Wabunge walipe kodi, wabunge kutolipa kodi ni rushwa inayotolewa na Serikali

Wabunge walipe kodi, wabunge kutolipa kodi ni rushwa inayotolewa na Serikali

Mshahara wa wabunge ni hela ya kodi, sasa kwa nini walipe kodi? Ni sawa na kumpa hela mwanao na halafu unamwambia akugawie hela ulizompa. Kama unahitaji hela mpe kidogo, nyingine ubaki nazo.
Hata mishahara ya watumishi wa Umma imetokana na hela ya Kodi Ila bado wanakatwa kodi, kwanini isiwe wabunge ?.....acha kutetea ujinga
 
Hii akili sijui wanaitoa wapi,ni ukosa akili kujifanya unaongea kwa uchungu kuhusu bajeti wakati wewe hulipi kodi
Mshahara unaodaiwa wanapata wengi wa Wabunge hawa wala rushwa ni chini ya Tsh. 3,000,000/= kwa mwezi lakini jumla hela wanazosukumiziwa mifukoni kila mwezi ikikaribia Tsh. 20,000,000/= kwa mwezi kutokana na posho na malipo mengine mengi tu.

Tunapoambiwa wanalipa kodi ni makato kwenye mshahara wa hizo milioni tatu lakini katika malipo ya milioni ishirini wanazojaziwa mifukoni kila mwezi hawalipi hata senti tano. Cha ajabu Mama ntilie mwenye kipato kisichofika hata laki moja analipishwa kodi.

Wananchi wapigwa butwaa wakimshangaa Waziri wa fedha kwa mbwembwe kuwahimiza hadi vijana wa miaka 18 kulipa kodi na bunge zima kulipuka kwa shangwe, vigelegele, ugongaji wa meza na ukataji wa mauno juu ya meza wakimpongeza Waziri kwa ubunifu.

Tumelogwa...
 
Hili mbona tulishalitolea ufafanuzi kuwa tayari wanalipa kodi?
Ulipaji kodi wao kwa kweli unatia wasiwasi...
Yaani kwa mfano mtu awekewe mshahara LAKI NANE ndio Unakatwa kodi halafu ana marupu rupu MILIONI TANO ambayo hayakatwi kodi; Nafikiri haihitaji kuwa na degree ili kujua kuwa kuna kitu hakipo sawa
 
Si wao tuu na majaji walipe kodi pamoja na viongozi wakuu yaani Rais wote walipe kodi
 
Ulipaji kodi wao ni changa la macho!
Yaani mtu awekewe mshahara LAKI NANE halafu marupu rupu MILIONI SABA ambayo hayakatwi kodi???
Kwahiyo mnataka hadi posho na marupurupu yakatwe kodi, hili sasa ni jipya.
 
Mshahara unaodaiwa wanapata wengi wa Wabunge hawa wala rushwa ni chini ya Tsh. 3,000,000/= kwa mwezi lakini jumla hela wanazosukumiziwa mifukoni kila mwezi ikikaribia Tsh. 20,000,000/= kwa mwezi kutokana na posho na malipo mengine mengi tu.

Tunapoambiwa wanalipa kodi ni makato kwenye mshahara wa hizo milioni tatu lakini katika malipo ya milioni ishirini wanazojaziwa mifukoni kila mwezi hawalipi hata senti tano. Cha ajabu Mama ntilie mwenye kipato kisichofika hata laki moja analipishwa kodi.

Wananchi wapigwa butwaa wakimshangaa Waziri wa fedha kwa mbwembwe kuwahimiza hadi vijana wa miaka 18 kulipa kodi na bunge zima kulipuka kwa shangwe, vigelegele, ugongaji wa meza na ukataji wa mauno juu ya meza wakimpongeza Waziri kwa ubunifu.

Tumelogwa...
Kulipia ml 3 Kodi Ili mil 17 ipite pembeni Si Kwa bahati mbaya.

Ni walijadiliana wakakubaliana.
 
Tuanzie kwa Rais mshahara wake uwe wazi na kodi tujue analipa kiasi gani sababu so far halipi na mshahara wameuficha.
 

Mbunge Anatokana Na Ccm Halafu Asimame Aseme Budget Mbaya Siku Hiyo Hiyo Ajue Ameingia Matatizoni Mwanzo ~Mwisho

Ndiyo Maana Kusifu Ni Kipaumbele Chao Ingawa Ndugu Zao Tunaumia

Mwafaa!!
 
Kwahiyo mnataka hadi posho na marupurupu yakatwe kodi, hili sasa ni jipya.
ninavyofaham ndio muongozo wa TRA na huwa wanafuatilia sana kwa mshirika binafsi; Ila inawezekana kwenye serikali TRA ina sheria tofauti.
 
CCM wanawaza kula pesa za umma na sivinginevyo
Siku Watanzania watakapozinduka hawataamini watakayoyaona kwa macho yao na kuyasikia kwa masikio yao.

Bila shaka watashangaa na kujiuliza kwa nini waliruhusu hali kama hiyo kutokea mpaka tukafika hapa tulipo.

Watahoji ilikuwaje mpaka rushwa ikatambulika na kukubalika kama kitendo halali katika jamii ya Watanzania?
 
Lipeni kodi ndugu zangu, huo ndio uzalendo wa kweli….. mtakaoyumba kiuchumi tutagawana vya kwangu.
 
Kwahiyo mnataka hadi posho na marupurupu yakatwe kodi, hili sasa ni jipya.
Mbona TRA wakienda kwenye mashirika ya Binafsi (private sector) wanataka malipo yote anayopewa mfanyakazi hata hayo marupurupu yawekwe mshahara ili yatozwe kodi? au kuna sheria za kodi za public sector na zingine za private sector?
 
Hatimaye sura halisi ya Wabunge wetu imefichuka, shukhrani zimwendee Mheshimiwa Musa Azan Zungu Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania!

Kumbe ndiyo maana hawana huruma na sisi wananchi, wao si wawakilishi wetu tena, ni wawakilishi wa serikali ya CCM na sisi tunatumika tu kama ngazi kuwapeleka bungeni.

Wakishafika bungeni hawana habari nasi tena na kila kikao cha bunge ni fursa ya shibe huko chini meza wanakozidi kunenepa kwa mifupa wanayotupiwa kutoka meza kuu.
 
Mshahara wa wabunge ni hela ya kodi, sasa kwa nini walipe kodi? Ni sawa na kumpa hela mwanao na halafu unamwambia akugawie hela ulizompa. Kama unahitaji hela mpe kidogo, nyingine ubaki nazo.
Kazi sana!! Wanacholipwa wafanyakazi wa serikali ni hela zinadondoka toka mbinguni!!

Tanzania wapumbavu ni wengi sana!!
 
Tanzania wapumbavu ni wengi sana!!
Na kumbuka CCM wanadai wana wananchama wengi. Kwa sisi watu wa hesabu idadi ya wanachama wa CCM is directly proportional to idadi ya wajinga, QED!

Ujinga ni mtaji mkubwa sana wa CCM na hapa tunaweza kuona uwezo wa bunge letu lililojaa wana CCM! Masikini Tanzania hili ni jinamizi ambalo tutaliepuka tu tukizinduka!
 
Back
Top Bottom