Wabunge wa CHADEMA wakubaliana kutohudhuria tena vikao vya Bunge kutokana na janga la COVID-9, Kujiweka Karantini kwa wiki 2

Wabunge wa CHADEMA wakubaliana kutohudhuria tena vikao vya Bunge kutokana na janga la COVID-9, Kujiweka Karantini kwa wiki 2

Wabunge wa CCM hovyo sana. Yani wanamuona kabisa mwenyekiti wao kala kona wao wamebaki tu kama mazuzu. Yani hawajielewi hata kidogo.
Amejichimbia kwenye mahandaki huko kwao, kama osama alivyokuwa anatafutwa na wamarekani
 
Unataka kusema kuwa wabunge wa CHADEMA wa leo ndio wale wale wa mwaka 2014? Bulaya mtoa taarifa mwaka 2014 alikuwa ni mbunge wa CHADEMA?

Na kati ya CHADEMA na CCM chama gani kilikuwa na wabunge wengi kwenye Bunge la Katiba? Yaani wabunge wachache walisababishaje wabunge wengi washindwe kupitisha Katiba waliyoitaka? Wana CCM waliobaki kwa nini hawakupitisha hiyo Katiba waliyoitaka?
Kaka akidi ilitimia huyo ajui anachoongea
 
Naunga mkono maamuzi haya ya akili ya wabunge wa CDM kutokuendelea na vikao vya bunge. Hii ndiyo maana halisi ya kuongea kwa vitendo. Lakini hii inaonesha kuwa kuwa si lazima kusubiri kila kitu kiamuliwe na viongozi wa CCM ambao hawana maono.
 
Una akili fupi sana. Yaani wewe unawaza uchaguzi wakati huna afya? Mungu akuhurumie tu wewe mkosa maarifa
Kwa akili yako ndefu unafikiri kukimbia bunge wakati waliomba kazi ya ubunge ni sahihi??
 
Acha ubishi basi google kwanza.
Wewe unadai kwamba "huongei na Robot" lakini unataka nitumie Robot (Google) kupata tafsiri ya neno uliloandika nisilolielewa!!

Kuwa na msimamo basi japo kwa jambo hili!!
 
Wakae nyumbani tu, as kodi zetu zinawapa kiburi hicho.

Ila watambue kwamba, wananchi hawajawachagua ili wakakae nyumbani, waliwachagua ili wakawawakilishe bungeni.
Kwani jiwe alichaguliwa ili akakae Chato?
 
Back
Top Bottom