Wachawi tukutane hapa

Wachawi tukutane hapa

Ungo wangu umepata hitilafu nipo mahenge huku gereji nautengeneza
Sie kwetu hatutumii ungo kupaa... Kuna wale ambao wanatumia pembe maalum wanachomeka kunako kijambio wanapaa. Mimi ninatumiaga fagio huwa halinipi usumbufu kwa safari ndefu, ila kwa visafari vidogo kama kuchezea watu hapa maeneo ya jiran natumia fisi a. k. a. uber... [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Toka enzi na enzi uchawi upo mkuu mababu na mababu waliutumia kama jadi yao na uliwanufaisha kwa namna moja au nyingine na zipo mila na desturi za kichawi kwaiyo kuitambua asili ya uchawi itakuwa ngumu mkuu mf. NIGERIA kule naweza sema ndio chimbuko halisi la uchawi kila kabira kunauchawi mkuu na asili ni mababu zetu wa kale.
Hata kwenye biblia wachawi tumeandikwa tupo.
 
wajameni swamahani sana kwa kuingia mlango huu mimi sio mchawi na ndo maana nimeingia kinyumenyume.!
mie sikai ila nawaomba tu mnifanyie mpango kuhusu haka kabiashara kangu ka majeneza na sanda kaende vizuri hasa haya maeneo niliyopo ili ikiwezekana nami niongeze hata kagari ka pili tofauti na haka nilikonunua(kanakofanana na kale ka Mr.Bean)
ni hayo tu mie natoka.
Cc:Mshana Jr
 
Sie kwetu hatutumii ungo kupaa... Kuna wale ambao wanatumia pembe maalum wanachomeka kunako kijambio wanapaa. Mimi ninatumiaga fagio huwa halinipi usumbufu kwa safari ndefu, ila kwa visafari vidogo kama kuchezea watu hapa maeneo ya jiran natumia fisi a. k. a. uber... [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
Eh eh mchawi mwe maendeleo eti uber....
 
Hivi ukiwa mchawi ni lazima ule nyama za watu,kunywa damu,kula maiti,kufuga misukule,kuroga watu na kuua watu,hivi vitu haviepukiki katika uchawi?.je mtu anaweza kuwa mchawi asifanye vitu hivi?
uchawi uko wa aina nyingi kunablack magic na white magic,sikuhizi uchawi unafanyika hadharan kwa nchi zilizoendelea,kama vile ktk american got talent,wachawi wanashindan hadharani kuonyesha uwezo wao ili wapata kipato,nguvu ya uchawi si lazima ule nyama ya mtu au damu,ni vile unavyoweza kucontrol nguvu yako ya asili na kuweza kuitumia
 
Naomba niwauliza nyie wachawi... Eti nikweli ukiacha mlango wazi ni vigumu nyinyi kuingia ndani, na kwanini kama mnaeza kupitia ukutan ukaingia ndani kwann usi njigi njigi warembo wote wa kitaa
unaweza fanya mapenzi na watu pasipo kujijua ila shida utamu utakuw tofauti kwani mmoja atakuw ktk ulimwengu wa kiroho na mwingine halisi
 
MBONA HAMUIBI HERA BENKI MKAACHANA NA UFUKARA?KWANINI WACHAWI WENGI NI VIZEE NA MASKINI?
wachawi ni matajiri sana,ila wanatofautiana uwezo,ukiona mchawi masikini ujue amerithishwa teknolojia ndogo,hivy haimsaidii kwa kipato zaidi ya kurudisha maendeleo ya watu nyuma
 
Mkuu ni kweli kabisa kuna rafiki yangu mwanae anasoma shule fulani ipo Tanga yupo form2,mtihani wa kuingia form2 alikuwa wa kwanza kapewa zawadi shuleni,alipokwenda kuanza term ya kwanza form2 kaanza kupagawa na mapepo hadi ninapoandika hapa bado hajakaa sawa!sasa sijui kama ndo wamefanya yao!ila tupo kwenye maombi mazito maana giza halijawahi kuishinda nuru!
dawa ya mchawi ni mchawi mwenzie
 
Back
Top Bottom