Wachawi tukutane hapa

Wachawi tukutane hapa

Wapo wachawi wanaologa kwa visasi au sababu wanazozijenga wenyewe katika bongo zao anaweza akakuchukia tu bila sababu ya msingi au sababu anazozijua yeye na akaamua kukuloga huku SUMBAWANGA ndo mkoa unao ongoza kwa vichaa (watu wasiokuwa na akili timilifu) huku ukiwa tajiri unalogwa ndo mana matajiri wa huku SUMBAWANGA wengi ni wageni(waliotoka mikoa mingine)

Binafsi mimi sio mzawa wa SUMBAWANGA ila nimekulia tu huku uchawi naujua vizuri.
Nina mashaka na wewe unaposema kuna vichaa wengi sumbawanga na suala la matajiri wenyeji kulogwa.
Ukiwa sumbawanga huwezi mjua mchawi.
Unaweza ukawa mchawi ama usiwe mchawi yote yanawezekana lakini nakutahadharisha acha kutuchafua wafipa na kutudhalilisha sampuli hii.
Waweza ukaona uko sawa kusema uwezavyo but mind that kuheshimiana ni kuzuri.
Kama wewe ni mtani wa wafipa jitambulishe hivyo ueleweke lakini si kwa style hii.
Mahali kwingine ukisema mimi ni mfipa tu waweza watapeli watu hadi wakakoma, natoa tahadhari kuweni makini na watu wanaotumia kiki ya kujiita wafipa kwa kiki ya uganga huku hata lugha hawaijui kabisa. Uchawi na uganga ni tofauti. Si kila mchawi ni mganga na si kila mganga ni mchawi. Kuna mganga na kuna mchawi, mwenye fani zote aweza kuwepo but rarely this to be.
Mungu anatujua sote na akili zetu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom