Wabunge CCM kulishana yamini... Lengo ni Mfumo wa Serikali TATU haupiti !!!

Siku zote ukikaa na kuwafikiria sana wabunge na viongozi wa CCM utabaki na mshangao wa kutisha ambao hujawahi kuushuhidia kabla hapa Afrika! Hivi kama serikali 3 ni wazo la watanzania wabunge hao wasiozidi 200 pamoja na viongozi wao wanaweza vipi kula yamini kwa ajili ya watanzania wanaotaka serikali 3 zaidi ya milioni 20?!

Kwa nini wasilishane yamini kuhakikisha kuwa kabla ya 2015 ahadi za JK ziwe zimekamilika kwa asilimia angalau 80 tu?! Yaamini haijawahi kuliwa na watu wanafiki na wazandiki! Zanzibar wanataka nchi yao na wameona serikali 3 ndio njia, watanganyika wenye kuitaka Tanganyika yao wameshaamka na sasa wanataka kuiona Tanganyika yao inarudi, wabunge na viongozi wa CCM hata wakilishana yamini mpaka shingoni hawawezi kuzuia wazo ambalo tayari muda wake muafaka umeshafika!

Wanatakiwa kujua hakuna yamini iliyowahi kuzuia mawazo ya watu ambayo muda wake muafaka ulikuwa umeshafika fika, kama jinsi ambavyo halikuwahi kutokea jeshi kubwa lenye vifaa vya kisasa ulimwenguni lililowahi kuzuia mawazo ya kimapinduizi hasa pale mapinduzi yanapokuwa kuwa ndio chaguo pendwa la mwisho la watu hao.
 
Sikwamba wazanzibari hawaitaki zanziba yao la hasha, ni propoganda za magamba wachache na ukitaka kupata ukweli huu waulize mwanasheria mkuu wa Zanziba, Mwasisi wa Muungano Nasoro Moyo, Maalimu Seif na wengineo, wanaotamani Serikali mbili ni wahafina magamba wachache wapenda ukuu kama akina Nahodha na wenzake
 
Mim CCM naishangaa sana... utafikiri familia ya kambale... Haohao CCM Zanzibar chini ya Baraza la Wawakilishi walifanya mabadiliko kwenye Katiba yao ya Zanzibar huku wakijua kabisa mabadiliko na Ibara walizoziongeza zilikuwa zinahatarisha Muungano... Wasiwe wanafiki,,, Kama wanataka Serikali mbili wafanye mabadiliko kwenye Katiba yao ili ieandane na Katiba ya Jamhuri...

Haiwezekani wanataka Serikali mbili, huku wao wenyewe wameshaisigina na kuinajisi Katiba ya Muungano... Kama walikuwa wanabip kwa Watanganyika sasa ndo wanapigiwa... Wasituchanganye!!! Kama Serikali mbili inafaa mabadiliko makubwa waliyoyafanya kwenye Katiba yao yalikuwa ni ya nini kama si kuudhofisha muungano... Kama wanaona Muungano ni muhimu basi suluhisho ni Serikali Tatu, kama wanaona watanganyika watafaidi basi iwe Serikali moja na kama nako kuna tatizo tukubali Serikali ya Majimbo...
 
Kama hawataki serikali tatu wavunje muungano. Halafu hawa ccm wanaangalia maslahi ya chama chao badala ya taifa.

I.D.I.O.T
 
Cha ajabu hao hao wabunge, mawaziri (hata mkuu wao) wazanzibar wanaoshinikizwa kukataa serikali 3 baaya ya mwaka mmoja tuu watasahau kila kitu na kuja kivingine kabisa ( ki-uamsho uamsho!)
 
Ni rahisi ccm kutumia nguvu kwenye bunge la katiba na kufanikiwa ila ni ngumu kuwashauri watanganyika kukataa serikali yao wakati wa kura ya maoni!!!,nadhani ccm lengo lao isiwepo katiba mpya.

Ushauri wangu kwa ccm,wanaweza kutumia nguvu kubwa kwenye kupitisha katiba hii,ila wajue ikipita bila tanganyika wajiandae na anguko 2015,anguko si lazima kutema urais!!,hata kwenye ubunge itakuwa balaa kama wakiitema serikali ya tanganyika,mwamko wa serikali ya tanganyika ni mkubwa ajabu,kamwe hawawezi kupingana nao ni suala la muda tu,nadhani mtu ukiwa kwenye madaraka uwezo wa kuona na kusikia unapungua!!!yetu macho.
 
Wapi uamsho, daini zanzibar yenu mkishindwa hapa tutawatawala milele,kudadadeki
 
sanduku la kura ndo kila kitu.waboreshe daftari la wapiga kura ili mbivu na mbichi zijulikane.
 
Chama chakavu sawa na ukoo wa panya!
Sisi tunajadili katiba kwa maslahi wa WaTZ wote wao wanaangalia maslahi ya chama na matumbo yao tu!
 
sanduku la kura ndo kila kitu.waboreshe daftari la wapiga kura ili mbivu na mbichi zijulikane.
 
kwa hiyo mchakato wa katba mpy si huru ni wa ccm.mhmm tuendako!
 
JK alisema ikishindwa kupita tutarudi kwenye katiba ya zamani ni sawa lakini pia sie watanzania tutataka kumaliza biashara kwa kuidai Tanganyika yetu iwe kwa mtaani,msituni ama kwenye makaratasi
 
awana hoja hawo wakajipange upya then ndo warudi, tanganyika ileeeeeeeeee!!! tunaisubiri kwa amu kubwa sana
 
kuna yamini ya sauti na ile ya kimoyo moyo huku umeuma meno.
 
Ninyi mna matatizo kweli. Mnafikiri Mungu ni CCM?
 
Hii ni demokrasia au ghasia tu. Watu wanajali chama kuliko nchi. Wananchi wasifanye makosa 2015
 
Serikali mbili zpi? Muungano na ZNZ wapi Tanganyika Au ndio 1+1=2? ilitumika La sivyo tupeane Zamu Next 50years tuwe na Tanganyika na Muungano.
 
Hawa wamezowea migogoro isiyokuwa ya lazima. Tukumbuke hata hatua za kuleta maridhiano walipiga kelele hivi hivi mpaka Raia Karume akawa mkali, leo ndio wapo mbele kutetea maridhiano hayo. Ndani ya CCM wapo wengi wenye busara na wanaunga mkono rasimu hii ya katiba. Tuwadharau tu.
 
Bunge la katiba ni sehemu tu ya mchakato. Hatma yake ni pale wananchi watakaposhiriki katika kura ya maoni ndio mzizi wa fitna utakapokatwa na maslahi ya wengi kuzingatiwa.

Mkuu unasemea wanaNCH gani? au ni hawa wanaolishwa Pilau nakuvishwa Kapelo kisha wanamchagua huyo Mwezeshaji wao? Mnaotegemea kuwa CCM wataleta KATIBA 2nayotamani 2tangoja sana!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…