Mtihani gani mugumu wakati watz wanachapakazi tu! Au wewe umejilockdown? Wabunge waoga hao kama wapigakura wao hawaogopi wanapigakazi wao wajifungia ndani.
Corona sio mvua hadi kusema ikinyesha wote walio nje mnaloa. Yenyewe inautaratibu wake mradi ujampa heshima yake na wewe unajijua umri umeenda, una maradhi mengine yanayo dhoofisha kinga ya mwili na utaki kuchukua tahadhari basi elewa kila siku ya mungu unachezea bahati nasibu maisha yako.
Uongozi ni dhamana ya kujua changamoto za jamii, kiongozi anatakiwa kuwa na ‘soft skills’ uwezi kuona nchi ipo kwenye hali ya hatari halafu una msimamo wa business as usual inaonyesha you are not compassion; wachina wanamsemo ‘jemedari asiyefikiria mauti yanayowasubiri askari wake kabla ya kuamua kuingia vitani hafai kuongoza.
As a leader you got to take ‘rationale decisions’ kutokana na hali mpya iliyojitokeza hata kama ukuitarajia.
Hao watu wanaotoka nje kila siku na wenyewe wanahatarisha maisha ya familia zao ambao wapo majumbani.
Tutumie mfano wa nchi kama UK lockdown yao aikupangwa Boris Johnson alikuwa mbishi kidogo ilikuwa kama Tanzania wanashsuri tu wananchi wao wanawe, wasitoke kama hawana ulazima. Jumatatu waliyopiga ban weekend yake jua lilitoka mijitu ikajazana parks, wengine wakaenda tembelea remotes tourist attraction za vijijini na wenyeji huko wakalalamika sana mijitu ya mjini inataka kuwapelekea maambukizi ndipo serikari yao walipo baini pamoja na somo lote walilokuwa wanatoa kuhusu social distancing lakini kuna mijitu ailewi somo jambo ambalo lilikera serikari kuokoa wengine ikaonekana bora lockdown ianze.
Sio sisi yaani tuna encourage mijitu kukusanyika kwenye masoko, ma bar na maisha yaendelee kama hakuna pandemic, sasa hivi kuna maambukizi ya kutosha ngoja incubation inayoisha baada ya wiki mbili ndio tutajua.
Si mlikuwa mnauliza watu lini hizo taharuki zitaanza muda umefika yaani kuanzia sasa kwenda mbele hili jambo aliwezi kuwa siri tena.