Wabunge Wetu, Macho ya Watanzania Wote Leo ni Kwenu!. Maslahi ya Taifa Mbele!. Tuwaogope Kama Ukoma Muflis Hawa!, Kama Huwezi, ni Lazima Usaidiwe Tuu!

Ndio maana mkatuita Wanyonge? Hii ni Slogan ya ajabu mnooooo. Ndugu yangu Kaka Paskali, unaaamini kabisa kuwa hatuwezi? Au hatujataka kuweza??
 
Msigwa na wengine kina Musukuma na Tulia, wote ni mawakala wa shetani Samia.
 
Sahihi kabisa..... uwekezaji happy bandarini ndio njia pekee ya kuimarisha ufanisi wa bandari.

Ila hilo bunge la chama kimoja ni kimeo tu....
 
Salaam ndugu Paskali, Asante kwa muhtasari huu, Ubinafsishaji sio dhambi, bali ni kiini na kichocheo cha Uchumi wa taifa, tafsiri ovu ya Ubinafsishaji Kwa Africa ni mikataba ya "kikupe" unyonyaji, Kelele zinazoendelea mitaani sasa ni matokeo ya historia dhidi ya mikataba mibovu Kwa Africa, Je wajua hata Kanali Gaddafi aliwai kukemea na kuonya Africa dhidi ya mikataba ya kitumwa, hata enzi za OAU, Mwaka 1967, Nkrumah alionya Africa dhidi ya mikataba ya kinyonyaji, Bila shaka Wabunge wetu watazingatia maslahi Pana ya nchi dhidi ya mkataba huu na DP World. Shukrani.
 
Nilipo ona umeandika kuruhusu kampuni ya DP World ya Dubai kutuboreshea bandari zetu. Niliamua kuishia kusoma hapohapo kwasababu tayari nilikutazama nawewe kama mamluki. Sababu hii ni kama kuwahadaa waTanzania kwa lugha laini kwenye mambo ya msingi.
 
Sasa Wabunge wanafanya kitu gani?
Ni maigizo kama maigizo mengine yeyote yale ya serikali yako,hakuna madhara yeyote yanayo weza kutokea kutoka kwenye mjadala huu wa bunge sababu kwa mujibu wa mkataba huo utahesabiwa kama ni mgogoro ambao itatakiwa ukatatuliwe Johannesburg , SA, kwa sababu mkataba ulisha sainiwa na ulisha kubalika
 
Nawatakia waheshimiwa wabunge wetu mjadala na majadiliano mema kwa kutanguliza mbele maslahi ya taifa.


Wabunge wenyewe ndio hao akina Msukuma na Kibajaji ambao hata "the" kumtamka hawawezi halafu ndio wajadili MOU iliyoandikwa kiingereza kilichojaa maneno ya mikataba (contract jargons)??!--- hapo hakuna kuremba bali tumepigwa na kitu kizito, the only solution is to topple CCM through ballot box that is the only recourse in our hands.--You can't sell our country to other country in such paltry price.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…