Wabunge wote wa CCM wameshindwa kutetea maslahi ya wamachinga nchi nzima. Nini maana yake?

Wabunge wote wa CCM wameshindwa kutetea maslahi ya wamachinga nchi nzima. Nini maana yake?

Uchaguzi gani umefanyika mpaka hawa kuitwa wapiga kura. Hakujawahi kuwepo uchaguzi bali uvamizi. Machinga wasituchafulie mji bwana waende zao. Machinga mtaji wake huwa laki mbili hawa wa millioni nne mpaka wanajenga mabanda ya 1m pasiporuhusiwa. Ila makala kawaweza. Taasisi isiyowafukuza italambwa juu kwa juu
Wahuni tu wameweka hadi maduka njiani unakuta duka linathamani ya milioni 8-10 anajiita Machinga
 
Hao vibaka waliopatikana kwa mtutu wa bunduki na kura za kwenye mabegi ndiyo unawaita wabunge? Wanajua hata ikifika 2025 mtindo ni uleule hawahitaji kura za kwenye sanduku, bunduki zitawarudisha bungeni
Au wanaona aibu kukutana na watu waliokuwa hawakuwachagua
 
jiulize wale wote waliokuwa wanapinga barakoa na chanjo ila sasa wanavaa barakoa na chanjo wamepiga.
Inasikitisha sana mishipa ya shingo iliwatoka mpaka wanaoga nyungu mbele ya makamera. Leo wamegeuka kama vile sio wao
 
WAMACHINGA WAONDOKE. HII NCHI HAIWEZI KUENDESHWA KAMA KUNDI LA WAHUNI. YANI KABISA MTU AFANYE BIASHARA KWENYE ENEO LA HIFADHI YA BARABARA? KUWENI NA AIBU
Wawaondoshe hao wahuni wanaotumika kisiasa kila miaka
 
Nan atetee mTanzania...mimi binafsi kura nitazitafuta hata kwA magoti ,alaf nikifika tu juu Napenda kuzipiga kisawasawa..Wakina Mdee ,Matiko ,Mbowe na walipigwa hadi vidole na kudhalilishwa na kuvunjwa mikono ,watu wakaishia kusambaza clip tu na kusikitika...wenyewe wakaona ujinga wakaamua kujipigia... Silaa alijitahidi kuraise hoja ya wabunge kulipa kodi ,waTz tukaishia kucheka kisa alikuja na mavitabu kipindi cha utetezi 🤣🤣🤣🤣

Mi naona njia pekee ya sisi kujitambua ni waendelee kututafuna tu Ili siku moja kila mmoja achoke🤣🤣
Tunakaribia kuchoka. Huko ccm chama la nyumbani kumechoka vibaya kila mtu analalamika. Tuendelee hivi hivi.
 
Kwanza katika suala la wamachinga, wananchi wenyewe wamegawanyika mara mbili, wapo wananchi ambao wanataka wamachinga waondolewe mjini kwa kuwa wanacahfu mjini bila kujiuliza mji msafi wa nini wakati hauna amani.
Wengine wanataka wamachinga wabaki mjini na biashara zao huku taswira ya mji ikiwa haieleweki.
Somo linalopatiklana hapo kulingana na hizo pande mbili, ni kujikuta sasa watanzania bila ya kufichana tumeingia katika zama kuweza kujigawa pande mbili.
Sisi wenyewe raia hatujuia cha kufanya, ndo wabunge na wao wanafanya kinachowahusu.
 
Ifike wakati tuwe na Taasisi imara kuliko kutegemea maono ya mtu mmoja! Leo akija kiongozi mwingine atakuja na mtazamo tofauti juu ya wamachinga. Hivyo basi tutaishi kwa kuyumbishwa kutokana tu na maono ya kiongozi fulani na walio chini yake wataunga mkono kwa ajili ya maslai yao binafsi.

Nasikia wamachinga wanaviongozi wao, na kama kweli ni viongozi wa kweli watakuwa na tija ya kweli ya kumaliza tatizo hili bila kuongeza migogoro mingine, kama wamewekwa kufuata maono ya mtu! Wataendelea kupelekwapelekwa tu. Binafsi nafikiria mambo haya;

(i) Viongozi wa Machinga kujitokeza hadharani- kuongea na vyombo vya habari, kuhusisha mashirika ya haki za binadamu katika maongezi yao. Kuiomba serikali kusitisha zoezi mpaka watakapo kaa mezani kutafuta njia muafaka ya jambo lao.

(ii)Maandamano- Ni njia nzuri ya kufikisha kilio chao sehemu husika, njia hii imekuwa na msaada mkubwa sehemu mbalimbali Duniani na itumike pale tu njia ya majadiliano imeshindwa kuzaa matunza mazuri kwa pande zote. Miaka ya nyuma ilisaidia sana katika Taasisi na Mashirika mbalimbali lakini kwa sasa imekuwa na changamoto kubwa hapa kwetu, ila wakiweza itawashtua na kuwakumbusha wajibu wao hasa Wabunge, Madiwani na viongozi wengine.

ZINGATIA- Mpangilio mzuri unaitajika kwa ajili ya kufanya biashara vizuri bila kukera watu wengine, sehemu nyingine wamejaa barabarani hata kupita na gari au kwa miguu ni kero na kuna mazingira mengine hawaitajiki kutokana umuhimu wa eneo.
Well said
 
Kwanza katika suala la wamachinga, wananchi wenyewe wamegawanyika mara mbili, wapo wananchi ambao wanataka wamachinga waondolewe mjini kwa kuwa wanacahfu mjini bila kujiuliza mji msafi wa nini wakati hauna amani.
Wengine wanataka wamachinga wabaki mjini na biashara zao huku taswira ya mji ikiwa haieleweki.
Somo linalopatiklana hapo kulingana na hizo pande mbili, ni kujikuta sasa watanzania bila ya kufichana tumeingia katika zama kuweza kujigawa pande mbili.
Sisi wenyewe raia hatujuia cha kufanya, ndo wabunge na wao wanafanya kinachowahusu.
penye mgawanyiko wa kusettle mambo ni viongozi
 
Kweli unaamini tuna Wabunge? Au Genge la wahuni wa CCM? Waliwekwa pale kwa maana Fulani ili mpira uongezwe muda kutoka dakika 90 za kawaida hadi ikiwezekana Dakika 450./ila Mungu fundi nyie....
Yule kichaa ambaye Dialo alimsema angejiongezea muda hata penalti zote angepiga mwenyewe
 
Wabunge wa CCM hawana sababu yoyote ya kuwatetea Machinga kwasababu wanajua waliingia na wataingia tena bungeni kwa kura feki kama walivyofanya October 2021.
 
Ukwel Ni huu hatuna kiongozi wa ngazi yoyote ambae anazungumza lugha inayozungumzwa na watu, kimsingi shule ipo mbali na Kijiji[emoji125][emoji125]
 
Back
Top Bottom