbowe alipolalamika wenzake hawapati chakula, na baadae upande wa mashtaka kuondoa mashahidi waliobakia Kama tisa na kufunga ushahidi wake, Rais kuonana na Tundu Lissu, na nguvu za wanachadema na wananchi kwa ujumla. Pia kesi yenyewe haikuwa na nguvu ushaidi ulikuwa wakujikanyaga tu.

But sio Kwa nguvu ya chadema sio kweli na ukweli unaujua.

Ni watu wameenda kuomba busara kutumika so sio nyie

Nyinyi kama chama mlishashindwa na ndio maana this time lisu ajaongea utopolo wake
 
Nadhani umekosea, ccm ndio wanacheza ngoma ya CHADEMA. Maana baada ya pressure ya kumtoa Mh Mbowe, Serikali ndio imemtoa. Sasa Kuna pressure ya Covid 19 waondoke.

Halafu, Vyama vipo vingi vya upinzani. Sio chadema tuu. Hata chadema kilikuwa chama kidogo in 1995, but vissionary leaders na hard work Leo kimekuwa chama kiku Cha upinzani. Wakati CHADEMA wanapitia madhira kipindi Cha Magufuri mlikuwa mnawacheka na kuwatenga hakuna aliyetaka kujihusisha nao kwa hofu ya kukamatwa.
Chadema hakijawahi kuwa chama chama kikuu cha upinzani hilo ni jina mumejipachika wenyewe, mulisema muna wanachama milioni 8 lakini wakati Mbowe anakamatwa kwa kesi za kubambika hakutoka hata mwanachama 1 kuonyesha wingi wenu, chadema imeshindwa na wanachama wa upinzani laki 3 kule zanzibar.

Tundu lissu baada ya uchaguzi aliitisha maandamano nchi nzima hakuna aliyetoka hata yeye mwenyewe na badala yake akakimbilia germany embassy kw sms aliyotumiwa na mtu asiyemjua eti

Mulisema serikali hamuitambui iliyo madarakani na wakati maalim seif anamfata magufuli ikulu kuzungumza maslahi ya nchi na zanzibar mulimuita msaliti lakini angalia lissu alivyomdoelea rais belgium lakini mbowe anaachiwa kabla kufika kwake ameenda Ikulu, na hatujasikia kiongozi wowote wa chadema akilaani ni wazi chama chenu kimeuzwa bei chee kabisa

Ndio mana ACT wazalendo wana take advantage baada ya failed chadema, na ubovu wa fikira na mbinu za waliokuwa wakijiita viongozi wa chadema.

Saivi tegemea mbowe na lissu kuitwa Ikulu mara kwa mara na kuzibwa midomo midomo, category ya chadema sasaivi ni ya kina TLP na NCCR mageuzi ya Mbatia kumpongeza rais kila mara kujivika upinzani kumbe mnatumiliwa kuuwa upinzani nchini, kwisha chadema
 
Kuna taarifa kwamba wabunge 19 wa viti maalumu wa Chadema wameshauriwa na mamlaka husika wajiuzulu ili kulinda hadhi zao badala ya kusubiri chama chao kithibitishe kuwafukuza.

Inasemekana wabunge 6 walikata rufaa na wengine kadhaa akiwemo Mrs Kafulila waliomba msamaha baada ya kujikuta tu wako bungeni.

Chadema wanategemea kufanya kikao cha kamati kuu na Baraza kuu hivi karibuni ambapo pia majina ya wabunge wapya 19 wa viti maalumu yatatangazwa.

Kwaresma njema!
Kuna siku Tanzania itarudi mikononi mwa wenyewe.
 
Shekhe mkuu ndio kafanya mbowe atoke wala sio chadema, ni huruma Tu Kwa utawala

That's why mbowe alisema anamshukuru mama Kwa kuwa concern

Nyie hamna nguvu now, endeleeni kugombana na wanawake 19 basi

Halafu kamsikilize Mbowe alichosema leo kanisani Azania Front kuwa nguvu ya umma ndio imemtoa sio mtu mmoja. Wewe bakia na assumptions zako. Shehe Ni sehemu ya nguvu ya umma.
 
But sio Kwa nguvu ya chadema sio kweli na ukweli unaujua.

Ni watu wameenda kuomba busara kutumika so sio nyie

Nyinyi kama chama mlishashindwa na ndio maana this time lisu ajaongea utopolo wake

Mbona unakataa sio CHADEMA?. Mimi najua nguvu ya chadema na umma wa Tanzania ndio imemtoa Mh Mbowe.
 
Mbona unakataa sio CHADEMA?. Mimi najua nguvu ya chadema na umma wa Tanzania ndio imemtoa Mh Mbowe.

Miezi nane yote ilikuwa wapi? Hao wengine wamefungwa huko singida mbona hawatoki?.

Hamna nguvu yoyote ya umma Kwa sasa
 
Halafu kamsikilize Mbowe alichosema leo kanisani Azania Front kuwa nguvu ya umma ndio imemtoa sio mtu mmoja. Wewe bakia na assumptions zako. Shehe Ni sehemu ya nguvu ya umma.

Nguvu ya umma Kwa nguvu gani?

Si mlienda EU walifanya nn? Si mpaka Bunge la EU limeongea Je serikali ilimtoa?

Kuweni na shukrani hata kidogo
 
Chadema hakijawahi kuwa chama chama kikuu cha upinzani hilo ni jina mumejipachika wenyewe, mulisema muna wanachama milioni 8 lakini wakati Mbowe anakamatwa kwa kesi za kubambika hakutoka hata mwanachama 1 kuonyesha wingi wenu, chadema imeshindwa na wanachama wa upinzani laki 3 kule zanzibar.

Tundu lissu baada ya uchaguzi aliitisha maandamano nchi nzima hakuna aliyetoka hata yeye mwenyewe na badala yake akakimbilia germany embassy kw sms aliyotumiwa na mtu asiyemjua eti

Mulisema serikali hamuitambui iliyo madarakani na wakati maalim seif anamfata magufuli ikulu kuzungumza maslahi ya nchi na zanzibar mulimuita msaliti lakini angalia lissu alivyomdoelea rais belgium lakini mbowe anaachiwa kabla kufika kwake ameenda Ikulu, na hatujasikia kiongozi wowote wa chadema akilaani ni wazi chama chenu kimeuzwa bei chee kabisa

Ndio mana ACT wazalendo wana take advantage baada ya failed chadema, na ubovu wa fikira na mbinu za waliokuwa wakijiita viongozi wa chadema.

Saivi tegemea mbowe na lissu kuitwa Ikulu mara kwa mara na kuzibwa midomo midomo, category ya chadema sasaivi ni ya kina TLP na NCCR mageuzi ya Mbatia kumpongeza rais kila mara kujivika upinzani kumbe mnatumiliwa kuuwa upinzani nchini, kwisha chadema

ACT ipi hiyo? Hii iliyokuwa inalilia Mbowe aombe msamaha aachiwe, refer Zitto na Duni haji. Mpaka kufikia Duni Haji kusema Lissu na wafuasi wa Chadema ndio wanafanya mbowe azidi kusota lupango. Maana wanamshawishi asiombe msamaha. Nashangaa Leo unasema Nini?

CHADEMA haijajipachika kuwa chama kikuu Cha upinzani. Nakuomba Kafuatilie vigezo vya kuwa chama kikuu Cha upinzani . Ambavyo ni kuwa na uwingi wa kura za urais na ubunge. Sasa kuanzia 2010 CHADEMA ndio imekuwa ikipata kura nyingi kwenye ubunge na urais.

ACT ya Sasa Ni masalia ya CUF na CHADEMA, hivyo sioni jipya huko. Kwa CUF kumkimbia Lipumba na CHADEMA kumfuata Zitto aliyetimka. So please you have a long way to go kufikia level ya chadema.

Halafu suala la kuandamana sio CHADEMA Wala Viongozi wake, Ni nature ya raia wa Tanzania. Kama kuandamana wangeandamana kwenye Mambo yanayowagusa moja kwa moja, Kama tozo, kupanda kwa Bei ya vitu, mauaji ya polisi kwa Raia nk. Tofautisha nature ya watu na maandamano.
 
Kuweka kumbukumbu sawa hapa JF kuhusu namna ya kuwapata wabunge wa viti maalum ndani ya CHADEMA unavyopaswa kuwa.

1. Kamati kuu ya CHADEMA kuketi ili kuyapokea matokeo, kuweka vigezo na kutengeneza utaratibu.

2. Katibu mkuu wa CHADEMA kutoa tangazo la umma kwa wanachama wa CHADEMA kuchukua fomu ili kugombea.

3. Wanawake wanaCHADEMA kuchukua fomu za kugombea na kukamilisha taratibu zote ikiwemo taratibu za BAWACHA.

4. Zoezi la kuchukua fomu za kugombea kuhitimishwa, kamati kuu kukaa, kupokea majina, kuchuja na kupendekeza majina ya wanaCHADEMA wenye sifa za kuteuliwa kuwa wabunge wa viti maalum.

5. Katibu mkuu wa CHADEMA kukamilisha taratibu zote za kiofisi kuhakikisha wale tu waliopendekezwa wanakamilisha ujazaji wa fomu za tume ya uchaguzi na ofisi yake kuzirejesha tume ya uchaguzi na kufikishwa bungeni.

NOTE
-Taratibu zote hizo mpaka sasa hakuna iliyofanyika.
-Taratibu zote hizo zinafanyika kwa mfuatano.
-Taratibu yoyote ile hapo inapofanyika umma hujurishwa rasmi na kila mtu atajua.
 
Miezi nane yote ilikuwa wapi? Hao wengine wamefungwa huko singida mbona hawatoki?.

Hamna nguvu yoyote ya umma Kwa sasa

Wewe unajadili muda wa kukaa ndani au achievement?. Hata mpunga unachukua muda kuandaliwa ndipo ukomae kwa kuvunwa. Cha msingi lengo limefikiwa.
 
Nguvu ya umma Kwa nguvu gani?

Si mlienda EU walifanya nn? Si mpaka Bunge la EU limeongea Je serikali ilimtoa?

Kuweni na shukrani hata kidogo

Shukrani yote kwa umma wa Tanzania kusimama pamoja na Mh Mbowe na CHADEMA
 
Wewe unajadili muda wa kukaa ndani au achievement?. Hata mpunga unachukua muda kuandaliwa ndipo ukomae kwa kuvunwa. Cha msingi lengo limefikiwa.

Nyie kazi yenu ni kupiga kelele jf tu
 
ACT ipi hiyo? Hii iliyokuwa inalilia Mbowe aombe msamaha aachiwe, refer Zitto na Duni haji. Mpaka kufikia Duni Haji kusema Lissu na wafuasi wa Chadema ndio wanafanya mbowe azidi kusota lupango. Maana wanamshawishi asiombe msamaha. Nashangaa Leo unasema Nini?

CHADEMA haijajipachika kuwa chama kikuu Cha upinzani. Nakuomba Kafuatilie vigezo vya kuwa chama kikuu Cha upinzani . Ambavyo ni kuwa na uwingi wa kura za urais na ubunge. Sasa kuanzia 2010 CHADEMA ndio imekuwa ikipata kura nyingi kwenye ubunge na urais.

ACT ya Sasa Ni masalia ya CUF na CHADEMA, hivyo sioni jipya huko. Kwa CUF kumkimbia Lipumba na CHADEMA kumfuata Zitto aliyetimka. So please you have a long way to go kufikia level ya chadema.

Halafu suala la kuandamana sio CHADEMA Wala Viongozi wake, Ni nature ya raia wa Tanzania. Kama kuandamana wangeandamana kwenye Mambo yanayowagusa moja kwa moja, Kama tozo, kupanda kwa Bei ya vitu, mauaji ya polisi kwa Raia nk. Tofautisha nature ya watu na maandamano.
ACT haijalilia mbowe aombe msamaha, Zitto kama Zitto baada ya kumtembelea mbowe jela alimshauri mbowe yeye kama Zitto amuombe rais amsamehe ndicho kilichofanyika lakini Tundulisu na aila zao wakaja juu lakini badala yake Huyo huyo tundu lissu ndiye aliyempigia magoti rais kule belgium mbowe asamehewe na ndivyo ilivyotokea mbowe anaachiwa anaenda Ikulu kwa bossi wake aliyemtoa jela na kupewa makaraipio aache siasa za kishamba. Chadema ya kudhalilika kwa kiwango hichi hakuna aliyetegemea.

ACT kama Act bado ni wapya katika macho yako tu lakini Act ya sasa ni taasisi ambayo maalim seif ameijenga tokea 1992 hata kabla ya hiyo chadema kuanza siasa ambao walijufunzia siasa kutoka zanzibar baadae. ni vile hufahamu itikadi za Wazanzibari tu, dakika 3 zilitosha kurudisha hiyo taasisi kupitia Act.

Kuandamana unasema sio itikadi na nature ya watanzania lakini bora useme ni natural ya uwoga kwa watanganyika tu, mara kadhaa Wazanzibari wanakuwa wakiandamana kama utakumbuka january 27 wakati wa Mkapa lakini hata juzi uchaguzi uliopita kina jussa wakapigwa na kuvunjwa miguu na kina mazurui kutekwa ndio mana nilikwambia kabla watu laki 3 zanzibar wamekuwa ni bora zaid kuliko hiyo idadi feki ya wanachama munaosema chadema munao wafikao milioni 8.

Chadema imepoteza muelekeo sasa muna mapandikizi mkapa kwenye uongozi wenu wa juu zaidi., Hatukutegemea mbowe atoke jela afikie Ikulu ni wazi alishindwa mapambano sasa amesarenda kwa bei chee kabisa., na atapelekeshwa kama remote, sioni tofauti ya mbowe, lissu na kina halima mdee na wenzake
 
Mngeionaje wakati mlikuwa mnamshangilia Ndugai aliyeapa na kuamua kuwalinda, kama ilivyokuwa kwa Mwambe aliyejivua uanachama. Ndugai alikataa hata kusikiliza ushauri wa Spika mstaafu Mzee Msekwa.

Umeandika uozo wa tumbaku
 
Please, chama kiwafukuze uanachama halafu Tena kiwateue. Kitateuaje mtu alyefukuzwa uanachama. Hapo walipo sio wanachama wa CHADEMA, watateuliwa na Nani?.

Tujipe muda maana walikata rufaa chamani ila hadi leo rufaa yao haijajibiwa
 
Kuna taarifa kwamba wabunge 19 wa viti maalumu wa Chadema wameshauriwa na mamlaka husika wajiuzulu ili kulinda hadhi zao badala ya kusubiri chama chao kithibitishe kuwafukuza.

Inasemekana wabunge 6 walikata rufaa na wengine kadhaa akiwemo Mrs Kafulila waliomba msamaha baada ya kujikuta tu wako bungeni.

Chadema wanategemea kufanya kikao cha kamati kuu na Baraza kuu hivi karibuni ambapo pia majina ya wabunge wapya 19 wa viti maalumu yatatangazwa.

Kwaresma njema!
Safi sana kama kuna ukweli ndani yake
 
Chondechonde dada zetu hawa wasamehewe wote kazi iendelee,CHADEMA mlishawahi kutukosea mwaka 2015 lakini tulisha wasamehe na bado tuna imani kubwa na nyinyi.
 
Back
Top Bottom