Kwanza wengi hawakumuelewa Makamba,
Hoja ya makamba alikua akieleza kwamba hata hizi bei za sasa ambazo watu wanalalamika kwamba ni kubwa bado serikali inaweka ruzuku.
Makamba ameeleza kwa makadirio tu kwamba gharama kwa wastani yakuunganisha umeme kama ukiutaka uhalisia inafika 800,000,hivyo hizi gharama za sasa ile ya 27000 kwa vijijini na hii ya mijini ambayo ni laki tatu na point nafikiri serikali inalazimika kuongeza ruzuku.
Makamba ameeleza mita moja ya waya ule unaotumika kuvuta umeme kutoka kwenye nguzo kuja kwenye nyumba inauzwa tsh 35,000/=.Sasa hemu fanya makadirio mfano nyumba yako ipo umbali 16m kutoka kwenye nguzo 35000×16=560000.Hizi ni gharama za waya kwa makadirio.
Na bei ya mita makamba amesema ni 250,000 hivyo ukijumlisha na 560,000 ya waya ndipo hapo alipokadiria gharama ya 800,000/=.
Kimsingi zipo nyumba zinaumbali hata wa 5m kutoka kwenye nguzo hivyo utaona gharama hazitafika 800,000/=.Alichotoa Makamba ni makadirio hakuna sababu yakuhukumiwa.
Chamsingi hapa wanaobisha wanapaswa waende madukani wakaulizie bei ya waya kwa kila useful wa mita moja pia waulize na bei ya mita waone kama makamba anadanganya ndipo mmuite mwongo kinyume cha hapo kaeni kimya.